Translate

Monday, August 30, 2010

watu wanaoishi na maambukizi ya virusi vya ukimwi wamezishukia Asasi zinazowahudumia kwa kwa madai ya kutowapatia huduma stahili,wadai ARV's basi

Na Thompson Mpanji,Mbeya

WAGONJWA wanaoishi na maambukizi ya Virusi vya ukimwi wamezilalamikia Asasi zinazoshughulika na masuala ya ukimwi,watoto yatima na wanaoishi katika mazingira magumu jijini Mbeya kwa kutowapatia lishe na huduma nyingine muhimu kama wanavyopangiwa na madaktari.

Madai hayo yametolewa na wagonjwa kutoka katika Kata mbalimbali jijini hapa walipokuwa wakizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti kufuatia kuwepo kwa tetesi za kutelekezwa kwa wagonjwa hao.

Walisema kuwa wameshangazwa na ukimya uliopo katika asasi wanazohudumiwa tofauti na ilivyokuwa awali kwani walikuwa wakipatiwa huduma zote kufuatana na maelekezo ya madaktari wanaowahudumia na kwamba maisha yao yapo hatarini kutokana na madawa wanayoyatumia kwa ajili ya kurefusha maisha yanawamaliza nguvu kutokana na kuyanywa bila kupata lishe.

Walisema tangu walipopima afya zao na kugundulika kuwa wanaishi na maambukizi ya virusi vya ukimwi walikuwa wakiandikiwa na madaktari kupata lishe bora kama samaki,matunda,mayai na maziwa pamoja na fedha ya nauli lakini tangu mwezi januari,2010 hadi sasa hakuna huduma yeyote waliyoipata zaidi ya kupigwa kalenda na wahusika katika Asasi wanazohudumiwa.

“Wanasema hawana fedha sasa wanawezaje kuja majumbani tulipo na kutupatia elimu kila kata kama hawajaletewa fedha na wafadhili kama wanavyotuambia,ni uongo hawa wanakula fedha kupitia migongo yetu,ni bora hata madawa haya tusiyatumie kwa sababu yanahitaji kula,”alilalamika mmoja wa wagonjwa ambaye hakutaka jina lake kuandikwa gazetini.

Mmoja wa viongozi wa asasi ambayo hakupenda kutaja jina lake alisema tayari asasi zilishatiliana saini katika mkataba wa kukubaliana kuwapatia fedha lakini hadi sasa wamelipwa awamu moja ambayo ilitakiwa waipate tangu mwaka 2009 lakini katika hali isiyokuwa ya kawaida wamelipwa kuanzia mwenzi mei,juni, na agosti,2010.

“Afadhari tusingesaini mkataba na sheria inasema ukivunja mkataba utashtakiwa sasa leo tuwashtaki wamarekani kwa kukiuka mkataba?,mama mmoja alikuja juzi huku analia njaa hata nauli hakuwa nayo huku ameandikiwa na daktari apewe lishe na sisi hatuna yeye ni mgonjwa wa BMI lakini hata mfukoni hatuna cha kumpa,”alisema.

Alisema kuwa kutokanma na hali hiyo hali imekuwa ngumu na watu wenye maambukizi ya virusi vya ukimwi hawaamini kama tatizo siyo lako kutokana na ahadi walizowahi kuwapatia kuwa wafadhiri walikubali kuwatumia hatua iliyofikia hata wahudumu na wafanyakazi wa Asasi hiyo kufukuzwa na matusi juu wanapowatembelea wagonjwa majumbani.

Mwenyekiti wa mtandao wa Mbeya HIV aids Padre Johnathan Mwashilindi, akizungumza na mwandishi wa habari hizi amekiri kuwepo kwa tatizo hilo kwa mara ya kwanza tangu waanze kusaidiwa na serikali ya Marekani kupitia wasimamizi wao Water reed na hasa kwa upande wa wagonjwa wa huduma za majumbani katika asasi zote 22 zilizopo katika mtandao huo.
Amezitaja asasi ambazo zimekumbwa na adha hiyo na mahali zilipo katika mabano ni pamoja na Caritas Mbeya,Anglikan,Shidepha+,Ok Tree,Seta,IRTF,Kihumbe na TPDF Mbalizi (jijini Mbeya),Hospitali ya misheni ya Mbozi,ABC Tunduma na Shidepha+ Mbozi (Mbozi),Hosana (Ileje),CSDO na Fedea (Chunya),Shidepha+Mbarali,TAG na SKIMMVU (Mbarali),LCCB na Igogwe Hospitali (Rungwe) na Usaka,Mango Tree na John Hus (Kyela)

Padre Mwashilindi alisema kuwa walifikia hatua ya kulazimika kukopa fedha kwa ajili ya kuondoa aza waliyokuwa wanakabiliana nayo watoto ya kufukuzwa mashuleni kutokana na kukosa ada na kuwapatia vifaa muhimu vya shule ambapo fedha zilizotumwa hivi karibuni zinatumika kwa ajili kurejesha madeni waliyokopa.
Alisema asasi nyingi zimeshindwa kukopa kutokana na kushindwa kulipia riba kwa sababu mikopo mingi ina masharti ya kulipa riba na wao hawafanyi biashara bali wanatoa huduma

Hata hivyo Padre huyo alisema baada ya kuwasiliana na wasimamizi wa Mradi huo unaosimamiwa na Shirika la Water Reed kutoka nchini Marekani wamesema kuwa tatizo kubwa ni kuchelewa kupitishwa kwa bajeti ya Wizara ya afya nchini Marekani.

Mwisho.

Thompson Mpanji


thompson