Na Thompson Mpanji,Chunya
MBUNGE wa Jimbo la Songwe(NEC),Mh.Philipo Mulugo amekanusha madai
ya Chama cha Demokrasia na maendeleo(CHADEMA) Mbeya amemwaga mamilioni
ya fedha kuhakikisha Chama Cha Mapinduzi (CCM) kinashinda katika
uchaguzi mdogo wa Kijiji cha Saza na vitongoji vyake,wilayani Chunya
sanjari na kuhakikisha Jeshi la polisi limewatia mbaroni viongozi wake
wakiwemo na wagombea.
Baadhi ya wanachama na viongozi wa vyama vya upinzani wamemtuhumu
Mh.Mulugo kuhusika na maagizo ya kukamatwa kwa viongozi hao kuwaita
maofisa usalama wa taifa waliomwagwa katika kampeni za uchaguzi huo
kuanzia Desemba,3,2012 siku ya uzinduzi sanjari na nguvu kubwa
iliyotumika ya magari zaidi ya matano ya polisi aina ya 110 defender na
askari Polisi wa kikosi cha kutuliza ghasia (FFU) yaani fanya fujo uone
wakivalia 'magwanda' ya kutisha na kofia ngumu
(element),ngao,mabomu,silaha za moto na virungu, ambapo walifika ameneo
hayo Desemba,8 majira ya saa 10 jioni.
Kufuatia madai hayo Mbunge Mulugo ambaye ni Naibu waziri wa Elimu
na mafunzo ya ufundi amekanusha vikali na kuhoji "nani
anayelalamika?,huku akijigamba kuwa yeye kama Mbunge wa eneo husika ni
lazima ahakikishe chama chake CCM kinapata ushindi mnono kwa kufanya
kampeni zinazofuata taratibu za uchaguzi, na kuendelea kuhoji kuwa
wanosema amemwaga mamilioni wameyaona wapi?."
Katibu mwenezi wa Chadema Wilaya ya Mbeya,Mh.Lucas Mwampiki ambaye
pia na Diwani wa kata ya Mwakibete jijini Mbeya amedai askari hao
walimwagwa kutokana na shinikizo la Mbunge kuhakikisha CCM inashinda na
kuhakikisha baadhi ya Viongozi na wanachama wanakamatwa ili kupunguza
kasi ya wapinzani na waogope kwenda katika mikutano ya kampeni.
Amewataja Viongozi waliokamatwa na Jeshi la Polisi wilayani Chunya
ni pamoja na Diwani viti maalum Kata ya Kanga,Katibu wa Chadema wilaya
ya Chunya Bryson Mwansimba,wagombea wawili wa kitongoji cha saza kati
ambaye ni Mwenyekiti wa Chadema Kata ya kanga John Mponzayo,Katibu
mwenezi wa Chadema Kata ya Kanga Suleimani Tanganyika,Katibu Mwenezi
Kata,Amosi Tanganyika aliyekuwa anagombea Mwenyekiti wa kitongoji cha
Saza kibaoni, wasanii waliofika na gari la matangazo na mpiga picha
aliyefahamika kwa jina moja la Chris.
Mwampiki alisema walishamwandikia barua msimamizi wa uchaguzi mdogo
wa Kata ya saza,Maurice Sapanjo ambaye ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya
wilaya ya Chunya kutokubaliana kufanyika uchaguzi huo kutokana na madai
matano ya ukiukwaji wa sheria za uchaguzi lakini amepuuza na uchaguzi
unafanyika leo.
Ametaja baadhi ya mambo yaliyokiukwa ni pamoja na 1.kuandikisha
watu wanaojuwa kusoma na kuandika 100 huku wote wanajuwa kusoma na
kuandika,kutowahusisha viongozi au vyama kujuwa na kukagua vituo vya
kupigia kura,3.kutowatambulisha wasimamizi wa vituo kwa wagombea au
vyama vyao, kutopokea,kuwapa voapo wala kupokea orodha ya mawakala wa
vyama pinzani,5.kutokujibu barua za malalamiko za wagombea au vyama kwa
wakati.
Katibu huyo ametaja rafu iliyochezwa na CCM katika vituo vya
kupigia kura ni kuongeza majina bandia ya wapiga kura ambapo katika
kituo cha Saza kati wapiga kura waliojiandikisha walikuwa 96 waliongeza
majina bandia 32 na kufanya idadi kufikia 128,kituo cha Bwana mzungu
walioandikisha kihalali walikuwa 86,majina bandia 38 na kufanya idadi
kuwa wapiga kura 124,kituo cha kibao 99 majina yaliyoongezwa 27 na kuwa
jumla ya watu 126,kituo cha bwawani 98 waliongeza majina bandia 47 kwa
hiyo watu waliowaongeza ni 144 ambapo ni vituo viwili vya Mwembeni na
makambini hawakupata idadi.
Amesema CCM imeandaa matokeo na kufanya idadi ya watu
walioandikishwa kihalali kufikia 844 badala ya 744 na matokeo
wameyapanga kuwa CCM itaibuka kidedea kwa kupata kura za kishindo 744
dhidi ya Chadema watakaoanguka vibaya kwa kupata kura 100 na kwamba
kijiji cha saza kina malalamiko ya uuzwaji wa kifusi cha mchanga wa
dhahabu kwa zaidi ya Sh.Mil.392 walizonufaika viongozi wachache kwa hiyo
ili kuepuka kashfa hiyo wameona njia pekee ni kucheza rafu.
.Hata hivyo Katibu huyo ameionya CCM kuwa Chadema haitarudi nyuma
kudai haki za wanyonge,haitarudi nyuma kupigania haki za watanzania na
matokeo yake wanawachochea zaidi kuelekeza nguvu zao Jimbo la
Songwe,waache kutumia vyombo vya dola sanjari na kuvishauri vyombo vya
dola kuacha kufanyakazi ya CCM waache mazoea,wasiwe chanzo cha kuvuruga
amani.
Wakati huo huo,kumekuwepo na hofu ya uvunjifu wa amani
na utulivu katika Kijiji ch Saza,Kata ya Saza,wilayani Chunya kutokana
na madai ya Chama cha demokrasia na maendeleo( CHADEMA)kudaiwa kukodi
makundi ya vijana,wanachama na wanaharakati kutoka mpakani mwa Zambaia
na Tanzania Tunduma na Mwanjelwa ili kufanya vurugu na kuhakikisha
uchaguzi mdogo usifanyike.
kutokana na hali hiyo hali ya ulinzi na usalama imezidi kuimarishwa
kuliko ilivyo kawaida kuanzia maeneo ya mji mdogo wa Mbalizi kuelekea
barabara ya Mkwajuni ndani ya jimbo la Songwe na barabara ya kupitia
Isanga Mbeya mjini kuelekea makao makuu ya Wilaya kupitia Makongolosi
hadi Saza ambapo askari wa kikosi cha kutuliza ghasia wametanda wakiwa
na silaha za moto,mabomu,virungu huku wakiwa wamevalia rasmi na ngao kwa
ajili ya kukabili hali yeyote itakayojitokeza ya uvunjifu wa amani.
Mmoja wa wanachama wa Chadema kutoka Mkwajuni aliyejitambulisha kwa
jina moja la Mambwe,ambaye yupo katika maeneo ya Saza anasema kuwa kila
kituo kuna askari wanne wa kikosi cha kutuliza ghasia wakiwa wamevalia
sare zao rasmi,ngao,mabomu na virungu huku maofisa usalama wakiwa
wametanda kila maeneo na kuongeza kuwa ni uchaguzi unaofanywa na wanaccm
pekee.
Msimamizi wa uchaguzi ambaye ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya
ya Chunya,Maurice sapanjo alipopigiwa simu yake ilikuwa ikiita licha ya
kumtumia ujumbe mfupi wa maandishi ambao nao hakujibiwa.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya,Diwani Athumani amekanusha madai ya
jeshi lake kutumika kwa maslahi ya chama chochote zaidi ya kuangalia
hali ya ulinzi na usalama na kuchukuwa majukumu yake hasa pale
inapoonekana uvunjifu wa amani na utulivu unatokea na usalama wa watu na
mali zao upo hatarini.
Kamanda Diwani amesema ni uzushi wa watu wasiopenda amani na
amefafanua kuwa jukumu la msingi la Polisi ni kuwalinda watu na mali zao
na kwamba juzi mali ziliharibiwa Saza,watu waliumizwa na kufanyika
uporaji kwa hiyo nafasi ya polisi katika mazingira hayo ni kuhakikisha
hali ya ulinzi na usalama inaimarishwa na kurejesha amani na amesema
anaamini kuwa mpenda amani hawezi kuwahofia askari.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment