Translate

Friday, November 2, 2012

wananchi Mbeya wafunga barabara kwa masaa sita ,ni kutokana na kugongwa watu zaidi ya 30 wakiwemo watoto wawili wa chekechea


Na Thompson Mpanji,Mbeya

MATUKIO ya ajali yameendelea kuundama Mkoa wa Mbeya  baada ya wananchi  wa Kijiji cha Imezu  kata ya Inyala  wilaya ya Mbeya Vijijini  leo kulazimika kufunga bara bara ya  Mbeya  Dar es Salaam kwa takribani saa sita baada ya kutokea ajali iliyoua watoto  wawili wa chekechea  wanaokadiriwa kuwa na umri wa miaka mitano mpaka sita.

Kamanda wa kikosi cha usalama barabarani  Mkoa wa Mbeya (RTO) Butusyo Mwambelo amewataja Watoto hao kuwa ni ,Timotheo  Omary (5) na Thadeo Braiston  Malila (5)  ambapo kati ya watoto hao mmoja tayari mazishi yake yamefanyika  na mwili wa mtoto mwingine utasafilishwa  kwenda kijiji cha uwanji Matamba Wilayani Makete.

Amesema kuwa tukio hilo  limetokea  majira ya saa 1.15 asubuhi baada ya watoto hao kugongwa na gari aina ya  yenye namba  za usajili T 798 BVY  tela  T698  BVA lilokuwa kiendeshwa na  Dominick  Mwakalundwa (34) mabibo dar e s salaam lililokuwa likitokea Mbeya  kwenda Mkoani Iringa liligonga watoto  hao waliokuwa pembeni ya bara bara wakitoka shule na kwamba aliokolewa na askari Polisi baada ya wananchi kutaka kumshambulia..

Wakizungumza na  Radio five na matukio  katika eneo la ajali hiyo Wananchi hao,  wamesema kuwa waliamua kuchukua  uamuzi huo  baada ya kuchoshwa na ahadi za serikali kupitia wakala wa bara bara  za kuweka matuta  katika eneo hilo la la shule  ili kuepusha ajali ambazo zimekuwa zikitokea mara kwa mara .

Bw.Michael Mashamba mkazi wa kijiji cha Imezu amesema kuwa baada ta tukio hilo kutokea wananchi walijaa eneo la ajali  na kuanza kufunga  bara bara kwa kutumia magogo na mawe  ili kuzuia magari yasipite eneo hilo kwa lengo la kushinikiza serikali kuweka matuta ili kuzuia ajali kutokana na madai ya kufariki watu zaidi ya 30 kwa ajili katika maeneo hayo.

 Hata hivyo baada ya tukio hilo Mkuu wa Wilaya ya Mbeya Dkt. Norman  Sigalla  aliwaomba wananchi  kufungua bara bara wakati serikali  kwa kushirikiana na wakala wa bara bara (TAN ROADS) ikiwa inaweka utaratibu  wa kuweka matuta hayo haraka iwezekanavyo.

Aidha Sigalla ameliagiza jeshi la polisi  Mkoani hapa kuwachukulia hatua  kali madereva watakoendesha  magari kwa mwendo kasi  na kwamba watozwe faini na adhabu kali ambayo itawafanya wawe na nidhamu  na askari wasiwe marafiki wa madereva.
Mwisho

No comments:

Post a Comment