Translate

Monday, December 24, 2012

watoto waandikishwa kwa malipo Mbeya

Na Thompson Mpanji,Mbeya
 
BAADHI ya wazazi jijini hapa wamelalamikia hatua ya serikali ya mtaa wa Ilomba,jijini Mbeya kuwatoza Sh.12,500 mchango wa kuandikisha jina  la kuingia darasa la kwanza mwaka 2013.
 
Hatua hiyo inadaiwa kwenda kinyume na maagizo ya Waziri wa nchi,Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI),Kassim majaliwa kuwa kuandikisha darasa la kwanza ni bure na hakuna michango yeyote iliyoruhusiwa kisheria.
 
Wakizungumza na gazeti hili baadhi ya wazazi (majina yamehifadhiwa)walisema kuwa wameshangazwa  viongozi wa serikali ya mtaa kuandikisha majina ya watoto kwa kutoza sh.12,500 na kwamba mzazi asiyekuwa na kiasi hicho mtoto wake hawezi kupokelewa.
 
Walisema wameambiwa kuwa mzazi ambaye hataweza kutoa fedha hiyo mtoto wake hawezi kusoma shuleni hapo na endapo atakubaliwa basi atatakiwa kukaa chini kwenye vumbi hatoruhusiwa kukalia dawati jambo ambalo wamedai ni unyanyasaji.
 
"Wametuambia eti kama hatutowi basi watoto wetu watakuwa wakisoma huku wakiwa wamekaa kwenye vumbi darasani na wenzao waliolipa watakaa katika madawati…ndiyo maana watoto wetu wanarudi wamechafuka ovyo kila siku kumbe ni sababu ya kuwanyanyapaa,"alisema.
 
Mmoja wa wajumbe wa serikali ya mtaa wa Ilomba,Mwl.Edwin Kamweli alisema hizo ni mbinu chafu za baadhi ya wanasiasa kutaka kuzorotesha maendeleo ya mtaa wa Ilomba kwani mkutano wa hadhara ulikaa na kukubaliana wanannchi wote kutoa mchango huo kwa ajili ya kuboresha mazingira ya shule.
 
"Huu mfumo wa vyama vingi utaturudisha nyuma tukiendekeza maneno bila vitendo…kuna watu wavivu wanatumia fursa ya demokrasia kuturudisha nyuma na sisi tunasema hatuwezi kukubali na haiwasaiidii tunasonga mbele…vikao na mikutano ikiitishwa wanasema wapo bize tuikipitisha maazimio wanasema tunawaonea,"alisema.
 
Mwl.Kamwela alisema kiasi hicho cha sh.12,500 kilipitishwa na wananchi waliohudhuria mkutano mmoja wa hadhara ikiwa na lengo la kuboresha mazingira ya shule na wanafunzi ili waweze kusoma bila kubanana.
 
Alisema mgawanyo wa fedha hiyo ni Sh.10,000 kwa ajili ya dawati litakalochangiwa na wanafunzi watatu watakaolitumia ambapo kila mmoja atachangia kiasi hicho na kukamilisha gharama ya ununuzi wa dawati moja kwa Sh.30,000.
 
Mwalimu huyo mstaafu aliendelea kufafanua kuwa katika shule hizo mbili za Kagera na Ruanda Nzwovwe kuna mlinzi anayelipwa na hivyo kila mzazi wamekubaliana achangie Sh.1,500 ambapo mchango wa maji ni Sh.1,000.
 
Ofisa Mtendaji wa Kata ya Ilomba,Erasto Mwakapoma alifafanua kuwa uandikishwaji ni bure lakini michango hiyo ilitokana na wananchi wenyewe baada ya kukaa katika mkutano wa hadhara wa mtaa wa Ilomba Novemba,30,2012 ambapo yeye alikaribishwa na kwamba wanaochangia ni wananchi wote na siyo wazazi wanaowaandikisha watoto shule pekee.
 
Mwakapoma alisema shule ya smingi Kagera na Ruanda Nzovwe zinatarajia kuandikisha watoto zaidi ya 200 ingawa lengo lilikuwa watoto 130,lakini hawatoweza kukataa kuwaaandiskisha watoto waliofikia umri wa kwenda shule hivyo kunahitajika madawati ya ziada.
 
Mwisho.

Kilio cha cha Askofu Chengula kwa serikali chajibiwa,asema hana neno sasa

Na Thompson Mpanji,Rungwe

KAMA wasemavyo wahenga kuwa machozi ya mtu mzima hayaendi bure ndivyo ilivyotokea kwa Askofu wa kanisa katoliki jimbo la Mbeya,Evaristo Chengula kwa serikali ya Mkoa wa Mbeya kuhusu ardhi ya Kijiji cha Lupata aliyoanza kuililia tangu mwaka 1992 kwa ajili ya kuwasaidia watanzania kwa kujenga chuo cha uuguzi na uganga bila mafanikio hatimaye kimesikika baada ya kukabidhiwa rasmi ardhi hiyo na Mkuu wa Wilaya ya Rungwe.

Askofu  ametoa  kilio chake kwa serikali na kuhoji sababu ya kukwama kwa mchakato huo hata alidiri kusema endapo ardhi hiyo ya mungu imekuwa na mlolongo mkubwa kwa maneno yaliyozoeleka serikali kuwa ' mchakato' unaendelea basi itafika wakati kanisa litahamishia ujenzi wa chuo hicho cha uuguzi katika maeneo mengine.

Askofu Chengula ametoa kilio chake katika jubilei ya fedha ya miaka 50 tangu kufunguliwa kwa Hospitali ya teule ya Wilaya ya Igogwe inayomilikiwa na kanisa katoliki Jimbo la Mbeya mwaka 1962 ambapo mgeni rasmi katika maadhimisho hayo Mkuu wa wilaya ya Rungwe Chrispin Meela alisema wanaozuia mchakato huo kukamilika washindwe na walegee na ardhi itatolewa baada ya wiki moja na alimsihi Askofu Chengula atulie na alale usingizi akiwa na uhakika wa kupata eneo hilo.

Akizungumza katika mkutano wa hadhara wa makabidhiano ya eneo hilo,Meela amesema baada ya kusikia mahubiri ya Askofu kutoa kilio chake kwa uchungu aliona ipo sababu ya kufanya haraka kufuatilia suala hilo na kulikamilisha na hivyo baada ya kupitia nyaraka za awali na kupata matokeo ya tume ya uchunguzi iliyoundwa na Katibu tawala wa Wilaya ya Rungwe aliamua kutoa ardhi kwa niaba ya Rais Jakaya Mrisho Kikwete ambaye ndiye mwenye ardhi kikatiba.

Amesema kazi yake kubwa kama Mkuu wa Wilaya ni kusimamia haki na sheria na kwamba katika suala la ardhi hiyo aliangalia taratibu zinasemaje na baadaye alichukuwa maamuzi baada ya kupima manufaa ya suala lenyewe kwa umma anayoiongoza.

"Nyaraka zilionesha kuna ubabaishaji mwingi kwa sababu taratibu zote za kutuma maombi zilifuatwa kuanzia ngazi ya Kijiji,nikaona Rungwe tuna upungufu wa wauguzi 128,nikaona chuo kitakuwa mkombozi katika zahanati na vituo vya afya ambavyo vina upungufu mkubwa wa wataalamu kwa hiyo ninakukabidhi ramani hii Baba Askofu anzeni mara moja kujenga baada ya Desemba 22 watakapokuja watu wa upimaji na ahadi ya watoto wa kijiji hiki na Rungwe kwa ujumla kupewa kipaumbele usisahau,"amesema Mkuu wa Wilaya.

Hata hivyo Mkuu huyo wa Wilaya amesema kuwa anao mzigo mkubwa wa wanafunzi zaidi ya 4,000 kati ya 5,000 waliomaliza kidato cha nne mwaka jana ambao wapo wanazurula mitaani baada ya kuchaguliwa wanafunzi 800 kati yao kuendelea na kidato cha tano.
 
Askofu Chengula ameishukuru serikali na kumtaka Mkuu wa wilaya kufikisha salam zake kwa serikali yote ya Wilaya,kwa Mkuu wa Mkoa na Rais Kikwete kwa kumkabidhi ardhi hiyo kwa ajili ya manufaa ya watanzania kwani wataalamu watakaosoma hapo watakuwa ni watoto wa watanzania.
 
"Watoto watakaosoma hapa ni wa kwetu na chuo kitakuwa hakifungamani na imani za kidini,itikadi za kisiasa,kabila wa rangi, na watakaokwenda kuwahudumia ni watu wa imani mbalimbali,itikadi za kisiasa tofauti na hata wale waliokuwa wakipinga kanisa kupewa ardhi watahudumiwa bila ubaguzi,watoto watapata ajira,wakazi wa hapa wataongeza vipato kwa ajili ya nyumba,biashara,usafiri na mengine mengi,na tatizo la upungufu wa wauguzi na waganga litapungua,"amesema Askofu.
 
Aliongeza,:Leo sina la kusema mtoto tumempata tumlee wote...kilio changu kilikuwa kumpata mtoto huyu...ninawaombea hata wale waliokuwa wanakataa kutoa ardhi wakiuguwa watibiwe...ningetoa mkono wa shukurani kwenu nyote lakini natoa baraka kwenu nyote,watakaofanyakazi,watakaofika kusoma."
 
Akisoma risala mbele ya mkuu wa wilaya Mganga Mkuu wa Hospitali ya Igogwe,Dkt.Oyeti Mwakosya chuo kinatarajia kuanza na wanafunzi 90 wa ngazi ya cheti kutokana na mipango ya serikali na wanatarajia kuendelea kutoa kozi za ngazi ya stashahada na shahada kwa wauguzi na kwamba ujenzi wa chuo ni faraja kwa Wilaya na Jimbo Katoliki la Mbeya.
 
Chifu wa Kijiji cha Lukata alimshukuyru Askofu Chengula na Mkuu wa wilaya kwa kushirikina nao hadi kuha,kikisha ardhi hiyo inapatikana kwani uwepo wa chuo hicho ni bahati kubwa kwao na kwamba watu wake wote wamepokea tukio hilo la kihistoria kwa furaha zote na ndiyo maana wamejitokeza kwa wingi kushuhudia tukio hilo la Askofu kukabidhiwa rasmi ardhi ambapo zaidi ya machifu 12 walishiriki.
 
Mwisho.

Kanisa katoliki laishangaa Tanesco Mbeya kuwabambikia deni la zaidi ya Sh.Mil.20,

Na Thompson Mpanji,Mbeya
 
KANISA Katoliki Jimbo la Mbeya  limelishangaa Shirika la Umeme la Taifa (TANESCO)Mbeya kwa kuliamisha deni la umeme lenye thamani ya zaidi ya Sh.Mil.20 na kulibambikia kanisa,kukataa umeme kwa takribani mwezi mmoja sasa sanjari na kung’oa waya wa ‘service line’ na kusababisha ukosefu wa umeme kwa takribani mwezi mmoja tangu mwezi Novemba,2012.
 
Aidha kanisa hilo limesema limeshindwa kuelewa nia ya uongozi wa tanesco Mbeya kutokana na deni hilo huku wakiwa na majibu ya dharau, limemuomba Waziri wa Nishati na Madini Prof.Sospeter Muhungo kuingilia kati suala hilo na kulimaliza.
 
"Hatutaki kuingia zaidi kuhusina na suala hili…tunamsihi Waziri Muhongo aingilie kati suala hili hatupendi kufika mbali …afuatilie ataona mauza uza wanayoyafanya watumishi wake wa Tanesco ambao wanaona kama shirika ni mali yao na kumpatia mtu deni mtu ambalo siyo haki yake ni rahisi ,"alisema Mwenyekiti wa Halmashauri ya walei jimbo la Mbeya,Magoma.
 
Mwenyekiti huyo alisema alipokea malalamiko kutoka kwa wapangaji wa nyumba ambazo zinamilikiwa na kanisa Katoliki jimbo la Mbeya kuwa wamekatiwa umeme kwa kudaiwa deni la Sh.Mil.4 na baada ya kufuatilia walibadilishiwa na kuambiwa wanadaiwa Sh.Mil.16 na kwamba wamehamishiwa deni hilo katika mita yao ili watoe msukumo kwa kanisa kulilipa deni ambalo wamekuwa wakipiga chenga kulilipa.
 
Magoma alisema mazingira ya majibu hayo yanaonesha dhahiri kuwa baadhi ya watumishi wa Tanesco hawajatenda haki kwa kuhamishia deni katika akaunti ambayo haidaiwi,lakini bado amekuwa akijiuliza kama kanisa linadaiwa Tanesco Mbeya imeshindwa nini kufuatilia badala ya kwenda kuwabambikia deni la mamilioni watu ambao hawana uwezo wa kulilipa deni hilo hata baada ya miaka 100 kama siyo kuwadhulumu haki ya kupata umeme.
 
 
Bibi.Veronika Mwazembe Mkazi wa nyumba hizo kwa sasa Mtakatifu mathias Mulumba alisema wanao ushahidi wa kulipa deni la mita lililoachwa na watumiaji wengine iliyokuwa ikidaiwa tangu mwaka 2010 na kuthibitishwa na ofisa wa Tanesco Mbeya aliyesaini ambapo wamelilipa taratibu hadi kulimaliza.
 
Bibi.Mwazembe alisema baada ya kumaliza deni hilo mwaka 2011 walibadilishiwa mita ya luku na kuendelea kuitumia lakini katika hatua ya kushangaza oktoba,2012 wamezuiwa kutumia huduma hiyo kwa madai ya kudaiwa zaidi ya Sh.mil.16 jambo ambalo limewakatisha tamaa ya kuendelea kunufaika na umeme wa shirika la Tanesco kwa madai hata kama lingekuwa ni deni halali hawana uwezo wa kulilipa hata kwa miaka 100 ijayo.
 
Mkazi mwingine ambaye aliomba jina lake kuhifadhiwa kwa sababu maalum alisema wateja wa Tanesco wanaokutwa wameiba umeme kwa kujiunganishia isivyo halali wanachukuliwa hatua kali za kisheria hivyo kwanini shirika hilo nalo lisifikishwe mahakamani kwa kuwalimbikizia deni watu wasiohusika huku wakijuwa ni uonevu,unyanyasaji, kinyume na haki za binadamu sanjari na makosa kisheria.
 
Alisema baada ya kufungiwa kutumia umeme walifika kutoa malalamiko yao kwa Mhasibu wa Tanesco Mkoa aliyemtaja kwa jina moja la Mkotwe ambaye alidai ofisa aliyekuwa akishughulikia suala hilo yupo Dar es salaam kikazi kwa hiyo anawafungulia kwa muda kutumia umeme wakati wakiendelea kumsubiri mhusika kuja kutatua madai hayo ya deni la Sh.mil.4.
 
Alifafanua kuwa mwezi Novemba,2012 walipoenda kununua umeme wa Luku waliambiwa wamefungiwa na baada ya kuwasiliana na wahusika wa huduma kwa wateja wa Luku makao makuu Dar es salaama waliwaambia kuwa wanadaiwa Sh.mil.10 katika mita moja na Sh.mil.6 katika mita nyingine jambo ambalo liliwashtusha.
 
Mteja huyo alisema walishangazwa na taarifa hiyo ambayo awali mwezi oktoba ilionekana wanadaiwa Sh.Mil.4 ambazo ziliingizwa kimakosa na kwamba katika hatua ya kushangaza inaonesha dhahiri kuwa Mhasibu wa Tanesco mkoa alionesha deni la awali wateja wamelikubali na hivyo kukatwa asilimia 100 yaani asilimia 50 kwa mita moja na asilimia 50 kwa mita nyingine jambo lililowatia mashaka kuwa Mhasibu huyo anahusika na kuwahujumu.
 
Aidha alisema baada ya kuwasiliana na Mhasibu huyo aliwaambia baada ya kufungua katika mfumo wa awali na kubadilisha masharti, wateja hao wanatakiwa kulipia kiasi cha Sh.100,000 ama 500,000 kupunguza deni ili wafunguliwe umeme na kuendelea kuutumia.
 
Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili umebaini kuwa kuna mchezo mchafu unaochezwa na baadhi ya maofisa wa Tanesco kubambika madeni watu wasiohusika ikiwa ni njia mojawapo ya kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu huku wakiwaacha walalahoi wakikosa matumaini na imani na shirika lao la kitanzania.
 
Gazeti hili liliwasiliana na Ofisa anayehusika na udhibiti wa madeni aliyejitambulisha kwa jina la Rehema ambaye alikiri kuwa deni hilo siyo la wahusika wanaotumia luku lakini kutokana na kanisa katoliki jimbo la Mbeya ambao wamenunua nyumba hizo kutoka kampuni ya Mbeya Retco kupuuzia kulilipa deni hilo wamefikia uamuzi wa kulihamishia katika mita ya luku inayotumiwa na wapangaji ambayo haikuwa na deni.
 
Ofisa huyo alisema wateja hao wanaolalamika wanapaswa kulishinikiza kanisa kulilipia deni hilo ili nao waendelee kupata huduma hiyo vinginevyo wataendelea kukosa huduma hiyo na kwamba hata kanisa likibomoa nyumba hizo na kujenga nyumba nyingine deni hilo litaendelea kuongezeka na watapaswa walilipe hata baada ya miaka 100.
 
Mmoja wa wafanyakazi wa Tanesco ambaye hakupenda kutajwa jina lake kwa madai yeye siyo msemaji alisema wateja hao hawakutendewa haki kwa sababu mmiliki wa deni hilo anafahamika ambaye ni Mbeya retco aliyemuuzia kanisa katoliki hivyo ilikuwa ni jukumu la kuwatafuta na kuwabana wahusika hao badala ya kuwaonea walala hoi hao.
 
Mfanyakazi mwingine alitoa ushauri kuwa wateja hao waonanne na uongozi wa kanisa ambao walinunua majengo hayo na kuwaomba waende katika shirika la Tanesco kwa kuandika barua kuwa hawakununua nyumba na madeni hili deni hilo liingie katika akaunti ya Mbeya Retco badala ya wapangaji hao.
 
Gazeti hili limepata nakala ya Ankara ya umeme iliyoandikwa" LUKU Sms operator fungua luku meter no.01319959639 ameshalipa deni lote bado kufuta riba chini kukiwa na sahihi yake julai,18,2011, na chini yake kukiandikwa ujumbe mwingine uliosainiwa na ofisa mwingine ukisema ," SRA mteja hana deni kiasi kilichobaki ni interest imeshaandikiwa bado kufutwa."
 
Hata hivyo gazeti hili lilikwenda kwa undani zaidi kuangalia jina la akaunti hiyo ambayo inatumika na wateja hao wanaodaiwa kubambikiwa ni Mr.Prince M John P.O.BOX 109,Mbeya ambayo ilonesha kuwa na deni la Sh.200,000 iliyopokelewa na kubakia Sh.1,566.05 katika nambari ya hesabu Prop Ref:T87.09.09203,cust Ref:85006773.
 
Wananchi hao walisema kuwa matumaini ya kuendelea kupata huduma ya umeme wa Tanesco yametoweka kabisa na kwamba wapo walala hoi kama wao waliobambikiwa madeni kama hayo na kwamba endapo Waziri wa nishati na madini atalivalia njuga suala hili kwa shirika la tanesco Mbeya na kwingineko watanzania watarudi katika dhama za mkolono kutumia vijinga vya moto na koroboi.
 
Meneja wa Shirika la Tanesco Mbeya,John Bandiye akizungumza na mwandishi wa habari hizi kwa njia ya simu aliulizia nambari ya akaunti ya mita na baada ya kupewa aliwaomba walalamikaji kufika ofisi ya Tanesco ke kwa ajili ya kueleweshwa kuhusiana na tatizo hilo ambapo baada ya kumjibu kuwa walishapewa kutoka kwa ofisa aliyekuwa akilishughulikia suala hilo hakuweza kujibu tena hadi tunakwenda mtamboni.
 
Mwisho.

Baada ya ARVs sasa tiba asili yachakachuliwa

Na Thompson Mpanji,Mbeya
 
WAKATI Serikali na baadhi ya mashirilka na watu mbalimbali wakikesha na kukuna vichwa wakitafuta tiba ya maambukizi ya virusi vya ukimwi,hali imekuwa tofauti kwa baadhi ya watanzania wasio na mapenzi mema kwa watu wanaopata maradhi hayo baada ya kuanza kuchakachua dawa na vyakula vya asili zinazodaiwa kuwasadia kwa asilimia kubwa kuwapatia nafuu wagonjwa wenye maambukizi.
 
Itakumbukwa kuwa hivi karibuni serikali kupitia mamlaka husika iliingia mzozo na hata kufikia kuzuia baadhi ya dawa zinazotolewa na shirika moja nchini kutokana na madai ya kutengeneza dawa feki za ARVs jambo ambalo lilileta sintofahamu na hata wahusika kuamua kutolea ufafanuzi wa sakata hilo ambalo lilidaiwa kuingiliana na masuala ya kisiasa na maslahi binafasi ya watu.
 
Wataalamu wa tiba asili nao wameanza kupaza sauti zao kupitia vyombo vya habari kuiomba serikali na mamlaka husika kuingilia kati na kuwadhibiti maharamia hao wa tiba na vyakula asili ambazo zimekuwa zikiwasaidia watanzania walio wengi wenye maradhi sugu na maambukizi ya virusi vya ukimwi kwa gharama nafuu na hatimaye kurudisha matumiani ya kuendelea kuishi na familia zao, sanjari na kufanyakazi.
 
Akizungumza na gazeti hili mmoja wa wajasiliamali wanaotengeneza `vyakula na tiba za asili kupitia matunda ya Ubuyu na Mlonge, Racher Alfan Mwasajone almaarufu Mama Peter,Mkazi wa Dodoma mtaa wa Makulu ya Njedengwa alisema wameingiliwa na maharamia wa madawa na kuanza kutengeneza bidhaa feki ambazo zimeanza kuonekana kutowasaidia tena na kuondoa matumaini kwa watu waliokumbwa na maradhi sugu ikiwemo Ukimwi.
 
Mjasiliamali huyo ambaye alihudhuria maonyesho ya wajasiliamali jijini Mbeya hivi karibuni alisema uchakachuaji huo unafanyika hasa katika mafuta ya ubuyu na mlonge na sasa wameingia katika unga wa ubuyu na mlonge kwa kuchanganya na unga mwingi wa mahindi ama muhogo ambapo kwa upande wa mlonge wanachanganya na majani ambayo hayaeleweki jambo ambalo linapunguza nguvu ya viini lishe vinavyokwenda kusaidia kinga ya mwili na kutibu maradhi mengine zaidi ya 40.
 
Racher alisema watu hao wasio na chembe ya huruma wamekuwa wakichanganya mafuta ya alizeti ama mafuta ya karanga katika mafuta ya mlonge na ubuyu na kuuza kwa bei ya chini huku wahitaji wakiyanunua kutokana na unafuu wa bei baada ya kupata ushuhuda ama historia ya kazi yake lakini matokeo yake hawapati aueni aidha kutokana na kutokana na ukosefu wa viini lishe katika bidhaa hizo feki ama vitu vinavyochanganywa kuwa sumu na kuuwa viini lishe.
 
Amefafanua kuwa ili kubaini mafuta ya ubuyu ama mlonge yaliyo safi ni vema kuangalia wepesi wa mafuta wakati wa kuinamisha chupa iliyokuwa na mafuta chini juu ambapo kwa unga wa ubuyu utajulikana kuwa ni halisi kwa kupata radha halisia ya ubuyu ambapo kwa majani ya mlonge hayana ukali na unga wake unanukia harufu nzuri ya kipekee inayomshawishi mtumiaji kunywa ama kulamba.
 
Hata hivyo Racher ametoa wito kwa serikali kupitia mamlaka husika kufuatilia kwa kina uhalifu huo na kuudhibiti kwani unaweza kuleta madhara makubwa kwa watumiaji wanaohitaji kupata tiba na hatimaye kuendelea kupoteza nguvukazi ya taifa kwa uzembe,makosa na tamaa ya watu wachache wasio na mapenzi mema na watanzania wenzao.
 
Mwisho.

Tuesday, December 11, 2012

Tanzania ikiwa imebakisha miaka 3 ya utekelezaji wamipango nane ya milenia

Na Thompson Mpanji,Mbeya
 
TANZANIA ipo katika utekelezaji wa millennia ambayo ni matokeo ya mkutano wa kilele wa millennia wa umoja wa mataifa uliofanyika mwezi septemba mwaka 2000 na kutokana na hali hiyo sitegemei kuwa kuna mtanzania asiyejuwa malengo hayo nane.
 
Lakini kwa kukumbushana ningependa kuyarejea tena maleongo hayo yaliyopangwa kutekelezwa katika mataifa 189 ambayo yalikuwa ni makubaliano yanayozitaka nchi zote zilizoendelea na zinazoendelea kufanyakazi kwa pamoja na kuhakikisha umaskini na njaa duniani vinatokomezwa,kuhakikisha elimu sawa kwa watoto wote,usawa wa jinsia na uwezeshwaji kwa wanawake.
 
Malengo mengine ni kupunguza vifo vya watoto wachanga,kuokoa maisha ya akina mama wazazi,kupunguza na kutokomeza ugonjwa wa ukimwi,marali na magonjwa mengine maambukizi,kudumisha usafi na ubora wa mazingira pamoja na kudumisha ushirikiano wa kimataifa kwa maendeleo kwa ujumla malengo ya millennia yanasisitiza zaidi maeneo ya afya,elimu,mazingira na ustawi wa jamii kwa ujumla.
 
Disemba,4,2012 kumefanyika tukio muhimu na la kihistoria kwa taifa la Tanzania kutokana na kuwa miongoni mwa nchi 50 kati ya 189 zilizochaguliwa kujadili,malengo hayo nane ya millennia katika kanda saba ambazo mahali yalipofanyika katikamabano ni kanda ya Ziwa (Mwanza),kanda ya kaskazini (Arusha),Kanda ya kati(Dodoma),kanda ya nyanda za juu (Mbeya),kanda ya kusini(Mtwara),kanda ya magharibi (Shinyanga) na kanda ya mashariki (Morogoro).
 
Katika kutekeleza hili,John kajiba mtafiti kutoka taasisi ya utafiti wa mambo ya uchumi na jamii (ESRF-Economic and Social Research Foundation) anasema taasisi hiyo imeombwa kusimamia majadiliano hayo kwa kushirikiana na Ofisi ya rais tume ya mipango katika kanda hizo saba na hasa katika maeneo ya Serikali za mitaa,Asasi za kiraia,watoto,wazee na wanawake wadogo ambapo kwa kanda ya Mbeya yamefanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Paradise,Soweto,jijini Mbeya.
 
Kajiba anasema kwa kuwa imebakia miaka mitatu ili kukamilisha miaka 15 iliyopangwa kufikia malengo ya millennia 2015 hivyo watu na taasisi mbalimbali zimeona ni bora kuanza kujadili na kujiuliza kitatokea nini na nini kifanyike baada ya mwaka 2015 ili kuongeza kasi na kutoa msukumo wa maendeleo duniani.
 
Kwa mujibu wa taarifa ya ESRF kuna mafanikio na changamoto ambazo zimejitokeza katika utekelezaji wa malebngo ya millennia ambapo kwa upande wa Tanzania imefanya vizuri katika maeneo mengi,licha ya baadhi ya maeneo kuwa na matokeo ambayo hayakuridhisha.
 
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya,Abbas kandoro ambaye alikuwa mgeni rasmi aliyefungua mkutano huo wa mashauriano katika hotuba yake amesema utekelezaji wa Tanzania unategemea utekelezaji wa kila Mkoa na Wilaya na hivyo ni dhahiri utatofautiana.
 
Ametolea mfano kwenye eneo la Ukimwi,Mkoa wa Mbeya una asilimia 9.2 kwa takwimu za mwaka 2008 wakati kitaifa ni asilimia 5.7,kupunguza umaskini kitaifa imetokea asilimia 39 kwa mujibu wa takwimu za mwaka 1990 hadi asilimia 33.6 kwa takwimu za mwaka 2007.
 
Kandoro anasema pato la mkazi wa Mbeya ni juu ya dola 1 hadi 1.5 kwa mujibu wa takwimu za mwaka 2010 ambapo katika elimu ya msingi na Sekondari ukiangalia katika uwiano wa Ke na Me wamevuka lengo kama nchi kwa asilimia 101 na 205 na kwa Mkoa wa Mbeya ni asilimia 102 na 88 ambayo kwa ujumla haijavuka lengo.
 
Anasema lazima kukiri kuwa bado kuna changamoto katika kutokomeza umaskini wa kipato,njaa,kuboresha afya ya uzazi na huduma za maji salama pamoja na elimu.
 
Kandoro ametoa maoni kuwa endapo kila mtanzania atajituma katika kutafuta maisha na kuzitumia fursa zinazomzunguka,akaacha kuwa mnung’unikaji wa hali ngumu ya maisha huku amekaa kijiweni,akaacha kumtafuta mchawi kwa kila linalomsibu,akawa mchangiaji katika kuhakikisha hali ya utulivu na amani inadumishwa kwa kuheshimu misingi ya utawala bora,kasi ya kuliendeleza taifa itakuwa kubwa.
 
"Kwa sasa bado tunaongea sana, ‘we are talking a lot,’ninaamini mkusanyiko huu utasaidia sana kufanya tathmini ya pamoja kujuwa tulikotoka,tulipo na tunakokwenda,ninaipongeza serikali kuteuwa Taasisi ya utafiti katika Nyanja za uchumi na jamii (ESRF) ifanye kazi ya kukusanya maoni ya wadau mbalimbali,"anasema.
 
Mkuu wa Mkoa huyo amesema kupitia warsha kutoka katika mikoa yote Tanzania, anao uhakika,ushauri na mapendekeo ya washiriki kuhusu kuamua nini kifanyike kwa siku zijazo baada ya 2015 ni muhimu sana.
 
Kutokana na mpango wa millennia mataifa makubwa yaliyoendelea yalipangiwa kutoa asilimia 7 ya pato lao la ndani kuchangia nchi zinazoendelea ambapo ni asilimia 4 ya nchi za Scandinavia zimeonekana kuongoza katika kuchangia ingawa siyo kwa asilimia zote na hiyo ni mojawapo ya changamoto kubwa iliyozikumba nchi nyingi tegemezi kukwama katika mipango na miradi yao ya maendeleo baada ya kukwama kwa misaada.
 
Dkt.John Mduma mwezeshaji ambaye ni Mhadhiri kutoka chuo kikuu cha Dar es salaam anasema lengo la mashauriano hayo ni kutoa kichocheo cha mjadala wa wadau mbalimbali,kujenga taswira ya kimataifa ya hali ya baadaye kwa mapendekezo madhubuti,kuhakikisha na kusikika sauti za maskini na wasio sikika,kutambua na kuchambua masuala yatakayoathiri maendeleo,kushawishi mchakato ndani ya serikali kuu ioane na taasisi na matokeo yanayotarajiwa.
 
Mwisho.

Mbunge wa Jimbo la Songwe akanusha kutoa mamilioni CCM ishinde

Na Thompson Mpanji,Chunya
 
MBUNGE wa Jimbo la Songwe(NEC),Mh.Philipo Mulugo amekanusha madai ya Chama cha Demokrasia na maendeleo(CHADEMA) Mbeya amemwaga mamilioni ya fedha kuhakikisha Chama Cha Mapinduzi (CCM) kinashinda katika uchaguzi mdogo wa Kijiji cha Saza na vitongoji vyake,wilayani Chunya sanjari na kuhakikisha Jeshi la polisi limewatia mbaroni viongozi wake wakiwemo na wagombea.
 
Baadhi ya wanachama na viongozi wa vyama vya upinzani wamemtuhumu Mh.Mulugo kuhusika na maagizo ya kukamatwa kwa viongozi hao kuwaita maofisa usalama wa taifa waliomwagwa katika kampeni za uchaguzi huo kuanzia Desemba,3,2012 siku ya uzinduzi sanjari na nguvu kubwa iliyotumika ya magari zaidi ya matano ya polisi aina ya 110 defender na askari Polisi wa kikosi cha kutuliza ghasia (FFU) yaani fanya fujo uone wakivalia 'magwanda' ya kutisha na kofia ngumu (element),ngao,mabomu,silaha za moto na virungu, ambapo walifika ameneo hayo Desemba,8 majira ya saa 10 jioni.
 
Kufuatia madai hayo Mbunge Mulugo ambaye ni Naibu waziri wa Elimu na mafunzo ya ufundi amekanusha vikali na kuhoji "nani anayelalamika?,huku akijigamba kuwa yeye kama Mbunge wa eneo husika ni lazima ahakikishe chama chake CCM kinapata ushindi mnono kwa kufanya kampeni zinazofuata taratibu za uchaguzi, na kuendelea kuhoji kuwa wanosema amemwaga mamilioni wameyaona wapi?."
 
Katibu mwenezi wa Chadema Wilaya ya Mbeya,Mh.Lucas Mwampiki ambaye pia na Diwani wa kata ya Mwakibete jijini Mbeya amedai askari hao walimwagwa kutokana na shinikizo la Mbunge kuhakikisha CCM inashinda na kuhakikisha baadhi ya Viongozi na wanachama wanakamatwa ili kupunguza kasi ya wapinzani na waogope kwenda katika mikutano ya kampeni.
 
Amewataja Viongozi waliokamatwa na Jeshi la Polisi wilayani Chunya ni pamoja na Diwani viti maalum Kata ya Kanga,Katibu wa Chadema wilaya ya Chunya Bryson Mwansimba,wagombea wawili wa kitongoji cha saza kati ambaye ni Mwenyekiti wa Chadema Kata ya kanga John Mponzayo,Katibu mwenezi wa Chadema Kata ya Kanga Suleimani Tanganyika,Katibu Mwenezi Kata,Amosi Tanganyika aliyekuwa anagombea Mwenyekiti wa kitongoji cha Saza kibaoni, wasanii waliofika na gari la matangazo na mpiga picha aliyefahamika kwa jina moja la Chris.
 
Mwampiki alisema walishamwandikia barua msimamizi wa uchaguzi mdogo wa Kata ya saza,Maurice Sapanjo ambaye ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya kutokubaliana kufanyika uchaguzi huo kutokana na madai matano ya ukiukwaji wa sheria za uchaguzi lakini amepuuza na uchaguzi unafanyika leo.
 
Ametaja baadhi ya mambo yaliyokiukwa ni pamoja na 1.kuandikisha watu wanaojuwa kusoma na kuandika 100 huku wote wanajuwa kusoma na kuandika,kutowahusisha viongozi au vyama kujuwa na kukagua vituo vya kupigia kura,3.kutowatambulisha wasimamizi wa vituo kwa wagombea au vyama vyao, kutopokea,kuwapa voapo wala kupokea orodha ya mawakala wa vyama pinzani,5.kutokujibu barua za malalamiko za wagombea au vyama kwa wakati.
 
Katibu huyo ametaja rafu iliyochezwa na CCM katika vituo vya kupigia kura ni kuongeza majina bandia ya wapiga kura ambapo katika kituo cha Saza kati wapiga kura waliojiandikisha walikuwa 96 waliongeza majina bandia 32 na kufanya idadi kufikia 128,kituo cha Bwana mzungu walioandikisha kihalali walikuwa 86,majina bandia 38 na kufanya idadi kuwa wapiga kura 124,kituo cha kibao 99 majina yaliyoongezwa 27 na kuwa jumla ya watu 126,kituo cha bwawani 98 waliongeza majina bandia 47 kwa hiyo watu waliowaongeza ni 144 ambapo ni vituo viwili vya Mwembeni na makambini hawakupata idadi.
 
Amesema CCM imeandaa matokeo na kufanya idadi ya watu walioandikishwa kihalali kufikia 844 badala ya 744 na matokeo wameyapanga kuwa CCM itaibuka kidedea kwa kupata kura za kishindo 744 dhidi ya Chadema watakaoanguka vibaya kwa kupata kura 100 na kwamba kijiji cha saza kina malalamiko ya uuzwaji wa kifusi cha mchanga wa dhahabu kwa zaidi ya Sh.Mil.392 walizonufaika viongozi wachache kwa hiyo ili kuepuka kashfa hiyo wameona njia pekee ni kucheza rafu.
 
.Hata hivyo Katibu huyo ameionya CCM kuwa Chadema haitarudi nyuma kudai haki za wanyonge,haitarudi nyuma kupigania haki za watanzania na matokeo yake wanawachochea zaidi kuelekeza nguvu zao Jimbo la Songwe,waache kutumia vyombo vya dola sanjari na kuvishauri vyombo vya dola kuacha kufanyakazi ya CCM waache mazoea,wasiwe chanzo cha kuvuruga amani.
 
Wakati huo huo,kumekuwepo na hofu ya uvunjifu wa amani na utulivu katika Kijiji ch Saza,Kata ya Saza,wilayani Chunya kutokana na madai ya Chama cha demokrasia na maendeleo( CHADEMA)kudaiwa kukodi makundi ya vijana,wanachama na wanaharakati kutoka mpakani mwa Zambaia na Tanzania Tunduma na Mwanjelwa ili kufanya vurugu na kuhakikisha uchaguzi mdogo usifanyike.
 
kutokana na hali hiyo hali ya ulinzi na usalama imezidi kuimarishwa kuliko ilivyo kawaida kuanzia maeneo ya mji mdogo wa Mbalizi kuelekea barabara ya Mkwajuni ndani ya jimbo la Songwe na barabara ya kupitia Isanga Mbeya mjini kuelekea makao makuu ya Wilaya kupitia Makongolosi hadi Saza ambapo askari wa kikosi cha kutuliza ghasia wametanda wakiwa na silaha za moto,mabomu,virungu huku wakiwa wamevalia rasmi na ngao kwa ajili ya kukabili hali yeyote itakayojitokeza ya uvunjifu wa amani.
 
Mmoja wa wanachama wa Chadema kutoka Mkwajuni aliyejitambulisha kwa jina moja la Mambwe,ambaye yupo katika maeneo ya Saza anasema kuwa kila kituo kuna askari wanne wa kikosi cha kutuliza ghasia wakiwa wamevalia sare zao rasmi,ngao,mabomu na virungu huku maofisa usalama wakiwa wametanda kila maeneo na kuongeza kuwa ni uchaguzi unaofanywa na wanaccm pekee.
 
Msimamizi wa uchaguzi ambaye ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya,Maurice sapanjo alipopigiwa simu yake ilikuwa ikiita licha ya kumtumia ujumbe mfupi wa maandishi ambao nao hakujibiwa.
 
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya,Diwani Athumani amekanusha madai ya jeshi lake kutumika kwa maslahi ya chama chochote zaidi ya kuangalia hali ya ulinzi na usalama na kuchukuwa majukumu yake hasa pale inapoonekana uvunjifu wa amani na utulivu unatokea na usalama wa watu na mali zao upo hatarini.
 
Kamanda Diwani amesema ni uzushi wa watu wasiopenda amani na amefafanua kuwa jukumu la msingi la Polisi ni kuwalinda watu na mali zao na kwamba juzi mali ziliharibiwa Saza,watu waliumizwa na kufanyika uporaji kwa hiyo nafasi ya polisi katika mazingira hayo ni kuhakikisha hali ya ulinzi na usalama inaimarishwa na kurejesha amani na amesema anaamini kuwa mpenda amani hawezi kuwahofia askari.
 
Mwisho.

watanzania waadhimisha 51 ya uhuru kwaibadarome

WATANZANIA  wanaoishi na kusoma Roma, Jumapili iliyopita tarehe 9 Desemba 2012 wameadhimisha Ibada ya Misa Takatifu kwa ajili ya kusherehekea Miaka 51 ya uhuru wa Tanzania. 

Katikamisa hiyo mahubiri yaliyotolewa na Askofu mkuu Protase Rugambwa, Katibu mwambata wa Baraza la Kipapa la Uinjilishaji wa Watu na Rais wa Mashirika ya Kimissionari ya Kipapa ambapo ibada ilifanyika kwenye Kanisa la Chuo cha Mtakatifu Petro, mjini Roma.

Alisema ni furaha kubwa wanapoadhimisha  Jumapili ya pili ya Majilio ikiwa ni pamoja na kuadhimisha miaka 51 ya Uhuru wa Tanzania ikiwani  pamoja uchaguzi wa Viongozi wa Umoja  wanaosoma rome kadiri ya Katiba inavyowaongoza.

Katika Jumapili hii ya pili ya Majilio, inasikika tena sauti ya nabii inayotangaza furaha iliyowajia waisraeli ambao ilibidi wakombolewe kutoka utumwani Babeli. Nabii Baruku anawatangazia waisraeli kuwa Mungu atawaongoza kwa furaha katika mwangaza wa utukufu wake, kwa ile rehema na haki itokayo kwake. Anawaalika wavue nguo za matanga na huzuni na wavae uzuri wa utukufu utokao kwa Mungu milele. Wajifunge nguo ya haki itokayo kwa Mungu na wajipige kilemba kichwani cha utukufu wake Aliye wa milele.

Katika Injili ya Luka tumeisikia pia Sauti ya Yohana Mbatizaji iliyokuwa inaunguruma nyikani ikiwaalika watu wafanye ubatizo wa toba liletelo ondoleo la dhambi kwa maneno aliyoyaandika Nabii Isaya akisema: “Itengenezeni njia ya Bwana Yanyosheni mapito yake…. Palipopotoka patakuwa pamenyooka, palipoparuzwa patalainishwa; na wote wenye mwili watauona wokovu wa Mungu”.

Katika somo la pili, kama ilivyosikika Jumapili iliyopita, Paulo akiwasifia Watesalonike kwa jinsi walivyoimarika katika imani na upendo kwa Kristo, leo Paulo anawasifia waamini Wafilipi kwa kazi nzuri waliyoifanya ya kuineneza injili na anawaombea ili pendo lao lizidi kuwa jingi sana, katika hekima na ufahamu wote; wapate kuyakabili yaliyo mema; ili wapate kuwa na mioyo safi, bila kosa, mpaka siku ya Kristo; hali wamejazwa matunda ya haki, kwa njia ya Yesu Kristo, kwa utukufu na sifa ya Mungu.

Ndugu zangu waamini, katika kipindi hiki cha Majilio tunaalikwa kwa namna ya pekee tuitayarishe njia ya Bwana anayekuja kutuletea furaha, haki, amani, umoja, mapatano na kila lilo jema. Ni kuiga mfano wa hao manabii kama Baruku na Yohana Mbatizaji, ni kuwa tayari kutangaza furaha inayokuja bila woga tukiambizana, kila mmoja katika nafasi yake na madaraka aliyo nayo, tuwe tayari kuishi na kutenda kadiri atakavyo Mungu.

Kutenda kama walivyofanya Wafilipi ambao Paulo amewasifia. Hapo ndipo tutakapokuwa tunashiriki nasi katika kuuleta ukombozi aliotuletea Bwana wetu Yesu Kristo, anayetangazwa na Mama Kanisa katika kipindi hiki cha Majilio, akitualika tuwe tayari kumpokea na kumpatia nafasi katika maisha yetu ili kazi yake ya ukombozi iendelee kufanyika.

Tumekutana leo pia kwa lengo la kuliombea taifa letu. Tunaposali kuliombea taifa linalofanya maadhimisho ya miaka 51 ya uhuru wake, yapo mambo mawili muhimu yanayoweza kutuongoza vizuri katika maadhimisho haya: kwanza ni shukrani kwa Mungu na jambo la pili ni tafakari juu ya safari yetu kama taifa.

Sisi Watanzania tuna kila sababu ya kumshukuru Mungu. Kwa kipindi hiki chote, taifa letu limeonja baraka nyingi za Mungu. Tumekuwa ni taifa lenye amani na utulivu. Tukiyainua macho yetu na kutazama nje ya mipaka yetu tunajionea wenyewe mataifa ambayo badala ya amani, umoja, mshikamano na ustawi yanaishi katika machafuko, vita na kutoaminiana. Tunazidi kumshukuru Mungu pia kwa ugunduzi wa rasilimali nyingi ambazo zinatufanya tuamini kuwa kama tutakuwa na moyo wa uzalendo, na mipango madhubuti, taifa letu linaweza kunyanyuka kutoka katika lindi la umaskini na kuhesabiwa kati ya mataifa dunia yenye kusimama vizuri.
Hata hivyo, tusingependa kujidanganya kuwa tumepiga hatua kubwa katika kuidumisha misingi hiyo tuliyoiona hapa juu, hata kama tunaweza kusema kwa dhati kabisa kuwa hali yetu si mbaya sana kama ya nchi zinazosambaratika kwa kukosa amani na umoja. Kwa hilo tuna kila sababu ya kumshukuru Mungu.

Lakini tunapomshukuru Mungu kwa mema anayolijalia taifa letu, tunapaswa pia kuitafakari safari yetu ya pamoja kama taifa. Hapo juu nimesema hali yetu si mbaya sana ikilinganishwa na mataifa mengine yanayosambaratika. Kwa maneno mengine, hali yetu pia si nzuri sana, na tunapaswa kuwa makini kuiboresha ili tusiangukie katika migogoro na machafuko.

Tunapenda katika maadhimisho haya kuiombea serikali yetu na watu wake. Tunapenda kuipongeza serikali pale inapotimiza vema wajibu wake na kutambua hatua za maendeleo ya kijamii zinazopigwa na serikali yetu. Tunaona na kutambua pia jinsi serikali yetu inavyojitahidi kuweka mipango madhubuti ya maendeleo. Lakini pia tunaona jinsi ambavyo mipango mingi haitekelezwi kikamilifu.

Katika taifa letu inazidi kujengeka mifumo ya kiuchumi na kisiasa ambayo haileti matumaini ya kulifanya taifa libaki limedumu katika misingi mizuri na madhubuti iliyoanzishwa na waasisi wa taifa letu. Hali hii inalifanya taifa letu, pamoja na kuwa taifa changa, kuanza kuonesha dalili nyingi za kuchoka. Hii ni kwa sababu pale mifumo ya kiutendaji inaposhindwa kuwa sababu ya matumaini, watu huchoka. Watu wanapochoka lolote linaweza kutokea.

Katika siku za hivi karibuni yamezidi kuongezeka matukio ya ukiukwaji wa haki. Tunazidi kushuhudia hali ya raia kukaidi amri za dola na mkono wa dola ukitumia nguvu zinazopitiliza. Tunaendelea pia kushuhudia utamaduni wa kujichukulia sheria mkononi unavyozidi kujengeka katika taifa letu.

Zaidi sana matukio ya vurugu za kidini yanazidi kuongezeka, yakivuka mipaka ya kashfa za maneno dhidi ya dini nyingine na kusababisha uharibifu mkubwa wa mali na kutishia usalama wa taifa kwa ujumla. Vile vile pengo la wenye nacho na wasiokuwa nacho linazidi kuongezeka, na kufanya utawale utamaduni wa ubinafsi na kutokujali.

Haya na mengine mengi yanazidi kuitikisa misingi ya umoja, amani na mshikamano iliyowekwa na waasisi wa taifa letu. Katika mazingira kama haya sote tunapashwa kuwajibika na kuwa sehemu ya ufumbuzi, kwa kuirudia njia sahihi ya mshikamano wa kitaifa, ili tuzidi kulinda amani na umoja, lakini pia kusaidia kuleta ustawi kwa kila mwananchi kwa kujali maslahi ya wote (common good).

Sisi kama waamini tuliosikia leo maneno ya manabii yanayo waalika waisraeli na hivyo kutualika sisi kuzivua nguo za matanga na huzuni na kuvaa nguo za uzuri na utukufu utokao kwa Mungu milele, kutubu na kuifuata njia ya Bwana, hatuna budi kuyatazama hayo tuliyoainisha hapo juu na hasa yale ambayo yanatufanya tubaki katika nguo za matanga na huzuni na tuone ni kwa namna gani tutaweza kushiriki kuyaondoa.

Bila woga, kama alivyofanya Yohani mbatizaji, hatuna budi kuwaalika watu kufanya toba na hili ni kwa kuyakemea kwa ushujaa kabisa, hayo yanayotukosesha uhuru na maendeleo tukabaki tumefungwa kama watumwa na mbaya zaidi kufanywa watumwa na ndugu zetu na watu wetu wenyewe wasiothamini utu wetu na maendeleo ya watanzania wote.

Taifa letu pia lipo katika kipindi mahsusi cha historia yake. Tunajua kuwa sasa nchini pote unaendelea mchakato wa Katiba mpya. Lengo ni kuwa na chombo kitakachosimamia misingi ya uadilifu na uzelendo kulingana na mahitaji ya mazingira ya sasa.

Ni sala yetu kuwa Katiba mpya iwe ni zao la uadilifu na isimamie misingi ya uadilifu inayotetea na kulinda haki na hadhi ya utu wa kila mtu. Hata hivyo, hatuna budi kukumbuka kuwa Katiba isiyoheshimiwa na kuzingatiwa kwa dhati inakuwa imepokonywa uhai wake.

Tunapaswa kama taifa kujenga pia utamaduni wa kuheshimu katiba na kuzingatia taratibu zinazotuongoza. Hata katika hili tujiulize, sisi tuko wapi na tumesimama wapi katika kuchangia, hasa katika yale ambayo tunafikiri ni muhimu yakatiliwa msisitizo na yaonekane wazi katika Katiba itakayotuongoza.

Nilipokutana nanyi kwa mara ya kwanza niliwaalika tuone ni kwa namna gani nasi twaweza kushiriki kikamilifu katika mchakato wa marekebisho ya Katiba. Naamini viongozi wrtu, na hasa hao watakaochaguliwa, watakuwa mstari wa mbele kutuingiza katika mawasiliano na wataalamu ambao waweza kutusaidia ili nasi tuwe tayari kutoa mchango wetu.

Katika haya yote, tunaona wazi kuwa taifa letu linapaswa kuitafuta upya ile fahari ya miaka ya kwanza ya uhuru wetu, ambapo wazo lililotawala lilikuwa ni ujenzi wa taifa lililoshikamana katika nyanja zote na nyezo kuu katika ujenzi huo wa taifa ilikuwa ni moyo wa uzalendo.

Maadhimisho ya kumbukumbu ya uhuru yanapaswa kuwa ni fursa ya kutoa matumaini ya kuijenga safari yetu kuelekea lengo la ustawi wa taifa letu na kukuza moyo wa kujali maslahi ya wote.

Baba Mtakatifu Benedikto 16 katika hati yake Spe Salvi anasema: “Wakati wa sasa, hata kama ni mgumu, tunaweza kuuishi na kuukubali kama unatuelekeza kwenye lengo, kama tunaweza kuwa na hakika na lengo hilo, na kama lengo hilo ni kubwa ya kutosha kuweza kuhalalisha jitihadi ya safari” (Spe Salvi, 1).

Changamoto zinazolikabili taifa letu tuzitumie kama kichocheo cha kujirekebisha na kujizatiti katika ujenzi wa taifa. Uhuru unaotoa matumaini ni kichocheo muhimu katika kuvishinda vikwazo vinavyotaka kutuzuia tusilifikie lengo la taifa.

Utume wa Kanisa katika Tanzania na kwetu pia tulio nje ya Tanzania katika kipindi hiki ni hasa kuwasaidia watu kuutambua wajibu wanaokuwa nao kwa Mungu na kwa taifa, kama walivyofanya hao manabii, kwa kusema, kukemea, kufariji na kutia moyo kwa yale yote waliyoona ya kujenga na kufaa, na yale ambayo hayakuwa na mwelekeo wa kujenga.

Ndugu zangu, nasi tuige mfano wa hao walioamini, wakawa na upendo kwa Mungu na Kristo Mkombozi wetu na tuhakikishe kuwa yale yaliyo na thamani na yatakayo tukomboa tunayakuza na kuyaendeleza na yaliyo kinyume chake tusiyape nafasi na tuwe tayari kuyapinga na kuyakemea. Tuitengeneze njia ya Bwana na kuyanyosha mapito yake ili wote wenye mwili wauone wokovu wake.

Tumsifu Yesu Kristo.


Jimbo Katoliki Mbeya lapata Mashemasi Wapya sita!



Askofu Evaristo Chengula wa Jimbo Katoliki Mbeya, ametoa daraja takatifu la Ushemasi kwa Mafrateri sita waliokuwa wanasoma Seminari kuu ya Kipalapala na Peramiho baada ya kuhitimu sehemu hii ya kwanza ya majiundo yao ya Kipadre. Ibada hii imefanyika kwenye Kanisa kuu la Mtakatifu Anthony wa Padua, Jimbo Katoliki Mbeya.

Katika mahubiri yake, Askofu Chengula, amewataka waamini kujitosa kwa hali na mali ili kujenga Kanisa linalowategemea sana, hasa wakati huu wa maadhimisho ya Mwaka wa Imani sanjari na kumbu kumbu ya maadhimisho ya Jubilee ya Mtaguso Mkuu wa Pili wa Vatican, ambao unatoa mwongozo wa pekee kwa waamini walei kushiriki kikamilifu katika maisha na utume wa Kanisa. Umoja na mshikamano wa dhati ni matunda ya Roho Mtakatifu kwa Kanisa.

Waamini wanachangamotishwa na Mama Kanisa kujenga na kudumisha umoja, upendo na mshikamano wa dhati na wachungaji wao, daima wakiwa mstari wa mbele kutolea ushuhuda wa imani tendaji badala ya kuendekeza majungu na migawanyiko isiyokuwa na tija wala maendeleo na ustawi kwa Kanisa. Imani hii kwa namna ya pekee, ijioneshe kwa kuiungama, kuiadhimisha, kuiishi na kuisali. Waamini walipambe Kanisa kwa njia ya matendo na maisha yao adili.

Mashemasi wapya ni Karolo Betold Ilonga kutoka Seminari kuu ya Kipalapala.
Shemasi Francisko Edward Ngao kutoka Seminari kuu ya Peramiho.
Shemasi Simoni Msompa kutoka Seminari kuu ya Peramiho.
Shemasi Thomas Mwampamba kutoka Seminari kuu ya Segerea.
Shemasi Augustino Kanku Lukusa wa Shirika la Marafiki wa Kristo.



Mwisho.

Padre Mapela achaguliwa kuwaongoza wakatoliki Rome

 

Umoja wa Wanafunzi Wakatoliki Watanzania wanaosoma na kuishi mjini Roma, Jumapili tarehe 9 Desemba 2012 pamoja na kusherehekea miaka 51 ya uhuru wa Tanzania, pia walifanya uchaguzi mkuu wa viongozi ambao wamepewa dhamana ya kuongoza Umoja huu kwa kipindi cha Mwaka mmoja.

Msimamizi wa uchaguzi uliongozwa na Mheshimiwa Padre Philip Massawe mmoja wa walezi wa wanafunzi hao na kuhudhuriwa pia na Askofu mkuu Protase Rugambwa, Katibu Mwambata wa Baraza la Kipapa la Uinjilishaji wa Watu na Rais wa Mashirika ya Kimissionari ya Kipapa.

Askofu mkuu Rugambwa amewashukuru na kuwapongeza viongozi waliopita kwa kujitoa kimasomaso kuendeleza umoja na mshikamano wa wanafunzi watanzania wanaosoma mjini Roma. Anawaalika viongozi wapya kukuza nguvu ya umoja na udugu ili kukabiliana na changamoto za malimwengu na ubinafsi ambao ni sumu ya maendeleo katika kukuza na kuendeleza mshikamano, maridhiano na umoja.

Hizi ni tunu ambazo zinapaswa kutangazwa kwa nguvu zote, lakini zaidi lazima zimwilishwe katika uhalisia wa maisha. Uongozi ni dhamana inayohitaji majitoleo na nidhamu ya hali ya juu. Wakati mwingine si rahisi kupokea dhamana hii.

Yafuatayo ni majina  mapya yaliyochaguliwa kuongoza Umoja wa Wanafunzi Watanzania Wakatoliki wanaosoma Roma:

Padre Moses Mapela kutoka Jimbo kuu la Mwanza anakuwa Mwenyekiti mpya.
Padre Alister Makubi kutoka Jimbo kuu la Dar es Salaam anakuwa Katibu.
Sr. Theresa Tarimo kutoka Shirika la Kazi za Roho Mtakatifu: mtunza hazina.
Padre Joseph Mahela kutoka Shirika la Kazi za Roho Mtakatifu: Liturujia.
Padre Nikodemo Mayala: Mkutubi.


Mwisho.

mizengwe yatawala uchaguzi mdogo Jimbo la Songwe,wilayani Chunya


Na Thompson Mpanji,Chunya
 
ULE usemi usemao mfa maji haishi kutapatapa na dalili za mvua ni mawingu umeanza kuonekana mapema katika jimbo la Songwe wilayani Chunya, ambapo kunatarajiwa kufanyika uchaguzi mdogo wa Mwenyekiti wa Kijiji cha saza na vitongoji viwili kutokana na wananchi kumtuhumu Mbunge wa Jimbo hilo Philipo Mulugo kuagiza kuhakikisha Chama cha Mapinduzi (CCM) kinashinda kwa gharama yeyote na kwa aina yeyote alimradi Jimbo hilo lisiingie dosari ya kushikwa na vyama vya upinzani hali ambayo inaelezwa na wachambuzi wa kisiasa kuwa ndiyo kwisha kisiasa.
 
Ujumbe mmoja kutoka kwa kada wa Chama cha mapinduzi (CCM) uliofanikiwa kunaswa na gazeti hili unasema kuwa,"Nilijaribu kuongea na usalama uchaguzi usimamishwe hadi mazungumzo ya mezani yatakapochukuwa nafasi wakaelewa ila wansema kesho (Desemba,10) uchaguzi."
 
Wanaodaiwa kukamatwa na Jeshi la Polisi wilayani Chunya ni pamoja na Diwani viti maalum Kata ya Kanga,Katibu wa Chadema wilaya ya Chunya Bryson Mwansimba,wagombea wawili wa kitongoji cha saza kati ambaye ni Mwenyekiti wa Chadema Kata ya kanga John Mponzayo,Katibu mwenezi wa Chadema Kata ya Kanga Suleimani Tanganyika,Katibu Mwenezi Kata,Amosi Tanganyika aliyekuwa anagombea Mwenyekiti wa kitongoji cha Saza kibaoni, wasanii waliofika na gari la matangazo na mpiga picha aliyefahamika kwa jina moja la Chris.
 
Tafsiri hizo kwa wachambuzi wa masuala ya kisiasa zimekuja kufuatia kukamatwa kwa Viongozi,wanachama,wapenzi na watu wanaofanya kazi na Chama cha Demokrasia na maendeleo (CHADEMA),wilayani Chunya ambao wanadaiwa kukamatwa kwa madai ya kusababisha uvunjifu wa amani na utulivu katika kampeni za uchaguzi mdogo wa Mwenyekiti wa Kijiji cha Saza na vitongoji viwili juzi.
 
Katika kampeni hizo zinazodaiwa kufungwa kwa amani na utulivu Desemba,4 mwaka huu majira ya saa 11 jioni viongozi hao wanadaiwa kukamatwa saa 9 usiku katika nyumba za kulala wageni na wengine majumbani mwao ambapo gari tano za jeshi la polisi aina ya 110 Defender zikiwa na askari zinadaiwa kuonekana kufanya doria mithili ya operesheni ya kusaka majambazi lakini kumbe ilikuwa inafanyakazi kubwa ya kuhakikisha Chama cha mapinduzi kinashinda.
 
"Haikuweza kufahamika mara moja kuwa kwanini kulikuwepo na askari lukuki na gharama za mafuta na posho kwa magari na askari polisi zinatokea wapi ingawa kulikuwepo na tetesi kuwa mamilioni kadhaa yamemwagwa kuhakikisha lengo la kuilinda CCM linatimia,"kilisema moja ya chanzo cha habari kutoka Saza, Chunya.
 
Kutokana na kuibuka kwa sintofahamu hiyo baadhi ya wachambuzi wa masuala ya kisiasa wanasema kuwa kitendo kinachoendelea kufanyika Jimbo la Songwe kulazimisha uchaguzi kufanyika Desemba,10,2012 licha ya Chadema kumwandikia barua msimamizi wa uchaguzi huo Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya,Maurice Sapanjo kutokubaliana na kuwepo kwa uchaguzi huo kutokana na kukiukwa kwa sheria za uchaguzi bado inaonesha dhahiri ni shinikizo kutoka kwa Mbunge huyo ambaye anadaiwa kusikika akisema lazima CCM ipite kwa gharama yeyote.
 
"Tulisikia juu juu maneno kuwa zimemwagwa Mil.10 kuhakikisha mafuta kwa ajili ya magari na posho za kutosha kwa watakaoendesha zoezi la kufanikisha ushindi wa kishindo kwa CCM,mimi pia nipo mafichoni kwa sababu ni miongoni mwa watu waliowekwa katika orodha kuwa lazima tukamatwe na kuswekwa mahabusu kwa sababu tunatishia kibarua chake cha ubunge lakini unadhani nini kitafuata kama siyo kuzijaza hasira ndugu,,jamaa na marafiki zetu tunaosaidiana kwa hali na mali,hiki ni kifo cha CCM Jimbo la Songwe," kilisema chanzo kingine.
 
Aliongeza, "Unajuwa mbinu wanazotumia baadhi ya wagombea ubunge za kupita bila kupingwa ni kuwaweka sawa baadhi ya viongozi wa upinzani ili wasisimamishe wagombea na hivyo kuonekana wanapita bila kupingwa jambo ambalo siyo kweli huku wakidai rafu hizo zitadhihirika 2015 itakapokuja kuanguka CCm jimbo Songwe kifo cha mende."
 
Akizungumza na gazeti Katibu Mwenezi wa Chama cha Demokrasi na maendeleo(CHADEMA),wilaya ya Mbeya Lucas Mwampiki hilo alisema walishamwamndikia barua msimamizi wa uchaguzi mdogo wa Kata ya saza,Maurice Sapanjo ambaye ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya kutokubaliana kufanyika uchaguzi huo kutokana na madai matano ya ukiukwaji wa sheria za uchaguzi lakini amepuuza.
 
Mwampiki ambaye ni Diwani wa Kata ya Mwakibete aliyataja makosa hayo ni pamoja na 1.kuandikisha watu wanaojuwa kusoma na kuandika 100 huku wote wanajuwa kusoma na kuandika,kutowahusisha viongozi au vyama kujuwa na kukagua vituo vya kupigia kura,3.kutowatambulisha wasimamizi wa vituo kwa wagombea au vyama vyao, kutopokea,kuwapa voapo wala kupokea orodha ya mawakala wa vyama pinzani,5.kutokujibu barua za malalamiko za wagombea au vyama kwa wakati.
 
Katibu huyo alitaja rafu iliyochezwa na CCM katika vituo vya kupigia kura ni kuongeza majina bandia ya wapiga kura ambapo katika kituo cha Saza kati wapiga kura waliojiandikisha walikuwa 96 waliongeza majina bandia 32 na kufanya idadi kufikia 128,kituo cha Bwana mzungu walioandikisha kihalali walikuwa 86,majina bandia 38 na kufanya idadi kuwa wapiga kura 124,kituo cha kibao 99 majina yaliyoongezwa 27 na kuwa jumla ya watu 126,kituo cha bwawani 98 waliongeza majina bandia 47 kwa hiyo watu waliowaongeza ni 144 ambapo ni vituo viwili vya Mwembeni na makambini hawakupata idadi.
 
"Watu walioandikishwa na kuongeza 844 kura zao (CCM)zilikuwa 744,kura za Chadema 100 walivyopanga matokeo yaani huo ndiyo ushindi waliojipangia.wananchi wamechoma moto na kuchana karatasi za kupigia kura baada ya kutoridhika na rafu zinazochezwa,"alisema Katibu.
 
Alisema hiyo ni idadi iliyotengenezwa kwa ajili ya ushindi kwa kuchukuwa katika kura za maoni ndani ya CCM na walichoshangazwa ni kupelekwa magari aina ya defender tano, mbili zilirudi Mbeya mjini na tatu zilirudi chunya,wamelazimisha leo (Desemba,10)ufanyike ni wao,vyombo vya ulizi na usalama vinahusika,kijiji cha saza kina malalamiko ya uuzwaji wa kifusi cha mchanga wa dhahabu kwa Sh.Mil.392,shinikizo ni kwa viongozi wakuu wa serikali na mtoto mmoja wa kigogo kwa gharama yeyote lazima ushindi.
 
"Nawaonya ccm hatutarudi nyuma kudai haki za wanyonge,haturudi nyuma kupigania haki za watanzania ndiyo wanatuchochea zaidi,ccm waache kutegemea vyombo vya dola na kama kweli wangekuwa wanataka haki mbona katika majukwaa yao hawasemi haki wanang'angaania amani na utulivu ,wajuwe amani na utulivu haviwezi kuja bila kutimiza ama kutekeleza haki,navishauri vyombo vya dola waache kufanyakazi ya CCM waache kufanyakazi kwa mazoea,wasiwe chanzo cha kuvuruga amani,"alisema.
 
Wakati yakiwa yametendeka,Hali ya ulinzi na usalama imezidi kuimarishwa kuliko ilivyo kawaida kuanzia maeneo ya mji mdogo wa Mbalizi kuelekea barabara ya Mkwajuni ndani ya jimbo la Songwe na barabara ya kupitia Isanga Mbeya mjini kuelekea makao makuu ya Wilaya kupitia Makongolosi hadi Sawa ambapo askari wa kikosi cha kutuliza ghasia wametanda wakiwa na silaha za moto,mabomu,virungu huku wakiwa wamevalia rasmi na ngao kwa ajili ya kukabili hali yeyote itakayojitokeza ya uvunjifu wa amani.
 
Kwa mujibu wa mshuhuda wamesema kuwa ulinzi huo umeimarishwa kufuatia kuwepo kwa tetesi kuwa wanachama wa Chadema kutoka Tunduma na Mwanjelwa jijini Mbeya wamepanga kuvamia jimboni Songwe kuhakikisha wanafanya vurugu ili uchaguzi usifanyike.
 
Mmoja wa wanachama wa Chadema kutoka Mkwajuni aliyejitambulisha kwa jina moja la Mambwe,ambaye yupo katika maeneo ya Saza anasema kuwa kila kituo kuna askari wanne wa kikosi cha kutuliza ghasia wakiwa wamevalia sare zao rasmi,ngao,mabomu na virungu huku maofisa usalama wakiwa wametanda kila maeneo na kuongeza kuwa ni uchaguzi unaofanywa na wanaccm pekee.
 
"Hali huku siyo shwari wanafanya uchaguzi wa CCM uliolazimishwa na Msimamizi wa uchaguzi wa Wilaya Sapanjo,amepita kutangaza leo kuwa lazima uchaguzi ufanyike na wanapita kuwalazimisha wanachama kwenda kupiga kura,picha za wagombea wa chadema hakuna zimebaki za wagombea wa CCM,nikwambie mizengwe ilianza tangu Desemba,3 walimwagwa maofisa usalama na kufuatilia kila mkutano wa Chadema,,Polisi waliingia tangu Desemba,8 majira ya saa 10 jioni na vitisho vyao utadhani kuna vita,"alisema Mambwe.
 
Msimamizi wa uchaguzi huo ambaye pia Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya chunya,Sapanjo alipopigiwa simu hakuweza kupokea licha ya kutumiwa ujumbe mfupi wa maandishi kuhusu madai ya ukiukwaji wa sheria za uchaguzi katika uchaguzi huo mdogo wa Kijiji cha saza na vitongoji vyake viwili hakuweza kujibu.
 
Mbunge wa jimbo la Songwe ambaye pia ni Naibu waziri wa Elimu na mafunzo ya ufundi,Philipo Mulugo alipoulizwa kuhusiana na madai hayo dhidi yake alijibu kwa kuhoji"nani anayelalamika?Mimi ni Mbunge wa eneo husika ni lazima nihakikishe chama changu kinapata ushindi mnono kwa kufanya kampeni zinazofuata taratibu za uchaguzi,sasa hao wanaosema mamilioni wameyaona wapi?."
 
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya,Diwani Athumani amekanusha madai ya jeshi lake kutumika kwa maslahi ya chama chochote zaidi ya kuangalia hali ya ulinzi na usalama na kuchukuwa majukumu yake hasa pale inapoonekana uvunjifu wa amani na utulivu unatokea na usalama wa watu na mali zao upo hatarini.
 
"Ni uzushi,nikukumbushe tu kuwa jukumu la msingi la Polisi ni kuwalinda watu na mali zao.juzi mali ziliharibiwa Saza,watu waliumizwa na uporaji ukafanywa.unadhani ni ipi nafasi ya ya polisi katika mazingira hayo? Naamini kuwa mpenda amani hawezi kuwahofia askari,"alisema kamanda Diwani.
 
Mwisho.
 
 

Friday, December 7, 2012

picha za ajali ya Mbeya

stendi  ya dala dala ya njia panda  ya Itende,kalobe ambapo dala dala inaonekana ikisimama  huku sentimenta chache gari nyingine zikipita katika eneo hilo ambalo ni muda mfupi tu zimegongwa dala dala mbili na kusababisha vifo vya watu wawili na wengine 10 kujeruhiwa,wananchi wanailalamikia stendi hiyo kuwepo  jirani na barabara kuu ya Mbeya/Zambia jambo linalosababisha kutokea kwa  ajali mara kwa mara

siyo paa la nyumba ni  basi dogo la abiria

Bora salama kwa pembeni

hiace Bora salama kwa mbele

hiace kubwa iliyoandikwa bora salama kwa ndani

lori kwa mbele

lori likionekana kwa nyuma baada ya kusimama  katika eneo la Iyunga  umbali wa nusu kilomita baada ya kusababisha ajali


lori liliumia kidogo

Leyland DAF likiwa limesimama  baada ya ajali huku askari wa usalama barabarani akiendelea na ukaguzi

shuhuda wa mwanzo mwisho wa ajali kibopile akionesha alipokuwa amekaa katika kiti chake

wananchi wakishuhudia ajali hiyo
kiti cha mbele cha abiria katika hiace ndogo kikionekana kilivyotapakaa damu

hiace ndogo pichani

picha hiace ndogo

nyaya zinazodaiwa za mfumo wa breki zilizokatika katika lori

Hiace ndogo

picha inaonesha gari la mizigo liliposimama (halipo pichani) baada ya kugonga dala dala mbili maeneo ya njia panda ya Itende,kalobe kama inavyoonekana kwa mbali katika mwinuko  na kusababisha vifo vya watu wawili na 10 kujeruhiwa vibaya (Picha zote na Thompson Mpanji,Mbeya)

JINAMIZI LA AJALI LAENDELEA KUUTESA MKOA WA MBEYA. Wawili wapoteza maisha, werngine kumi wajeruhiwa vibaya.




Moses Ng’wat na Thompson Mpanji, Mbeya.

WATU wawili , akiwemo mtoto  mdogo wamepoteza maisha na  wengine 10 kujeruhiwa vibaya katika ajali, mkoani Mbeya , baada ya Lori la mizigo kuzigonga na kuzitumbukiza Mtaroni Daladala mbili zilizokuwa zimeegeshwa kituoni.

Tukio hilo lilitokea jana majira ya saa 5:30 katika eneo la Kalobe baada ya Lori la Mizigo lenye namba za usajili T 7821 BVD  lililokuwa likielekea nchini Zambia kuzigonga gari mbili za abiria (Daladala) zenye namba za usajili T 945 AFJ na T 150 AJL  zilizokuwa zimeegeshwa katika kituo cha Njia Panda eneo la Kalobe Jijini hapa.

Kwa mujibu wa Muuguzi Mkuu wa Hospitali ya Ruufaa ya Mbeya, Thomas Isidory, alithibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kwamba walipokea maiti ya mtu mmoja ambaye hata hivyo jina lake halikuweza kupatikana licha ya kukutwa na tiketi yenye jina moja la Joshua, huku kifo cha mtoto huyo mdogo kilitokea wakati akipatiwa matibabu katika chumba cha wagonjwa mahututi (ICU).

Alisema kwa upande wa majeruhi waliopokelewa Hospitalini hapo,  walikuwa 10,  ambapo kati ya hao wawili hali zao zilikuwa mbaya na wamelazwa katika chumba cha wagonjwa mahututi wenye kuhitaji uangalizi maalumu (ICU).

Hata hivyo Isidory  alisema kati ya hao waliolazwa chumba cha wagonjwa mahututi ni mmoja tu aliyetambuliwa  kwa jina la Jane Mligo(19), ambaye ni mwanafunzi wa chuo cha ufundi VETA Mbeya, ambapo mwingine hakuweza kutambuliwa mara moja.

Aliwataja majeruhi wengine nane ambao wamelazwa katika Wodi za kawaida hospitalini hapo kuwa ni Jose Kalale (28) ambaye ni dereva wa moja ya Daladala hizo mbili zilizogongwa zikiwa kituoni, pamoja na Kondakta wake Elia Ambakisye.

Wengine ni Willy Claud (34), Winnie Ipyana(22), God Sanga (23), Josia Choga (28), Said Omary (18), pamoja na  mtoto mdogo, Nasra Japhary, ambaye hata hivyo umri wake haukuweza kupatikana mara moja .

Kwa upande wake mmoja wa majeruhi hao waliolazwa hospitalini hapo katika wodi namba moja, Josiah Choga, akisimulia tukio hilo, alisema yeye alikuwa akitokea katika Mji wa Mwanjelwa na walipofika eneo la Kalobe Daladala aliyopanda iliegesha kituoni wakati watu wakishuka na ghafla alisikia kishindo kikubwa kikitokea kwa nyuma .

“Pale kituoni kulikuwa na Daladala Mbili yakwetu ilikuwa mbele ghafla nilisikia kishindo kikubwa na nilipojaribu kugeuka nyuma nilishangaa Daladala tuliyokuwemo ikipigwa na kuanza kubingilika hadi mtaroni” alisimulia Chonga.

Aliongeza kuwa wakati akiwa wamefunikwa ndani ya Mtaro alishangaa kundi la watu wakifika na kuanza kuwachomoa toka ndani ya Daladala hilo huku akishuhudia baadhi ya abiri wakichuruzika damu nyingi mwilini mwao.

Naye Nsubiri Kibopile, ambaye ni mashuhuda wa ajali hiyo, alisema Roli hilo liliziparamia Daladala hizo baada ya kulikwepa gari lililokuwa likitokea mbele yake ambalo lilikuwa limebeba shehena ya vinywaji  vya moja ya kampuni ya vinywaji baridi.

“Huyu bwana wa Roli anaonekana tayari alikuwa ameharibikiwa na Breki hivyo akawa anashuka nalo na alipofika hapa kituoni aliojikuta akibanwa na lile fuso  lililobeba Soda  hivyo kuamua kutanua  na ndipo alipozivaa zile Daladala na kuzitumbukiza Mtaroni” Alisema Kibopile.

Hata hivyo baadhi ya askari wa kikosi cha usalama barabarani waliokuwepo katika eneo la tukio waliozungumza na Jambo Leo kwa masharti ya majina yao kutoandikwa gazetini kwa kuwa wao si wasemaji wa jeshi hilo, walidai ajali hiyo ilisababishwa na Roli hilo la mizigo baada ya kuharibika mfumo wa Breki.

“’Unajua hilo Roli lazima lilikuwa ‘limefeli’  ndio maana baada ya kuzigonga zile Daladala lilienda kusimamia mbali zaidi ya nusu kilomita, hata hivyo tunamshukuru mungu madhara hayakuwa makubwa kwani lingeweza kuacha njia na kwenda kuvamia  nyumba ” alisema mmoja wa askari hao.

Mwisho.