Translate

Monday, November 26, 2012

kuhusu sakata la Mbegu feki Mbozi,wakulima wapewa somo na mtafiti


Na Thompson Mpanji,Mbeya
 
WAKULIMA nchini wameshauriwa kujenga utamaduni wa kudai lisiti wakati wa kununua mbegu za mazao ya aina mbalimbali katika maduka ya pembejeo yanayotambulika ili kuepuka kuuziwa mbegu feki ambazo zimetapakaa na kuwaletea hasara kubwa wakulima walio wengi sanjari na kuhatarisha maisha ya walaji.
 
Aidha imeleezwa kuwa mbegu za mahindi ya njano ambazo zinadaiwa kutoa unga wa njano baada ya kusagwa zinazodaiwa kusambazwa kwa wakulima walio wengi wilayani Mbozi zinatumika kwa ajili ya malisho ya mifugo na siyo kwa binadamu.
 
Akizungumza na gazeti hili Mtafiti wa zao la mahindi kutoka taasisi ya utafiti kanda ya nyanda za juu kusini (ARI Uyole), Anderson Elibariki Temu alisema mbegu za mahindi zenye rangi ya njano ni mojawapo ya aina inayopendelewa sana nchini Marekani na imekuwa ikitumika kwa ajili ya vyakula vya kuku na ng’ombe wa maziwa.
 
Mtafiti huyo alisema ingwa hajabahatika kuyaona mahindi hayo yanayozungumziwa lakini kutokana na maelezo aliyoyapata ana uenda yalizalishwa kwa ajili ya mifugo na siyo kwa ajili ya chakula cha binadamu.
 
"Lakini nawashauri wakulima kwa kuona tatizo hilo na mbegu hazijifichi inatakiwa wakulima wawe makini wawe waangalifu wakati wa kununua mbegu kwa sababu hii imekuwa ni kero kubwa kwa wakulima wa kanda ya nyanda za juu kusini na Tanzanja kwa ujumla Mkulima anapojitahidi kuwa na mtaji hadi kununua mbegu, anaipanda,gharama za mbolea ,maandalizi ya shamba na gharama nyingine alafu mwisho anaikuta mbegu aliyoipanda kwa mfano siyo Uyole Hybrid 615 ni hasara kubwa,"alisema.
 
Temu alisema ili mkulima aweze kukwepa udanganyifu huo anapaswa anapoenda kununua mbegu ahakikishe mbegu ipo kwenye mifuko ya kampuni halisia inayozalisha hiyo mbegu mfano kampuni inayozalisha mbegu za uyole ya Highland seed growers ambapo nje ya mfuko kuna anuani na jina la kampuni,na kwamba akwepe kununua mbegu zinazouzwa baada ya kufunguliwa katika mfuko .
 
Alisema Mkulima naweza kununua mbegu iliyokuwepo katika mifuko kwa sababu wanaweza kuiba mifuko ama kutumia ujanja wowote,kwa hiyo njia ya mwisho ya kuwabana wauzaji wa mbegu feki ni kudai lisiti na kuitunza hadi wakati wa msimu wa amvuno.
 
"ili tatizo likijitokeza la mbegu kutokuwa halisi nenda kwa ofisa shamba ukikutana na tatizo atakuelekeza ngazi na utaratibu wa kufuata ili mhusika weze kufuatiliwa na ikibidi sheria ichukuwe mkondo wake kwa sababu sheria zipo kuanzia kuzalisha mbegu kuhakikisha zina ubora na mamlaka husika zinazofuatilia zipo,hakikisha una lisiti hadi mwisho wa msimu,"alisisistiza Mtafiti huo.
 
Mwisho.

No comments:

Post a Comment