Na Thompson Mpanji,Mbeya
CHAMA cha akiba na mikopo cha walimu Mbeya Teacher’s Saccos,jijini
Mbeya kimefanikiwa kutoa mkopo wa zaidi ya Sh.Bil.1.1 kwa wanachama
wake zaidi ya 1,148 wakiwemo wanaume 539 na wanawake 609 hadi kufikia
hicho,Bibi,Anna Mwakalukwa alisema kuwa Chama hicho kilianzishwa mwaka
1995 na kusajiliwa mwaka 1997 kikiwa na wanachama 100 wakiwemo wanaume
54 na wanawake 46 wakiwa na akiba ya Sh.45,000 bila kuwa na hisa wala
Bibi.Mwakalukwa alisema kuwa kutokana na mwamko wa wanachama Mbeya
Teacher’s Saccos imefikia akiba ya Sh.Mil.408.8,hisa Sh.Mil.54.1 na
amana Sh.275,000 na amewataka wanachama kujenga utamaduni wa kujiwekea
Aidha Mwenyekiti huyo alisema takwimu za idadi ya wanachama
zinathibitisha ukweli usiopingika kuwa akina mama ni nguzo na mfano wa
kuigwa katika kutambua umuhimnu wa kujiwekea akiba ili kumtokomeza
Hata hivyo Mwenyekiti huyo amewataka wanachama wa Mbeya Teacher’s
Saccos kujitokeza kwa wingi katika mkutano mkuu wa 13 unaotarajiwa
kufanyika julai,22 mwaka huu katika ukumbi wa Nuru Park (Royal
Zambezi),uliopo Soweto,jijini Mbeya.
Mwisho.
CHAMA cha akiba na mikopo cha walimu Mbeya Teacher’s Saccos,jijini
Mbeya kimefanikiwa kutoa mkopo wa zaidi ya Sh.Bil.1.1 kwa wanachama
wake zaidi ya 1,148 wakiwemo wanaume 539 na wanawake 609 hadi kufikia
Disemba,2010.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi,Ofisini kwake,Mwenyekiti wa Chama
hicho,Bibi,Anna Mwakalukwa alisema kuwa Chama hicho kilianzishwa mwaka
1995 na kusajiliwa mwaka 1997 kikiwa na wanachama 100 wakiwemo wanaume
54 na wanawake 46 wakiwa na akiba ya Sh.45,000 bila kuwa na hisa wala
amana.
Bibi.Mwakalukwa alisema kuwa kutokana na mwamko wa wanachama Mbeya
Teacher’s Saccos imefikia akiba ya Sh.Mil.408.8,hisa Sh.Mil.54.1 na
amana Sh.275,000 na amewataka wanachama kujenga utamaduni wa kujiwekea
amana badala ya kukimbilia mikopo.
Aidha Mwenyekiti huyo alisema takwimu za idadi ya wanachama
zinathibitisha ukweli usiopingika kuwa akina mama ni nguzo na mfano wa
kuigwa katika kutambua umuhimnu wa kujiwekea akiba ili kumtokomeza
adui umaskini.
Hata hivyo Mwenyekiti huyo amewataka wanachama wa Mbeya Teacher’s
Saccos kujitokeza kwa wingi katika mkutano mkuu wa 13 unaotarajiwa
kufanyika julai,22 mwaka huu katika ukumbi wa Nuru Park (Royal
Zambezi),uliopo Soweto,jijini Mbeya.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment