Na Thompson Mpanji,Mbeya
ASKARI 10 wa Jeshi la wananchi (JWTZ) kikosi
cha 44kj Mbalizi,wanashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa tuhuma za mauaji
na kujeruhi watu wengine sita sanjari na kuharibu mali mbalimbali.
Kamanda wa polisi Mkoa wa Mbeya,Diwani
Athumani amethibitisha kutokea kwa kifo hicho Nov,18 majira ya saa 5 usiku katika hospitali teule ya Ifisi wilaya ya
mbeya vijijini mkoa wa mbeya na amemtaja marehemu kuwa ni Petro Sanga,( 25),mkulima,mkinga,
mkazi wa chapakazi, mbalizi ambaye alifariki dunia wakati akiendelea kupatiwa
matibabu hospitalini hapo.
Athuman amesema marehemu alichomwa kisu shingoni na mdomoni na
kikundi cha watu wanaosadikiwa kuwa askari
wa jeshi la wananchi wa Tanzania, tarehe hiyo majira ya saa 3 usiku akiwa katika
grocery iitwayo vavene mwe iliyopo mbalizi mara baada ya watu hao kuvamia bar iitwayo power night club
ambamo awali alikuwepo pia marehemu.
Amesema watu wengine sita walijeruhiwa kwa kupigwa sehemu mbalimbali za
miili yao na wanaodaiwa kuwa askari wa JWTZ
na kupatiwa hati ya matibabu [pf3] kwa matibabu kati yao watatu walilazwa
katika hospitali teule ya ifisi kwa matibabu zaidi na majeruhi wengine watatu walipatiwa matibabu na
kuruhusiwa.
Kamanda huyo amesema kufuatia vurugu hizo baadhi ya mali za watu
ziliharibiwa ambazo ni pamoja gari T.106 AWB aina ya toyota vista mali ya Paulo
Maximilian ilivunjwa kioo cha mbele,gari T.884 AUU Toyota Cresta mali ya Alile
Godfrey lilivunjwa side mirror upande wa kulia.
Kamanda huyo amesema kuwa wahalifu hao walianza kuwashambulia wananchi
kwa kuwapiga wakitumia ngumi, mateke, mikanda, marungu, sime na mapanga na
kwamba marehemu alijaribu kuokoa uhai wake kwa kukimbia toka
eneo hilo hadi katika grosary hiyo
lakini watu hao walimkimbiza hadi eneo hilo na kumjeruhi vibaya kwa kumchoma
kisu.
Amesema chanzo cha tukio hilo ni kulipiza
kisasi kufuatia askari Godfrey Matete( 30),mjita, wa kikosi cha 44kj mbalizi
kupigwa na walinzi wa kilabu cha pombe za kienyeji kiitwacho DDC kilichopo
mbalizi waliokuwa lindoni Nov,17,2012
majira ya saa 01:30.
Amefafanua kuwa baada ya kushambuliwa askari huyo alifungua kesi kituo cha polisi
mbalizi usiku huo kosa la kujeruhi na alipatiwa
hati ya matibabu [pf3] kwa ajili ya kwenda kupata matibabu hospitalini ambapo walinzi
wanne walikamatwa kuhusiana na tukio
hilo kwa mahojiano.
Amewataja walinzi hao kuwa ni Frenk
Mtasimwa (25),Mure Julias (26),Omari Charles (28) wote wakazi wa DDC mbalizi na Legnard Mwampete (30),mkazi wa Izumbwe na
kwamba upelelezi wa kesi hiyo bado
unaendelea.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment