Translate

Friday, July 29, 2011

walimu Mbeya nusura wachapane makonde kwa kudai posho

Na Thompson Mpanji,Mbeya

OFISI ya Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya imewataka walimu kuilinda heshima ya taaluma yao pindi wanapokuwa katika makundi mbalimbali ya kijamii na mikutano sanjari na kujenga uaminifu katika vyombo vya fedha badala ya kugushi nyaraka za mishahara kwa lengo la kujikupatia mikopo kwa njia ya rahisi ya udanganyifu.

Ushauri huo umetolewa na mweka hazina wa Halmshauri ya Wilaya ya Mbeya,Bw.Chamba Bigambo kwa niaba ya Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo,Bibi.Juliana Malange wakati wa Mkutano Mkuu wa 13 wa Chama cha akiba na mikopo cha Mbeya Teacher,s Saccos uliofanyika jana jijini hapa.


Bw.Bigambo aliyasema hayo kufuatia vuta nikuvute na baadhi ya walimu ambao ni wanachama wa Saccos hiyo kudai posho ya kikao huku wakihoji uhalali wa wanachama wengine kulipwa na wengine kukosa.

Mvutano huo ulitokea mara baada ya kufunguliwa kwa mkutano ambapo baadhi ya kundi lililoonekana kuandaa ajenda hiyo ya siri kunyoosha mkono na kudai hawapo tayari kuendelea na mkutano hadi suala lao la kulipwa posho liwe limetatuliwa.


Mwenyekiti wa Mbeya Teachers Saccos,Bibi.Anna Mwakalukwa aliurejesha mkutano huo katika hali ya kawaida baada ya viongozi mbalimbali akiwemo Ofisa Ushirika kutoka Wizara ya kilimo,Chakula na Ushirika na Ofisa Ushirika wa Wilaya kuwasomea vifungu vya sheria,kanuni na taratibu ambapo yeye alitoa ufafanuzi kuwa katika mkutano mkuu wa 12 uliofanyika mwaka 2010 katika ajenda nambari 9 kuhusu hisa za mwanachama, walikubaliana kila mwanachama awe na hisa 10 ambapo hisa moja ni sh.10,000 na kwamba mwanachama asiyefikisha idadi hiyo ya hisa siyo mwanachama kamili .


Bibi.Mwakalukwa alisema kuwa kutokana na ajenda hiyo mkutano mkuu huo wa 12 ulipitisha azimio kuwa mwanachama ambaye hajafikia hisa 10 hatohusika na posho zitakazotolewa kuanzia katika mkutano mkuu wa 13 jambo ambalo limetekelewa na kwamba endapo kutakuwa na hoja ya kutenguliwa kwa azimio hilo basi lijadiliwe mwishoni.


Hata hivyo Mgeni rasmi huyo aliposimama alielezea masikitiko yake kuhusu mvutano huo ambao haukuwa na mantiki yeyote kutokana na walalamikaji kutofuata maandishi yaliyokuwemo katika muhtasari wa mkutano uliopita na kwamba endapo walikuwa na hoja za msingi basi ni vema wangetumia busara kuandika na kupitisha mbele kwa mwenyekiti kuliko kuanzisha malumbano yasiyo na msingi kwa wanataaluma hao ambao ni mfano wa kuigwa kwa jamii,.

Bw.Bigambo aliwafunda walimu hao kujiheshimu na kujenga nidhamu mbele ya mgeni rasmi katika mikusanyiko yeyote na mahali penginepo badala ya kuonesha utovu wa nidhamu jambo ambalo amedai halikumfurahisha hata kidogo.


Naye Meneja wa Benki ya CRDB tawi la Mbeya,Lucas Busigazi amewashauri walimu waache tabia ya kughushi hati za mishahara kama Bibi.Mwakalukwa alivyodai katika taarifa yake na kwamba ni vema walimu wakawa na nidhamu katika kukopa na kurejesha kwa wakati badala ya kutanguliza tama ambazo zinaweza kuja kuwagharimu katika vyombo vya sheria pindi wakibainika.


Mwisho.

Thursday, July 21, 2011

Na Thompson Mpanji,Mbeya

CHAMA cha akiba na mikopo cha walimu Mbeya Teacher’s Saccos,jijini

Mbeya kimefanikiwa kutoa mkopo wa zaidi ya Sh.Bil.1.1 kwa wanachama

wake zaidi ya 1,148 wakiwemo wanaume 539 na wanawake 609 hadi kufikia

Disemba,2010.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi,Ofisini kwake,Mwenyekiti wa Chama

hicho,Bibi,Anna Mwakalukwa alisema kuwa Chama hicho kilianzishwa mwaka

1995 na kusajiliwa mwaka 1997 kikiwa na wanachama 100 wakiwemo wanaume

54 na wanawake 46 wakiwa na akiba ya Sh.45,000 bila kuwa na hisa wala

amana.


Bibi.Mwakalukwa alisema kuwa kutokana na mwamko wa wanachama Mbeya

Teacher’s Saccos imefikia akiba ya Sh.Mil.408.8,hisa Sh.Mil.54.1 na

amana Sh.275,000 na amewataka wanachama kujenga utamaduni wa kujiwekea

amana badala ya kukimbilia mikopo.


Aidha Mwenyekiti huyo alisema takwimu za idadi ya wanachama

zinathibitisha ukweli usiopingika kuwa akina mama ni nguzo na mfano wa

kuigwa katika kutambua umuhimnu wa kujiwekea akiba ili kumtokomeza

adui umaskini.


Hata hivyo Mwenyekiti huyo amewataka wanachama wa Mbeya Teacher’s

Saccos kujitokeza kwa wingi katika mkutano mkuu wa 13 unaotarajiwa

kufanyika julai,22 mwaka huu katika ukumbi wa Nuru Park (Royal

Zambezi),uliopo Soweto,jijini Mbeya.



Mwisho.