Translate

Thursday, July 21, 2011

Na Thompson Mpanji,Mbeya

CHAMA cha akiba na mikopo cha walimu Mbeya Teacher’s Saccos,jijini

Mbeya kimefanikiwa kutoa mkopo wa zaidi ya Sh.Bil.1.1 kwa wanachama

wake zaidi ya 1,148 wakiwemo wanaume 539 na wanawake 609 hadi kufikia

Disemba,2010.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi,Ofisini kwake,Mwenyekiti wa Chama

hicho,Bibi,Anna Mwakalukwa alisema kuwa Chama hicho kilianzishwa mwaka

1995 na kusajiliwa mwaka 1997 kikiwa na wanachama 100 wakiwemo wanaume

54 na wanawake 46 wakiwa na akiba ya Sh.45,000 bila kuwa na hisa wala

amana.


Bibi.Mwakalukwa alisema kuwa kutokana na mwamko wa wanachama Mbeya

Teacher’s Saccos imefikia akiba ya Sh.Mil.408.8,hisa Sh.Mil.54.1 na

amana Sh.275,000 na amewataka wanachama kujenga utamaduni wa kujiwekea

amana badala ya kukimbilia mikopo.


Aidha Mwenyekiti huyo alisema takwimu za idadi ya wanachama

zinathibitisha ukweli usiopingika kuwa akina mama ni nguzo na mfano wa

kuigwa katika kutambua umuhimnu wa kujiwekea akiba ili kumtokomeza

adui umaskini.


Hata hivyo Mwenyekiti huyo amewataka wanachama wa Mbeya Teacher’s

Saccos kujitokeza kwa wingi katika mkutano mkuu wa 13 unaotarajiwa

kufanyika julai,22 mwaka huu katika ukumbi wa Nuru Park (Royal

Zambezi),uliopo Soweto,jijini Mbeya.



Mwisho.

No comments:

Post a Comment