Translate

Friday, January 31, 2014

Mmachinga mbaroni kwa kumbaka ng'ombe

Na Thompson Mpanji
 
KIJANA mmoja mfanyabiashara ndogo ndogo almaarufu Machinga,mkazi wa Ntokela,Wilaya ya Rungwe amekamatwa na Jeshi la Polisi katika kituo kidogo cha polisi Kiwira  leo kwa tuhuma za kumwingilia mnyama aina ya ng'ombe  usiku wa kuamkia leo kinyume na maumbile akidai ni masharti aliyopewa na mganga wa jadi kuwa atakuwa tajiri kwa kupata fedha nyingi.
Mtuhumiwa  amepelekwa na ng'ombe kituoni kwa hatua zaidi,taarifa zaidi utaendelea kuipata kupitia blog hii.

Sunday, January 19, 2014

baraza jipya la mawaziri-2014 latangazwa leo

THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
Telephone: 255-22-2114512, 2116898
E-mail: ikulumawasiliano@yahoo.com
press@ikulu.go.tz
Fax: 255-22-2113425
PRESIDENT’S OFFICE,
THE STATE HOUSE,
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL
COMMUNICATIONS,
P.O. BOX 9120,
DAR ES SALAAM.
Tanzania.
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
UHAMISHO NA UTEUZI WA MAWAZIRI NA NAIBU MAWAZIRI
______________________________________________
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete,
amewahamisha na kuwateua baadhi ya Mawaziri na Naibu Mawaziri kama ifuatavyo:-
1.0 OFISI YA RAIS
Hakuna mabadiliko.
2.0 OFISI YA MAKAMU WA RAIS
2.1 Waziri wa Nchi (Muungano) - Hakuna mabadiliko
2.2 Mhe. Eng. Dr. Binilith Satano MAHENGE (Mb)
Waziri wa Nchi (Mazingira).
2.3 Mhe. Ummy Ali MWALIMU (Mb)
Naibu Waziri
3.0 OFISI YA WAZIRI MKUU
Hakuna mabadiliko
4.0 WIZARA
4.1 WIZARA YA FEDHA
4.1.1 Mhe. Saada Mkuya SALUM (Mb)
Waziri wa Fedha
Mhe. Mwigulu Lameck NCHEMBA (Mb)
Naibu Waziri wa Fedha
4.1.2 Mhe. Adam Kighoma Ali MALIMA (Mb)
Naibu Waziri wa Fedha
4.2 WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA
Hakuna mabadiliko
4.3 WIZARA YA KATIBA NA SHERIA
4.3.1 Mhe. Dkt. Asha-Rose Mtengeti MIGIRO (Mb)
Waziri wa Katiba na Sheria
4.3.2 Naibu Waziri - Hakuna mabadiliko
4.4 WIZARA YA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI
Hakuna mabadiliko
4.5 WIZARA YA VIWANDA NA BIASHARA
4.5.1 Waziri - Hakuna mabadiliko
4.5.2 Mhe. Janet Zebedayo MBENE (Mb)
Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara
4.6 WIZARA YA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA
Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi (Mb)
Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa
4.7 WIZARA YA UJENZI
Hakuna mabadiliko
4.8 WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI
4.8.1 Mhe. Mathias Meinrad CHIKAWE (Mb)
Waziri wa Mambo ya Ndani
4.8.2 Naibu Waziri - Hakuna Mabadiliko
2
4.9 WIZARA YA AFYA NA USTAWI WA JAMII
4.9.1 Mhe. Dkt. Seif Seleman RASHIDI (Mb)
Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii
4.9.2 Mhe. Dkt. Kebwe Stephen KEBWE (Mb)
Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii
4.10 WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI
4.10.1 Waziri: Hakuna mabadiliko
4.10.2 Mhe. Jenista Joakim MHAGAMA (Mb)
Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi
14.11 WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO
14.11.1 Waziri: Hakuna mabadiliko
14. 11.2 Mhe. Dkt. Pindi Hazara CHANA (Mb)
Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
14.12 WIZARA YA MAENDELEO YA MIFUGO NA UVUVI
14.12.1 Mhe. Dkt. Titus Mlengeya Dismas KAMANI (Mb)
Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi
14.12.2 Mhe. Kaika Saning’o TELELE (Mb)
Naibu Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi
14.13 WIZARA YA KAZI NA AJIRA
Hakuna mabadiliko
14.14 WIZARA YA MAWASILIANO, SAYANSI NA TEKNOLOJIA
Hakuna mabadiliko
14.15 WIZARA YA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI
14.15.1 Waziri - Hakuna mabadiliko
14.15.2 Mhe. George Boniface Taguluvala SIMBACHAWENE (Mb)
Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi
14.16 WIZARA YA MAJI
14.16.1 Waziri - Hakuna mabadiliko
3
14.16.2 Mhe. Amos Gabriel MAKALLA (Mb)
Naibu Waziri wa Maji
14.17 WIZARA YA KILIMO, CHAKULA NA USHIRIKA
14.17.1 Waziri - Hakuna mabadiliko
14.17.2 Mhe. Godfrey Weston ZAMBI (Mb)
Naibu Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika
4.18 WIZARA YA UCHUKUZI
Hakuna mabadiliko
4.19 WIZARA YA HABARI, VIJANA, UTAMADUNI NA MICHEZO
4.19.1 Waziri - Hakuna mabadiliko
4.19.2 Mhe. Juma Selemani NKAMIA (Mb)
Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo
4.20 WIZARA YA MALIASILI NA UTALII
4.20.1 Mhe. Lazaro Samuel NYALANDU (Mb)
Waziri wa Maliasili na Utalii
4.20.2 Mhe. Mahmoud Hassan MGIMWA (Mb)
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii
4.21 WIZARA YA NISHATI NA MADINI
4.21.1 Waziri - Hakuna mabadiliko
4.21.2 Naibu Waziri (Madini) - Hakuna mabadiliko
4.21.3 Mhe. Charles Muhangwa KITWANGA (Mb)
Naibu Waziri (Nishati)
Balozi Ombeni Y. Sefue
KATIBU MKUU KIONGOZI
Ikulu
4
DAR ES SALAAM
19 Januari, 2014
5

Tuesday, January 14, 2014

Jan,13,2014 matukio ya uvutaji wa banghi na unywaji wa pombe haramu ya gongo yatagonga vichwa vya habari Mbeya




TAARIFA YA JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA KWA VYOMBO VYA HABARI
“PRESS RELEASE” TAREHE 14.01. 2014.

WILAYA YA MBEYA MJINI – AJALI YA PIKIPIKI KUGONGA GARI NA
                                                   KUSABABISHA VIFO.

MNAMO TAREHE 13.01.2014 MAJIRA YA SAA 04:30HRS HUKO KATIKA ENEO LA SAE, KATA YA MWAKIBETE, TARAFA YA IYUNGA, JIJI NA MKOA WA MBEYA BARABARA YA MBEYA/NJOMBE. PIKIPIKI T.436 CLP AINA YA T-BETTER IKIENDESHWA NA GABRIEL S/O NGALELE, MIAKA 24, KYUSA, MKAZI WA UYOLE   ILIGONGA KWA NYUMA GARI T.684 BVY AINA YA SCANIA LILILOKUWA LIMEEGESHWA NA DEREVA ASIYEFAHAMIKA JINA WALA MAKAZI YAKE NA KUSABABISHA KIFO CHA MWENDESHA PIKIPIKI HUYO PIA KUSABABISHA KIFO KWA ABIRIA ALIYEKUWA KATIKA PIKIPIKI HIYO AMBAYE HAFAHAMIKI JINA WALA MAKAZI YAKE JINSI YA KIKE. CHANZO CHA AJALI KINACHUNGUZWA. KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHNA MSAIDIZI MWANDAMIZI WA POLISI AHMED Z. MSANGI ANATOA WITO KWA MADEREVA KUWA MAKINI WANAPOTUMIA VYOMBO VYA MOTO KWA KUZINGATIA SHERIA NA ALAMA ZA USALAMA BARABARANI ILI KUEPUKA AJALI ZINAZOWEZA KUEPUKIKA.

WILAYA YA MBEYA MJINI – KUPATIKANA NA POMBE HARAMU YA MOSHI
                                                 [GONGO].

MNAMO TAREHE 13.01.2014 MAJIRA YA SAA 11:40HRS HUKO UYOLE VILABUNI, KATA YA IGAWILO, TARAFA YA IYUNGA, JIJI NA MKOA WA MBEYA, ASKARI POLISI WAKIWA DORIA/MSAKO WALIMKAMATA JOSEPH S/O MWAKISA, MIAKA 38, KYUSA, MKULIMA MKAZI WA NSALAGA NA WENZAKE WANNE WAKIWA  NA POMBE YA  MOSHI [GONGO] UJAZO WA LITA MOJA NA NUSU [1 ½ ]. WATUHUMIWA NI WATUMIAJI WA POMBE HIYO. TARATIBU ZA KISHERIA ZINAFANYIKA DHIDI YAO.  KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHNA MSAIDIZI MWANDAMIZI WA POLISI AHMED Z. MSANGI ANATOA WITO KWA JAMII  KUACHA TABIA YA KUTUMIA POMBE HARAMU YA MOSHI KWANI NI KINYUME CHA SHERIA NA NI HATARI KWA AFYA YA MTUMIAJI.

WILAYA YA MBEYA MJINI - KUPATIKANA NA POMBE HARAMU YA 
                                                               MOSHI [GONGO].

MNAMO TAREHE 13.01.2014 MAJIRA YA SAA 14:30HRS HUKO MWANJELWA,  KATA YA  MAANGA, TARAFA YA  IYUNGA, JIJI NA MKOA WA MBEYA, ASKARI POLISI WAKIWA DORIA/MSAKO WALIMKAMATA SUMA D/O MWAMPIKI, MIAKA 29, KYUSA, MKULIMA MKAZI WA ILOLO NA WENZAKE WANNE WAKIWA  NA POMBE YA  MOSHI [GONGO] UJAZO WA LITA MOJA NA NUSU [1 ½ ]. WATUHUMIWA NI WATUMIAJI WA POMBE HIYO. TARATIBU ZA KISHERIA ZINAFANYIKA DHIDI YAO. KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHNA MSAIDIZI MWANDAMIZI WA POLISI AHMED Z. MSANGI ANATOA WITO KWA JAMII HASA VIJANA KUACHA TABIA YA KUTUMIA POMBE HARAMU YA MOSHI KWANI NI KINYUME CHA SHERIA NA NI HATARI KWA AFYA YA MTUMIAJI.





WILAYA YA MBEYA MJINI - KUPATIKANA NA POMBE HARAMU YA 
                                                               MOSHI [GONGO].

MNAMO TAREHE 13.01.2014 MAJIRA YA SAA 14:30HRS HUKO MWANJELWA,  KATA YA  MAANGA, TARAFA YA  IYUNGA, JIJI NA MKOA WA MBEYA, ASKARI POLISI WAKIWA DORIA/MSAKO WALIMKAMATA TUKULAMBA D/O ASTON, MIAKA 30, KYUSA, MKULIMA MKAZI WA MAFIATI  AKIWA  NA POMBE YA  MOSHI [GONGO] UJAZO WA LITA TATU [03] .MTUHUMIWA NI MTUMIAJI  NA MUUZAJI WA POMBE HIYO. TARATIBU ZA KISHERIA ZINAFANYIKA DHIDI YAKE. KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHNA MSAIDIZI MWANDAMIZI WA POLISI AHMED Z. MSANGI ANATOA WITO KWA JAMII KUACHA TABIA YA KUTUMIA POMBE HARAMU YA MOSHI KWANI NI KINYUME CHA SHERIA NA NI HATARI KWA AFYA YA MTUMIAJI.

WILAYA YA MBEYA MJINI - KUPATIKANA NA BHANGI.

MNAMO TAREHE 13.01.2014 MAJIRA YA SAA 10:00HRS HUKO ITEZI, KATA YA  ITEZI, TARAFA YA  IYUNGA, JIJI NA MKOA WA MBEYA, ASKARI POLISI WAKIWA DORIA/MSAKO WALIMKAMATA FRED S/O MBOGELA, MIAKA 24, KYUSA, MKULIMA MKAZI WA UYOLE  AKIWA  NA BHANGI KETE TATU [03] SAWA NA UZITO WA GRAM 15 .MTUHUMIWA NI MTUMIAJI  NA MUUZAJI WA BHANGI HIYO. TARATIBU ZA KISHERIA ZINAFANYWA DHIDI YAKE. KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHNA MSAIDIZI MWANDAMIZI WA POLISI AHMED Z. MSANGI ANATOA WITO KWA JAMII HASA VIJANA KUACHA TABIA YA KUTUMIA DAWA ZA KULEVYA KWANI NI KINYUME CHA SHERIA NA NI HATARI KWA AFYA YA MTUMIAJI.

WILAYA YA KYELA – KUPATIKANA NA POMBE HARAMU YA MOSHI [GONGO].

MNAMO TAREHE 13.01.2014 MAJIRA YA SAA 17:30HRS HUKO KATIKA KIJIJI CHA KATUMBATUKUYU, KATA YA  IBHIGI, TARAFA YA  UKUKWE, WILAYA YA  RUNGWE, MKOA WA MBEYA, ASKARI POLISI WAKIWA DORIA/MSAKO WALIMKAMATA VICK D/O EMANUEL, MIAKA 20, KYUSA, MKULIMA MKAZI WA KATUMBA  AKIWA  NA POMBE YA  MOSHI [GONGO] UJAZO WA LITA MBILI [02]. MTUHUMIWA NI MTUMIAJI NA MUUZAJI WA POMBE HIYO. TARATIBU ZA KISHERIA ZINAFANYWA DHIDI YAKE.  KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHNA MSAIDIZI MWANDAMIZI WA POLISI AHMED Z. MSANGI ANATOA WITO KWA JAMII  KUACHA TABIA YA KUTUMIA POMBE HARAMU YA MOSHI KWANI NI KINYUME CHA SHERIA NA NI HATARI KWA AFYA YA MTUMIAJI.


Signed by:
[AHMED Z. MSANGI – SACP]
KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA.




Monday, January 13, 2014

Wawili wasakwa kwa mauaji Kyela na Momba,Mbeya

Na Thompson Mpanji,Mbeya

WATU wawili wanasakwa na Jeshi la polisi kwa udi na uvumba  ili waweze kupandishwa kwa pilato baada ya kutuhumiwa kufanya mauaji katika matukio mawili tofauti Wilaya ya Kyela na Momba,mkoani Mbeya.

Katika tukio la kwanza Bicco Mwakibibi (28),Mkazi wa kijiji cha Lema,Kata ya Ngana,Tarafa ya Tembela,Wilaya ya Kyela,mkoani Mbeya  aliuawa  kwa kupigwa na silaha za jadi,mawe na fimbo sehemu mbalimbali za mwili wake  na kundi la wananchi.

Imeelezwa kuwa tukio hilo limetokea Januari,12,2014 majira ya saa 11.00 alfajiri  baada marehemu na mwenzake  ambaye jina lake halikuweza kufahamika mara moja kuvunja kibanda cha biashara  na kuiba  ambapo wananchi walijichukulia sheria mkononi na kwamba mwenzake alikimbia baada ya tukio hilo.

Kamanda wa Polisi mkoani Mbeya,Kamishana msaidizi mwandamizi,Ahmed Msangi amethibitisha tukio hilo  na kwamba juhudi za kumtafuta kijana aliyekimbia zinaendelea  na ameionya jamii kuacha kujichukulia sheria mkononi.

Katika tukio la pili, kijana Bonny Silumbe,Mkazi wa Kijiji cha Kapele,Tarafa ya Ndalambo,Wilaya ya Momba,mkoani Mbeya anatafutwa na Jeshi la Polisi kwa tuhuma za kumuuwa kaka yake Adamu Silumbe(27) baada ya kumchoma kisu mgongoni na kufariki dunia akiwa anapatiwa matibabu katika Hospitali ya wilaya ya Mbozi.

Kamanda Msangi amethibitisha kutokea kwa tukio hilo  januari,12,2014 majira ya saa 3.30 usiku  na ameonya wananchi kuacha tabia ya kujichukulia  sheria mkononi.

Mwisho.

Sunday, January 12, 2014

mauaji mbeya



TAARIFA YA JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA KWA VYOMBO VYA HABARI
“PRESS RELEASE”TAREHE 09.01. 2014.

WILAYA YA ILEJE – MAUAJI.

WATU wawili wakazi wa Kitongoji cha Lupungu,Kijiji cha Ikinga,Kata ya Ikinga,Tarafa ya Bundali,Wilaya ya Ileje,mkoani Mbeya wanashikiliwa na Jeshi la polisi  kwa tuhuma za mauaji.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Kamishna msaidizi Mwandamizi wa polisi,Ahmed Msangi amesema watuhumiwa hao Laison Mshani(55), na Queen Minga(40) walitenda kosa hilo Januari,7,2014  baada ya kumkata kwa mapanga kichwani na sehemu mbalimbali  za mwili wake  Francis Mshani(30) kisha kumchoma moto kuanzia kwenye magoti hadi kichwani.

Amefafanua kuwa marehemu  alitoka kifungoni  gerezani  mwezi Novemba,2013 kwa kosa la kumjeruhi mtalaka  wake na kwamba chanzo cha mauaji hayo bado hakijafahamika.

Hata hivyo Kamanda ameendelea kutoa wito  kwa jamii kuacha tabia  ya kujichukulia sheria mkononi kwani madhara yake ni makubwa  na badala yake watumie njia za busara katika kutatua migogoro ya kifamilia na kijamii kwa ujumla.

Wakati huo huo,Mtu mmoja  aliyefahamika kwa jina la Dastan Gama(38),Mfanyabiashara Mkazi wa Songea,mkoani Ruvuma anashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa kosa la kukutwa na vipodozi vilivyopigwa marufuku  na serikali.

Kamanda msangi amesema mtuhumiwa  alikamatwa Januari,8,2014 majira ya saa 10.30 mchana  huko maeneo ya Ifisi,Kata ya Utengule,Tarafa ya usongwe,Wilaya ya Mbeya vijijini  ambapo askari polisi wakiwa katika doria  walifanikiwa kumkata Dastan  akiwa na  Sabuni boksi mbili,Carolight ndogo dazani nne,Epictem 10,Extra Crela dazani mbili,Diplozoni dazani 17,Movey dazani nne,soft touch dazani nne na Lemovet boksi tatu.
Mwisho.

matukio ya uhalifu mwaka 2013





TAARIFA YA JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA KWA VYOMBO VYA HABARI
“PRESS RELEASE” KUHUSIANA NA HALI YA UHALIFU KWA MWAKA, 2013.

§         JUMLA YA MAKOSA YOTE YA  JINAI YALIYORIPOTIWA KATIKA KIPINDI CHA MWAKA 2013 YALIKUWA NI 22,262 IKILINGANISHWA NA MAKOSA 29,722 YALIYORIPOTIWA KIPINDI KAMA HICHO MWAKA 2012.
§         KATI YA MAKOSA HAYO MAKOSA MAKUBWA YALIKUWA 2,213 WAKATI KIPINDI KAMA HICHO MWAKA 2012 MAKOSA MAKUBWA YALIKUWA 2,283.
§         MAKOSA YATOKANAYO NA JITIHADA ZA JESHI LA POLISI KWA KUSHIRIKIANA NA WANANCHI NA WADAU WENGINE KUPITIA MISAKO/DORIA KWA MWAKA 2013 YALIKUWA 430, WAKATI KIPINDI KAMA HICHO MWAKA 2012 YALIKUWA 416.
§         KWA UPANDE WA MAKOSA YA USALAMA BARABARANI, JUMLA YA MAKOSA  YOTE YA  AJALI PAMOJA NA UKIUKWAJI WA SHERIA ZA USALAMA BARABARANI YALIKUWA 46,565, WAKATI KIPINDI KAMA HICHO MAKOSA 54,304 YALIRIPOTIWA.
§         MATUKIO YA AJALI KWA MWAKA 2013 YALIKUWA 490, WAKATI KIPINDI KAMA HICHO MWAKA 2012 YALIKUWA 606.
§         AJALI ZILIZOSABABISHA VIFO MWAKA 2013 ZILIKUWA 276, WAKATI KIPINDI KAMA HICHO MWAKA 2012 ZILIRIPOTIWA AJALI 606.
§         WATU WALIOKUFA KUTOKANA NA AJALI MWAKA 2013 WALIKUWA 329, WAKATI KIPINDI KAMA HICHO MWAKA 2012 WALIKUFA WATU 323.
§         AJALI ZA MAJERUHI MWAKA 2013 ZILIKUWA 214, WAKATI KIPINDI KAMA HICHO MWAKA 2012 ZILIRIPOTIWA AJALI 352.
§         WATU WALIOJERUHIWA KATIKA AJALI MBALIMBALI MWAKA 2013 WALIKUWA 649, WAKATI KIPINDI KAMA HICHO MWAKA 2012 WALIKUWA WATU 875.
§         PESA  ZILIZOKUSANYWA KUTOKANA NA MAKOSA MBALIMBALI YA  UKIUKWAJI WA SHERIA ZA USALAMA BARABARANI [NOTIFICATION] MWAKA 2013 ZILIKUWA TSHS 1,219,020,000/= WAKATI KIPINDI KAMA HICHO MWAKA 2012 ZILIKUSANYWA PESA TSHS 1,440,150,000/=
§         BAADHI YA  SABABU ZA KUONGEZEKA KWA MATUKIO YA  AJALI NI KUONGEZEKA KWA VYOMBO VYA USAFIRI MKOANI MBEYA HASA MAGARI NA PIKIPIKI, BAADHI YA  MADEREVA KUTOKUZINGATIA SHERIA ZA USALAMA BARABARANI IKIWA NI PAMOJA NA MWENDO KASI HASA USIKU NA ULEVI  LICHA YA  JITIHADA ZA JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA KWA KUSHIRIKIANA NA BAADHI YA  WADAU KUTOA ELIMU HIYO MARA KWA MARA PAMOJA NA HALI YA  HEWA HUSUSANI UKUNGU NA UTELEZI KATIKA BAADHI YA  MAENEO YA  BARABARA YA  MBEYA/RUNGWE/KYELA.
§         BAADHI YA  MAFANIKIO AMBAYO JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA KWA KUSHIRIKIANA NA WANANCHI YAMEPATIKANA NI PAMOJA NA :-

v     KWA UJUMLA HALI YA UHALIFU MKOA WA MBEYA KWA MAKOSA YOTE YA JINAI  MAKUBWA NA MADOGO UMEPUNGUA KWA ASILIMIA 25.

v     MATUKIO YA AJALI YAMEPUNGUA KWA ASILIMIA 19.

v     POMBE HARAMU YA MOSHI [GONGO] UJAZO WA LITA 583 NA MITAMBO MINNE ILIKAMATWA.

v     BHANGI YENYE UZITO WA KILO 1,096 NA GRAM 786 PAMOJA NA MASHAMBA MAWILI YENYE UKUBWA WA EKARI MOJA NA NUSU ILIKAMATWA.
v     MIRUNGI UZITO WA KILO 1 NA GRAM 500 ILIKAMATWA.
v     MADAWA YA KULEVYA KILO 1 NA GRAM 404.6 YALIKAMATWA.
v     SILAHA /BUNDUKI 35 ZILIKAMATWA KATI YA HIZO SMG 3,S/GUN 5,GOBOLE 21,SAR 1,BASTOLA ZILIZOTENGENEZWA  KIENYEJI 3 NA RIFFLE 2.
v     JUMLA YA RISASI 193 ZILIKAMATWA, KATI YA HIZO RISASI 38 ZA SMG/SAR, RISASI 130 ZA S/GUN NA RISASI 25 ZA BASTOLA.
v     SARE ZA JWTZ “KOMBATI” SURUALI 4, MASHATI 4, KOFIA 3 NA VIATU /MABUTI JOZI MBILI ZILIKAMATWA.
v     JUMLA YA SILAHA AINA YA GOBOLE 174 ZILISALIMISHWA MAENEO MBALIMBALI WILAYA YA CHUNYA KUFUATIA AGIZO LA KAMATI YA  ULINZI NA USALAMA WILAYA HIYO KUAGIZA WAMILIKI WOTE WA SILAHA HIZO KUFANYA HIVYO.
v     NYARA ZA SERIKALI ZENYE THAMANI YA TSHS 103,362,00/= NA USD 4,445 ZILIKAMATWA.
v     NOTI BANDIA 1,521 @TSHS 10,000/= SAWA NA TSHS 15,210,000,NOTI 19 @ TSHS 5,000/= SAWA NA TSHS 95,000/= NA DOLA  70 ZA KIMAREKANI @ DOLA 100 SAWA NA DOLA 7,000 ZILIKAMATWA.

PAMOJA NA MAFANIKIO HAYO LAKINI PIA KUNA BAADHI YA CHANGAMOTO ZINAZOLIKABILI JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA. CHANGAMOTO HIZO NI PAMOJA NA:-

-          KUONGEZEKA KWA MATUKIO YA MAUAJI KWA ASILIMIA 10 IKILINGANISHWA NA KIPINDI KAMA HICHO MWAKA 2012. ONGEZEKO HILO LINATOKANA NA KUKITHIRI KWA MAUAJI YA IMANI POTOFU ZA KISHIRIKINA NA KUJICHUKULIA SHERIA MKONONI [WIZI] PIA KUTOKANA NA HALI NGUMU YA KIUCHUMI. AIDHA KATIKA KIPINDI CHA MWAKA 2013 KULITOKEA MATUKIO MATATU YA WATU WANNE KUUAWA KWA KUZIKWA WAKIWA HAI KUTOKANA NA IMANI POTOFU ZA KISHIRIKINA [UCHAWI].

-          KUONGEZEKA KWA MATUKIO YA KUBAKA KWA ASILIMIA 64 IKILINGANISHWA NA KIPINDI KAMA HICHO MWAKA 2012. SABABU ZA KUONGEZEKA NI PAMOJA NA TAMAA ZA KIMWILI, ULEVI NA HALI NGUMU YA KIUCHUMI.

-          KUONGEZEKA KWA MATUKIO YA WIZI WA PIKIPIKI KWA ASILIMIA 56 IKILINGANISHWA NA KIPINDI KAMA HICHO MWAKA 2012. SABABU IKIWA NI PAMOJA NA TAMAA YA KUJIPATIA KIPATO KWA NJIA HARAMU.











WITO WA KAMANDA:

KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHNA MSAIDIZI MWANDAMIZI WA POLISI AHMED Z. MSANGI ANATOA PONGEZI KWA  WANANCHI WOTE WA MKOA WA MBEYA KWA USHIRIKIANO WAO WA DHATI KWA JESHI LA POLISI KATIKA MAPAMBANO DHIDI YA  UHALIFU NA WAHALIFU KUPITIA DHANA YA  ULINZI SHIRIKISHI NA POLISI JAMII KATIKA KIPINDI CHOTE CHA MWAKA 2013. AIDHA ANATOA RAI KWA JAMII KUENDLEA KUSHIRIKIANA NA JESHI LA POLISI KATIKA KIPINDI CHA MWAKA 2014.

PIA KAMANDA MSANGI ANATOA WITO KWA JAMII HASA WAHALIFU KUACHA TABIA YA KUWA NA   TAMAA YA UTAJIRI WA HARAKA KWA NJIA YA  MKATO/HARAMU BADALA YAKE WAJISHUGHULISHE KWA KUFANYA KAZI HALALI NA KUPATA KIPATO HALALI KWA KUZINGATIA MKOA WA MBEYA UNAZO FURSA NYINGI ZA KIUCHUMI IKIWA NI PAMOJA NA HALI YA  HEWA. ANATOA RAI PIA KWA VIONGOZI WA MADHEHEBU YA DINI, VIONGOZI WA SERIKALI, VYAMA VYA SIASA, MACHIFU, WAZEE WA MILA NA WATU MASHUHURI MKOANI MBEYA KUSHIRIKIANA NA JESHI LA POLISI KWA KUTOA ELIMU ZAIDI KWA JAMII ILI IEPUKANE NA IMANI POTOFU ZA KISHIRIKINA. AMEWATAKA PIA MADEREVA  KUENDESHA VYOMBO VYA MOTO KWA KUZINGATIA SHERIA NA ALAMA ZA USALAMA BARABARANI ILI KUEPUKA AJALI ZINAZOWEZA KUEPUKIKA KWANI ZINARUDISHA NYUMA MAENDELEO YA JAMII NA HATA NGUVU KAZI YA  TAIFA.

PIA ANATOA SHUKRANI KWA VYOMBO VYA HABARI VYA NDANI NA NJE YA MKOA WA MBEYA KWA USHIRIKIANO WENU NA KUWATAKA KUENDELEA NA HALI HII KWANI IMELETA MAFANIKIO MAKUBWA KATIKA KUFIKISHA HABARI KWA WAKAZI WA MBEYA NA TAIFA KWA UJUMLA. AIDHA NATOA WITO KWA WAANDISHI WA HABARI KUFUATA NA KUZINGATIA MAADILI YA UANDISHI WA HABARI [MEDIA ETHICS] ILI KUTOPOTOSHA UMMA NA KUEPUKA MADHARA KATIKA JAMII NA TAIFA.


MWISHO KAMANDA MSANGI ANAWATAKIA KHERI YA MWAKA MPYA WA 2014 WANANCHI WOTE WAKAZI WA MKOA WA MBEYA.


Signed by:
[AHMED .Z. MSANGI - SACP]
KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA.