Translate

Thursday, January 31, 2013

Mwanamke anayedaiwa kumuuza mtoto aibuka mafichoni aweka mambo hadharani ni baada ya kumnasa anapoishi na mgahawani,Mama mkubwa anayedaiwa kuwa msimamizi wa kituo cha yatima naye aibukia katika semina ya kiroho atoa ufafanuzi

Na Thompson Mpanji,Mbeya
SAKATA la mwanamke mmoja Mkazi wa Mtaa wa Ikuti,Kata ya Iyunga, jijini Mbeya kutuhumiwa kumuuza mtoto aliyemzaa mwenyewe kwa raia wa kigeni wanaomiliki kituo kimoja cha watoto yatima cha jijini hapa limezidi kuchukuwa sura mpya kunaswa na mwandishi wa habari hizi akiwa mafichoni na kuweka mambo hadharani huku anayedaiwa kuwa msimamizi wa kituo cha Care and Share-Children's home Anna Kasile akiibukia katika semina ya Makatekista akikiri kumsaidia mwanamke huyo na amekuwa akizushiwa kuuza watoto.
Aidha Anna Kasile ambaye anadaiwa kuwa ni mama mkubwa,msimamizi wa kituo aliyedaiwa kuwa muda wote na wazungu hao amepasua ukweli katika semina ya Mapadre,watawa wa kike na kiume na makatekista kuhusu kilichotokea.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi,Amina Nganile (29)ambaye anafanyakazi ya kupika chakula katika mgahawa wa baa moja iliyopo katikati ya Mwanjelwa na Kabwe (jina tunalihifadhi),jijini hapa alikiri kuingia mkataba wa kutunza mimba na wazungu waliopelekwa na Mama yake mkubwa (Anna Kasile) baada ya kuuguwa nusuraya kufa.
Amina alisema yeye ni mama wa watoto wawili akiwemo Agapto mwenye umri wa miaka minne na huyo aliyemzaa Novemba,2013 ambaye anatunzwa katika kituo cha care and share cha Simike kinachosimamiwa na Kasile ambaye ni mama yake Mkubwa.
"Sina hamu na wanaume kwa sababu aliyenizalisha awali hamtunzi mtoto na huyu aliyenizalisha anaitwa Amos Mfanyakzi wa stela Farm ni mkazi wa Kyela hajanitunza wakati wa mimba,niliugua nusura nipoteze maisha na hivyo nilitaka kuitoa lakini Mama Kasile alinisaidia kunipeleka Hospitali wakanipima Ultra Sound na kukuta mtoto yupo hai nami nikatibiwa hadi kupona na nikajifunguwa salama,"amesema.
Ameongeza"nilijifunguwa mtoto wa kiume mwenye uzito wa kilo tatu na siyo kilo nne na kwamba nilikaa naye baada ya muda nikawakabidhi mtoto waende kumtunza na mimi nililazwa na baadaye nikatoka na ninaendelea vizuri na mtoto ninakwenda kumuona."
Alipoulizwa kuhusu mkataba wa kumtunza mtoto hadi baada ya kufikia umri wa mika 18 ndipo atamchukuwa alikiri na kusema ni bora aendelee kukaa huko huko kwa sababu hali yake kiuchumi ni mbaya hata kufikia kudaiwa fedha za mkopo alizokopa katika shirika la mikopo la Eclof Mbeya baada ya kuuguwa na mdogo wake kuufilisi mradi wa mkaa aliomuachia.
"Nilikuwa na stoo ya Mkaa nikiuza kwa madebe na magunia lakini baada ya kuuguwa nilimkabidhi mdogo wangu aendeshe biashara hiyo lakini ilikufa,kwa hiyo nililazimika kuuza kila kitu changu na sasa ninaishi kwa rafiki yangu Nzovwe,hapa nimepata kibarua ninalipwa Sh.2,000 kwa siku sh.1400 pesa ya kula na Sh.600 pesa ya nauli ya dala dala,hali ni mbaya na ninashindwa kulipa deni,"amesema.
Hata hivyo Amina alisema hataki kusikia juu ya wanaume kwa sababu ni wauaji wanapokutaka kimapenzi wana ahadi lukuki lakini baada ya kujifunguwa wanakukana hali inayoweza kusababisha kujiuwa ama kufanya jambo lolote baya kwa hasira baada ya kuchanganyikiwa na anamshukuru Anna Kasile kwa kumnusuru yeye na mtoto wake.
Anna kasile akitoa mada inayozungumzia utetezi wa uhai alisema tangu ajiunge na mikakati hiyo ya kunusuru maisha ya watoto na Prolife amekuwa akikumbana na mikasa mingi ikiwemo kuhojiwa na watu wa ikulu kuwa anajishughulisha kuuza watoto anaowaokota jambo ambalo siyo la kweli.
Akizungumzia suala la Amina amesema baada ya kusikia anataka kutoa mimba kutokana na kutomjuwa mwanaume aliyempa uja uzito huo alilazimika kumsaiia na kuzungumza na wazungu akina Kaufmann waliokubali kumtunza na kumuuguza hadi akapona na kujifunguwa salama na kwamba mtoto yupo hai anaendelea kulelewa katika kituo chake hadi atakapofikia miaka 18 atamchukuwa.
Amesema walilazimika kufika kwa Mwanasheria Mwakolo kwa ajili ya kuwekeana mkataba wa kumtunza mtoto huyo ambapo amedai walilazimika kutoa sh.100,000 kama ada baada ya kuomba kupunguziwa kutoka Sh.150,000.
Wakili Mwakolo hakuweza kupatikana licha ya kumuomba miadi ya kuonana naye kupitia simu yake ya kiganjani baada ya kuomba ufafanuzi wa sheria iliyotumika katika makubaliano ya mkataba wa kutunza mimba sanjari na kufika ofisini kwake januari,29 na 30,2013 bila mafanikio ya kuonana naye.
Ofisa wa Idara ya ustawi wa jamii Mkoa wa Mbeya,Tobias Mwalwego akizungumza na KIONGOZI amethibitisha kupokea mkataba wa makubaliano kutoka kwa wasamaria wema waliolalamikia suala hilo na kwamba kwa kifupi hawakifahamu kituo hicho.
"Leo(januari,30) asubuhi tulikuwa tunajadili mkataba huo ni kitu cha kushangaza wala hakipo katika sheria na taratibu za kuasili mtoto,na ukiangalia kipengere cha nne cha masharti hayo(Kwamba baada ya mtoto kufikisha umri wa miaka 18 MAMA MZAZI ataruhusiwa kumchukuwa mtoto wake) hakiingii akilini kwa sababu atakosa haki za msingi za malezi na mapenzi ya mama,wakati Mama yake yupo,"amesema.
Aidha Ofisa huyo amesema hana uhakika kama kituo cha Care and Share-children's home kama kimesajiliwa kisheria kwa sababu katika idara ya ustawi wa jamii Mkoa wa Mbeya haikitambui wala shughuli zao licha ya mtu aliyefika ofisini kwake kujitambulisha kwa jina la Melvin Kauffman kama Ofisa utawala wa kituo hicho kilicho chini ya Shirika la Harmony International (januari,30,2013).
"Leo amekuja mgeni mmoja akiwa na familia yake akajitambulisha kuwa ni Melvin Kauffman kuwa ni Ofisa utawala wa kituo cha Care and Share kilichopo Simike na kwamba alikuwa anaomba idhini ya kumchukuwa mtoto mmoja yupo Hospitali ya Rufaa Mbeya kitengo cha uzazi Meta kwa ajili ya kumlea na kwamba anawatunza watoto kama hao watatu ambao wanaonekana wakubwa lakini huyo mtoto anayedaiwa kuchukuliwa baada ya mkataba hayupo katika orodha ya watoto aliowaonesha katika picha na maandishi,"amesema Mwalwego.
Amesema kuwa amemjibu Melvin kuwa kabla ya kumchukuwa huyo mtoto aliyekuwa Hospitali atalazimikia kufika katika kituo chake ikiwemo na kufuatilia suala la mkataba wa Amina Nganile na baadaye kujiridhisha kama kituo hicho kimesajiliwa kisheria na taratibu za kuwachukuwa na kuwatunza watoto hao kama zimefuatwa.
Kamanda wa polisi Mkoa wa Mbeya Diwani Athumani ameahidi kulifuatilia suala hilo na kujuwa ukweli na undani wake ili kama kuna tatizo liweze kushughulikiwa na endapo kuna makosa ya kisheria, sheria iweze kuchukuwa mkondo wake.
Mwisho.

Mama adaiwa kumuuza mtoto ni baada ya kuwekeana mkataba wa kutunza mimba na 'wazungu',yadaiwa baada ya kujifunguwa Hospitali ya Ifisi Mbeya wazungu watoweka naye hakumuona hata sura,aliambiwa alimzaa mtoto wa kiume wa kilo 4,akienda kituo cha kulelea watoto Simike adaiwa kuoneshwa watoto yatima waliokotwa


Na Thompson Mpanji,Mbeya
MWANAMKE mmoja  Mkazi wa Mtaa wa  Ikuti,Kata ya Iyunga, jijini Mbeya  amedaiwa  kumuuza  mtoto aliyemzaa mwenyewe kwa wazungu  wanaomiliki kituo kimoja cha watoto yatima   cha jijini hapa ambao hadi sasa haieleweki walipo  pamoja na kichanga chake  kiume kinachodaiwa kuzaliwa  kikiwa na uzito wa kilogramu nne.
Tukio hilo ambalo limewasikitisha wananchi walio wengine  linadaiwa kutokea mwanzoni mwa Novemba,2012 ambapo makubaliano yanadaiwa kufanyika mwezi,oktoba,2012  katika maeneo  ya Ikuti  mbele ya mashahidi  likiwepo  kampuni  moja la  mwanasheria  wa kujitegemea  la jijini Mbeya.
Mwenyekiti wa mtaa wa Ikuti,Kata ya Iyunga,Immanuel Mwasote amekiri kuwepo kwa tukio hilo  na kumtaja mwanamke huyo kuwa ni Amina Nganile ambaye alikuwa akiishi katika mtaa huo na alikuwa mjazito  na  wenzake kuthibitisha alijifungua salama  lakini baada ya siku mbili alionekana bila mtoto jambo lililowashtusha wengi na kumfikisha ofisini kwake kwa kesi mbili.
Mwasote amesema  Amina alifikishwa ofisini kwake  na wanakikundi  wenzake wa kikundi cha Tumaini kwa madai ya kushindwa kurejesha deni la mkopo katika shirika la Eclof sanjari na kumhoji  alikompeleka mtoto  ambapo alijibu yupo ustawi wa jamii akiendelea kulelewa .
“Kutokana na majibu hayo tuliingiwa wasiwasi na ndipo tukampeleka katika kituo cha polisi Iyunga kwa mahojiano na baadaye walimwachilia,kwa hiyo  tuliwaachia polisi waendelee na uchunguzi na baadaye amehama mtaa wangu sijuwi alipokwenda,”amesema.
Akizungumza na Mwandishi wa  gazeti hili Msimamizi wa kikundi Tumaini ,Winfrida Nzunda  amesema  mwenzao huyo  alipokuwa mjamzito   walikuwa wakija wazungu na gari ambalo nambari zake hawakuzishika na kumchukuwa kumpeleka kuhudhuria  kliniki katika Hospitali ya Ifisi na kumrudisha hadi alipojifungua  na kulazwa  siku moja na kutoka bila mtoto.
Winfrida amesema  baada ya kumhoji  alielezea kuwa   baada ya kujifungua  hakuiona sura ya mtoto wake  baada ya kuchukuliwa na wazungu  hao ambao walikuwa wanawake wawili na wanaume watatu zaidi ya kumfahamisha kuwa  amejifungua mtoto wa kiume mwenye uzito wa kilo nne  na kwamba hadi leo haelewi  alipo mtoto wake  na wazungu hajawaona tena.
“Lakini baada ya kumbana sana alituambia kuwa Mama yake huyo aliyemtaja kwa jina la Mama Kasile  anayesimamia kituo cha kulelea watoto cha  For Care & Share-Children’s  Home kilichopo Simike jijini Mbeya  ndiye aliyemshawishi  kuwekeana mkataba na wazungu hao kumhudumia  hadi atakapojifunguwa  baada ya kutomjuwa mwanaume aliyempa mimba  na ndipo watamchukuwa mtoto kumlea hadi baada ya miaka 18  watamrejesha kwake,”amesema.
Msimamizi huyo wa kikundi amesema kuwa  baada ya kumbana zaidi aliwaeleza kuwa  mkataba wa kumhudumia ulimalizika  baada ya kujifungua na hivyo  wazungu hao  walimchukuwa mtoto huyo  na kwamba alipotoka Hospitali alikwenda kwa Mama Kasile ambako alihudumiwa kwa siku nne na baadaye kufukuzwa  kwa madai akajitegemee.
Amesema mwanamke huyo amethibitisha kuwa amedhurumiwa fedha na Mama  huyo kwani ana imani amepewa fedha nyingi  na kwamba katika hatua ya kushangaza  akifika kumwangalia mtoto anaoneshwa wale waliokotwa na kupewa muda wa dakika mbili  aondoke jambo ambalo linathibitisha kuwa mtoto wake ameshatoroshwa kwenda mashariki ya mbali.
Hata hivyo Winfrida amesema kuwa baada ya tukio hilo mwanamke huyo  amehama hapo mtaa wa Ikuti na haileweki anapoishi maeneo ya Nzovwe  na wanaendelea kumsaka  kutokana na kushindwa kurejesha deni la zaidi ya Sh.370,000 katika shirika la mikopo la Eclof  na hivyo wanahofia kufikishwa mahakamni kutokana na deni  la mwenzao huyo.
Meneja wa shirika la mikopo midogo  la Eclof tawi la Mbeya,Magdalena  Lekaaya amethibitisha kukopeshwa  Amina Nganile mkopo wa Sh.400,000 na kutakiwa kurejesha Sh.79,000 kila mwisho wa mwenzi pamoja na wanakikundi wenzake  lakini  baadaye hakuonekana hadi  wanakikundi walipomkamata.
Amesema baada ya kumhoji  na kumtania kwanini ameshindwa kurejesha mkopo ilhali ameshamuuza mtoto  alikiri na kudai hajapewa hata senti moja  na kwamba hana uwezo wa kulipa deni  wamfikishe kokote  na hivyo kumuona  kama amechanganyikiwa na kumwagiza aende kutafuta  hela hiyo chini ya udhamini wa wanakikundi wenzake lakini hajaonekana.
Baadhi ya ndugu,jamaa na marafiki wa Amina kutoka katika kijiji cha Isongole Umalila,wilaya ya Mbeya vijijini  wakizungumza  na gazeti hili wamesikitishwa na kulaani vikali tukio hilo na kjuiomba serikali  iweze kuchukuwa mkondo wake.
Gazeti hili linayo nakala ya mkataba wa makubaliano ya kumuuza mtoto huyo  baada ya ‘wazungu’ hao kutunza mimba  ya mwanamke huyo aliyetajwa kwa jina la Amina Paulo Nganile  na mtoto atayezaliwa  hadi afikie umri wa miaka 18.
Nakala ya mkataba huo una masharti sita yaliyoainishwa  katika kutimiza makubaliano  yaliyofanywa Oktoba,5,2012 kati ya kituo cha kulea watoto maarufu “Watunzaji’ Care & Share-Children’s home wa S.L.P. 573,Mbeya-Tanzania,East Afrika Phone No.0252502749 na Amina Paulo Nganile anayeishi karibu na Itende JKT,eneo la Nzovwe,Mbeya ambaye kwa upande mwingine anaitwa MAMA MZAZI.
Sehemu ya makubaliano hayo yameandikwa kama ifuatavyo:” kwamba watunzaji ni wenye kumiliki kituo cha kulelea watoto wadogo chini ya umri wa miaka 18,kwamba kwa hiari yao watunzaji  na kwa hiari ya MAMA MZAZI ambaye ni mjamzito wamekubaliana  kuwa MAMA MZAZI atatunzwa  na kituo hicho yeye mwenyewe na kusaidia gharama za kujifungua mtoto.
“Kwamba baada ya mtoto kuzaliwa ‘watunzaji’ wataendelea kumtunza  mtoto atakayezaliwa mpaka atakapofikia umri wa miaka 18,kwamba baada ya mtoto kufikisha umri wa miaka 18 ‘mama mzazi ‘ataruhusiwa kumchukuwa mtoto  wake,kwamba matunzo kwa mama mzazi yatakoma mara baada ya kujifungua.”
Sharti la sita limesema,” kwamba MAMA MZAZI hamjuwi aliyempa mimba na hivyo hana uwezo wa kutunza mimba na mtoto atayezaliwa  hivyo anakubali kuwa mtoto atayezaliwa atunzwe  na ‘watunzaji ‘hadi atakapofikia umri wa miaka 18.”
Aidha sehemu ya mkataba huo imesema makubaliano hayo yametiwa sahihi na wahusika wote  mbele ya mwanasheria ambaye ni  Melvin Kauffman wa For care & share-children’s home na ‘Mama Mzazi’ Amina Paulo Nganile na shahidi aliyeandikwa kwa jina la Anna Kasile mwenye nambari ya simu 0754 615021 mbele ya Wakili kutoka kampuni ya Mwakolo and Co.Advocates,P.O.BOX 2908,Mbeya-0754052231 ikiwa imewekwa na mhuri wa kampuni hiyo ya mwanasheria wa kujitegemea.
Jitihada za kumtafuta ‘mama mzazi’ ambaye ni mama wa  kichanga cha kiume   kilichozaliwa na uzito wa kilo nne  zinaendelea ili kupata ukweli  wa tukio hili ambapo anayedaiwa mama mkubwa aliyemshawishi  kumuuza mtoto huyo  alipopigiwa simu  na kuhojiwa kuhusiana na tukio hilo alijibu kwa jazba kuwa hasipotezewe muda
Anna Kasile ambaye anadaiwa kuwa ni mama mkubwa,msimamizi wa kituo aliyekuwa  muda wote na 'wazungu' hao alimwambia mwandishi wa habari hizi kuwa  amuulize vizuri Amina sababu ya yote hayo na ikiwezekana amtafute aende naye kituoni hapo.
Kasile amesema  amehojiwa na watu wengi  ikiwemo waandishi wa habari na polisi kwa hiyo amechoka kujieleza, hawezi kupoteza muda kwa ajili ya masuala ya kipuuzia na hatimaye alikata simu na alipopigiwa zaidi ya mara nne alikata simu licha ya kutumiwa ujumbe mfupi wa maandishi kufafanua tuhuma dhidi yake kuwa amekuwa na kawaida ya kuwauza watoto anaowaokota wametupwa na kuwalea hakujibu.
Jitihada  za  kuwasiliana na Kamanda wa Polisi mkoa wa Mbeya,Diwani Athumani,a Kampuni ya Wakili Mwakolo(Mwakolo and Co. Advocates)  na Ofisi ya ustawi wa jamii  Mkoa wa Mbeya kujuwa  utaratibu wa kuasili watoto na mkataba wa makubaliano  zinaendelea.
 Mwisho.

Taarifa ya Polisi Mbeya,mchungaji mbaroni kwa uchochezi



TAARIFA YA JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA KWA VYOMBO VYA HABARI
“PRESS RELEASE” TAREHE 31. 01.2013.

WILAYA YA MBEYA MJINI   – MUINJILISTI AHOJIWA POLISI KWA UCHOCHEZI.

MUINJILISTI NICHOLAUS S/O LUWONEKO @ KAMWAGILA,UMRI MIAKA 35,MHEHE,MKAZI WA MTONI MTONGANI – DAR ES SALAAM ALIKAMATWA NA MAKACHERO JANA JIONI TAREHE 30.01.2013 HUKO ENEO LA IYUNGA NJE YA KANISA LA MORAVIAN USHIRIKA WA IYUNGA JIJINI MBEYA KWA TUHUMA ZA KUHUBIRI KANISANI HAPO AKITUMIA MANENO YA KICHOCHEZI DHIDI YA DINI NYINGINE.UCHOCHEZI HUO HAUKUWAFURAHISHA BAADHI YA WAUMINI NDIPO WAKATOA TAARIFA. AMEKAMATWA AKIWA PIA NA CD’S NA VIPEPERUSHI AMBAVYO NI SEHEMU YA UCHUNGUZI UNAOENDELEA. KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHNA MSAIDIZI WA POLISI DIWANI ATHUMANI ANATOA WITO KWA WANA MBEYA /WANANCHI WOTE KUWACHUKIA /KUTOWAKUMBATIA WACHOCHEZI WA MADHEHEBU /DINI YOYOTE ILI KUJIEPUSHA NA MADHARA AMBAYO YAMEKUWA YAKIONEKANA KATIKA BAADHI YA MAENEO NCHINI NA DUNIANI. AIDHA ANATOA PONGEZI KWA WOTE WANAOENDELEA KUTHAMINI AMANI,USALAMA NA UTULIVU HUSUSANI WAUMINI WALIOTOA TAARIFA HII NA KUFANIKISHA KUKAMATWA MUINJILISTI HUYU.JESHI LA POLISI MKOANI  WA MBEYA HALITAVUMILIA KAMWE UCHOCHEZI WA NAMNA YOYOTE MKOANI HAPA.

WILAYA YA MBEYA MJINI - KUPATIKANA NA BHANGI

MNAMO TAREHE 30.01.2013 MAJIRA YA SAA 21:30HRS HUKO UYOLE JIJI NA MKOA WA MBEYA. ASKARI POLISI WAKIWA DORIA WALIMKAMATA TITO S/O SAMSON,MIAKA 21,MKINGA,BIASHARA MKAZI WA UYOLE AKIWA NA BHANGI KETE 42 SAWA NA GRAM 220 KATIKA KIBANDA CHAKE CHA BIASHARA YA KUUZA JUICE NA MAJI .MTUHUMIWA NI  MVUTAJI NA MUUZAJI  WA BHANGI NA TARATIBU ZA KISHERIA ZINAFANYWA ILI MTUHUMIWA AFIKISHWE MAHAKAMANI. KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHNA MSAIDIZI WA POLISI DIWANI ATHUMANI ANATOA WITO KWA JAMII KUACHA KUTUMIA DAWA ZA KULEVYA  KWANI NI KINYUME CHA SHERIA NA NI HATARI KWA AFYA YA MTUMIAJI.

WILAYA YA RUNGWE- KUPATIKANA NA BHANGI

MNAMO TAREHE 30.01.2013 MAJIRA YA SAA 21:30HRS HUKO ENEO LA MWISHOLWA- TUKUYU WILAYA YA RUNGWE MKOA WA MBEYA. ASKARI POLISI WAKIWA DORIA WALIWAKAMATA 1.FRANK S/O BENARD, MIAKA 25, KYUSA, MKULIMA MKAZI WA BUJINGA 2.AMBONISYE S/O MLONGOTI, MIAKA 25, KYUSA, MKULIMA MKAZI WA BUJINGA NA 3. EDWARD S/O EDWINE ,MIAKA 30,KYUSA MKULIMA, MKAZI WA MTAA WA BAGAMOYO WAKIWA NA BHANGI MISOKOTO MITATU  SAWA NA GRAM 15 . WATUHUMIWA NI WAVUTAJI WA BHANGI. WATUHUMIWA NI WAVUTAJI WA BHANGI NA TARATIBU ZA KISHERIA ZINAFANYWA ILI WATUHUMIWA WAFIKISHWE MAHAKAMANI. KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA KAMISHNA MSAIDIZI WA POLISI DIWANI ATHUMANI ANATOA WITO KWA JAMII KUACHA KUTUMIA DAWA ZA KULEVYA  KWANI NI KINYUME CHA SHERIA NA NI HATARI KWA AFYA YA MTUMIAJI.


Signed By,
[DIWANI ATHUMANI – ACP]
KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA.

Monday, January 28, 2013

Maoni ya Wasomi kutoka Roma kuhusu Katiba Mpya ya Tanzania

Maskani > Haki na Amani >  2013-01-26 07:42:11
A+ A- Chapisha ukurasa huu Tuma kwa e-mail






Mchakato wa kukusanya maoni ya Katiba Mpya ya Tanzania unaendelea vyema, awamu ya kwanza ilikuwa ni kuhamasisha na kukusanya maoni kutoka kwa watanzania mmoja mmoja. Hatua ya pili imekuwa ni kukusanya maoni kwa makundi maalum. Yafuatayo ni baadhi ya maoni yaliyotolewa na wanafunzi wanaosoma mjini Roma, kama sehemu ya mchango wao katika kuandika Katiba Mpya ya Tanzania.
1. Kuhusu Mahakama ya Kadhi:
Mahakama hii ni ya kidini na inahusiana na utatuzi wa maswala ya kidini. Hivyo basi, kutokana na kwamba Tanzania yetu tangu kupata uhuru wake inajukana kama nchi isiyo fuata misingi ya dini yoyote, swala la Mahakama ya Kadhi isiingie kwenye katiba; mahakama iendelee kubaki kama mmojawapo wa mihimili mikuu ya nchi inayo ratibu maswala ya dini husika, bila kuihusisha Katiba ya nchi ambayo ni ya wananchi wote wafuasi wa dini fulani na wasio fuata dini yoyote. Mahakama za kidini zisiingie katika katiba kwani Tanzania haina dini.
2. Kuhusu Tanzania kujiunga na OIC
Jumuiya ya Nchi za Kiislam OIC ina malengo na itikadi zake zinazojikita hasa katika masuala ya kidini. Tanzania hadi sasa haina dini yoyote rasmi ila ni wananchi wake wanao abudu kwenye dini na madhehebu mbalimbali. Ikiwa kuna wananchi wanaotaka kujiunga na Jumuiya hii wapewe nafasi kama watu binafsi na si kama nchi. Tanzania isijiunge na OIC kwa kuwa hii ni Jumuiya ya Kidini. Suala la Tanzania kuwa na uhusiano wa kidiplomasia na Vatican halina uhusiano wowote na madai ya baadhi ya watu kutaka Tanzania kujiunga na OIC.
3. Kuhusu mfumo wa Elimu
Kwakuwa Serikali inalo jukumu la kuhakikishia wananchi wake Elimu, mfumo wa Elimu usiwe wa kidini badala yake uendelee kusimamiwa na serikali itakayokuwa madarakani.Mchango wa dini mbalimbali katika sekta hii uendelee kuheshimiwa na kuthaminiwa, ila serikali iliyoko madarakani ndiyo itoe taratibu na sheria (zisizoshikamana na dini yoyote) zinazopaswa kufuatwa katika swala zima la utoaji Elimu.
4. Kuhusu uteuzi wa viongozi wa serikali na wa mashirika ya kiserikali
Uteuzi wa viongozi hawa uzingatie sifa za anayeteuliwa na wala usifanyike kulingana na sera za kiundugu au kidini. Si kwa sababu mteuliwa ni rafiki au ndugu wa Kiongozi fulani au ni muumini wa dini fulani, basi anafaa kushika madaraka. Nyadhifa zitolewe kwa kuzingatia “Mastahili, sifa na vigezo vinavyohitajika.
5. Kuhusu uchaguzi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano.
Hadi sasa watanzania tunajua kuwa bara na visiwani ni Taifa moja na kwamba hatuna tofauti yoyote kama raia. Hivyo basi, kwakuwa Zanzibar na Tanzania bara ni nchi moja, Raisi wa Jamhuri ya Muungano atoke upande wowote ule wa Muungano na kusiwepo utaratibu wa kupata Rais kwa zamu kati ya Tanzania bara na Zanzibar. Utaratibu wa kupata Rais kwa zamu kati ya pande hizo mbili unaweza ukawa hatari na kutishia zaidi usalama na amani ya Taifa kwani inawezekana kutokea kwamba kusitokee aidha mgombea nafasi hiyo mahali ambapo Rais alitakiwa kutokwa kadiri ya mfuno uliopo hadi sasa.
Nafafanua: ikiwa kwa mfano kwenye uchaguzi ujao Rais anapaswa kutokea Zanzibar au bara, na ikatokea kwamba kwenye ukanda huo hakuna mgombea aliyejitokeza, au aliyejitokeza asipigiwe kura, nini kitafanyika? Kumbe kipengele kinachosititza kuwa Rais achaguliwe kwa kuzingatia bara na visiwani kingeweza kuangaliwa upya na kufanyiwa marekebisho ili Rais achaguliwe kutoka eneo lolote la Tanzania.
6. Kuhusu utoaji mimba
Utoaji mimba ni swala linalohusu haki msingi za binadamu zinazoongozwa na dhamiri nyofu. Hakuna serikali yoyote inayoweza kuingilia dhamira ya mwananchi. Kama vile ambavyo serikali haiwezi kumchagulia mwananchi yeyote mwenza wa maisha, au kuwaamuru wananchi kuvaa mavazi yaliyoshonwa kwa mtindo fulani au ya rangi fulani, hali kadhalika, serikali haipaswi kujiingiza kwenye maswala ya kuratibu na kuhalalisha kisheria maswala yanayohusu dhamira na hasa mauaji ya watu wasio kuwa na hatia!
Jukumu la serikali ni kulinda maisha na usalama wa raia wake wote na si kuratibu mauaji ya baadhi ya raia ambao bado hawajazaliwa. Licha ya hilo, mila na desturi za kiafrika si mila za mauaji bali ni mila zinazotetea uhai na kuulinda. Utoaji mimba ni utamaduni wa kifo usiopaswa kukumbatiwa na mwanadamu yeyote na hasa chombo kinacho ratibu maisha ya wananchi kama ilivyo Katiba ya nchi. Katiba ilinde haki za watoto ambao bado hawajazaliwa.
7. Kuhusu ndoa za watu wa jinsia moja
Serikali isitambue ndoa ya watu wa jinsia moja na kuiweka katika Katiba ya nchi, kwa kuwa ni jambo linalo kwenda kinyume na maadili ya kiutu na kijamii. Hivyo swala hili lisipate nafasi katika Katiba ya nchi. Kama ilivyo hoja iliyopita, hata hii inayofuata inahusu dhamira ya mtu binafsi. Kama baadhi ya wananchi wakiamua kuishi muunganiko (kwani haiwezi kuitwa ndoa) wa watu wa jinsia moja, liwe ni chaguo lao binafsi, ila lisitambulike kikatiba! Katiba ya nchi izingatie maadili na utu wema.
8. Uraia wa nchi mbili:
Kuna haja kwa Katiba ya Tanzania kusoma alama za nyakati kwa kuruhusu raia wake kuwa na fursa ya uraia wa nchi mbili pale inapowezekana ili kuweza kufaidi matunda ya jasho la watanzania wanaoishi ughaibuni.

Friday, January 25, 2013

Waachieni Mapadre mliowateka, ili wamtumikie Mungu na Jirani zao!




Baraza la Maaskofu Katoliki DRC limerudia tena ujumbe wake, kwa kuwaomba watu ambao waliwateka nyara Mapadre watatu wa Shirika la Assumption, Mwezi Oktoba 2012 kuwaachia mara moja, ili waweze kuendeleza huduma kwa waamini wao kiroho na kimwili.

Maaskofu wanasema, Mapadre hawa waliotekwa hawana sababu ya kuendelea kuteseka katika mazingira hayo. Ni nafasi kwa wateka nyara kutubu na kuongoka, kwa kuwaachia ili waendelee kutekeleza wajibu wao. Mapadre waliotekwa tangu mwezi Oktoba, 2012 ni Jean Pierre Ndulani, Anselme Wasikundi pamoja na Padre Edmond Bamutate.

Mapadri hawa walitekwa nyara hapo tarehe 19 Oktoba 2012 walipokuwa kwenye Parokia ya Notre Dame des Pauvres iliyoko Mbau, Jimbo Katoliki la Butembo, DRC. Tangu wakati huo, hakuna taarifa juu ya Mapadre hawa.







Uwasilishaji wa Ujumbe wa Papa kwa ajili ya adhimisho la 47 la Siku y Mawasiliano Jamii.




Askofu Mkuu Claudio Maria Celli, amewasilisha Ujumbe wa Papa kwa ajili ya adhimisho la 47 la Siku ya Mawasiliano Duniani, itakayo adhimishwa tarehe 12 May 2013. Ujumbe wa Papa,unaongozwa na Kauli mbiu: Mifumo ya mawasiliano jamii Nafasi Mpya za Uinjilishaji.
Hotuba ya Askofu Mkuu Claudio Maria Celli, kwa ajili ya uwasilishaji huo, imepembua yaliyomo katika ujumbe wa Papa , ikiangalia pia , matokeo ya takwimu za tafiti zilizofanyika katika nchi za 21 za bara tano.
Askofu Mkuu Celli ametaja kati ya yaliyoainishwa katika takwimu hizo ni pamoja na madhara hasi ya matumizi ya mitandao ya habari katika maendeleo ya watu, kama ilivyoelezwa na Mwandishi mmoja wa vitabu wa Marekani, jinsi mfumo huu mpya wa internent unavyoweza kufanya mazuri mengi kwa kasi ,lakini wakati huohuo, pia unaonekana kupumbaza akili za watu , au kuwafanya kuwa wavivu wa kufikiri kwa kina. Na hivyo anaonyesha kushakia iwapo mtandao huo, hauna mwelekeo wa kupumbaza na kubadilisha akili za watu.
Kwa muktadha huu, Askofu Mkuu ameuangalia ujumbe huo wa Papa , akisema, ujumbe unaonyesha pia tathimini chanya za kijamii kwa vyombo vya habari, kwamba yote si mabaya, lakinii pia ni fursa kwa ajili ya mazungumzo na majadiliano, hasa katika utambuzi wa uwezo wake, katika kuimarisha mahusiano ya pamoja au miongoni mwa watu kwa ajili ya kukuza ufanisi wa maelewano ya familia ya binadamu.
Hata hivyo, kwa ajili ya kufanikisha hili, Ujumbe umeasa, ni muhimu kuheshimu faragha za watu na kuwajibika katika kutoa habari za kweli na uhalisi wa kushirikisha, si tu taarifa na tambuzi, lakini kama sehemu ya kiini cha mawasiliano kati ya watu.
Na pia umegusia mabadiliko ya mienendo ya kijamii katika vyombo vya habari, ukisisitiza umuhimu wa kuingizwa katika jitihada na hasa zaidi katika kuzingatia moyo wa ubinadamu, kwenye vipindi vya mwingiliano wa maswali na majibu,kwa ajili ya kutoa maana ya uwepo wa binadamu.

Kwa mtazamo huo, Askofu Mkuu Celli, ameutaja ujumbe wa Papa kwamba, unagusa maeneo mengi muhimu katika maisha ya kijamii, na hivyo kama ilivyosema kauli mbiu ya ujumbe huo, inakuwa ni nafasi nzuri ya uinjilishaji mpya , kazi ya kulitangaza Neno, Kama Yesu Kristu Mwenyewe alivyoagiza.



Jiji la Roma limeamua kumuenzi Mwenyeheri Yohane Paulo II




Eneo linaloangaliana na Lango kuu la Makao Makuu ya Jimbo kuu la Roma, kwenye Kanisa kuu la Mtakatifu Yohane wa Laterano, litapewa jina la Mwenyeheri Yohane Paulo wa Pili, kama kielelezo cha heshima ya kutambua mchango wa Baba Mtakatifu Yohane Paulo wa Pili, aliyeliongoza Kanisa Katoliki kuanzia mwaka 1978 hadi mwaka 2005.

Kanisa likatambua utakatifu na mchango wake katika maisha na utume wa Kanisa; hapo tarehe Mosi Mei, 2011 akatangazwa kuwa Mwenyeheri na Baba Mtakatifu Benedikto wa kumi na sita. Uongozi wa Jiji la Roma unabainisha kwamba, Yohane Paulo wa Pili amekuwa ni Kiongozi mkuu wa Kanisa, lakini zaidi ya yote, alikuwa ni mtu mwenye imani thabiti, ambaye kwa njia ya imani hiyo ameweza kubadili uso wa dunia katika karne ya ishirini. Ndiyo maana Jiji la Roma linapenda kumuenzi Yohane Paulo wa Pili ambaye amejidhihirisha kuwa ni Baba wa wote.

Baada ya taratibu kukamilika, eneo hili ambalo liko mbele ya Lango kuu la kuingilia kwenye Makao Makuu ya Jimbo kuu la Roma, sehemu ya Uwanja wa Kanisa kuu la Mtakatifu Yohane wa Laterano utajulikana kama "Largo Giovanni Paolo II- Karol Josef Wojtyla - Pontefice 1978 - 2005".

Katiba ya Tanzania: madaraka ya Rais, Tume huru ya Uchaguzi, Udini, Muungano, Haki ya kuishi na Umiliki wa Ardhi




Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania katika mchakato wa mabadiliko ya Katiba ya Tanzania mintarafu mwongozo wa uhamasishaji, leo katika makala haya wanazungumzia kuhusu madaraka ya rais, tume huru ya uchaguzi, dhana ya kuwa na Serikali isiyokuwa na dini, muungano na umiliki wa ardhi. RealAudioMP3
Madaraka ya Rais
Madaraka ya uteuzi wa viongozi wa juu yana wigo mpana mno unaoingilia mihimili mingine ya dola - jaji mkuu na majaji na wabunge wa kuteuliwa. Vile vile huteua mkuu wa Jeshi la polisi, wakuu wa mikoa na wilaya nk. Pia ana mamlaka ya kusamehe wafungwa, kuvunja bunge na baraza la mawaziri nk. Madaraka haya yanaweza kutumiwa vibaya, na pia uwajibikaji kwa wateuliwa hao kwa wananchi unakuwa mdogo. Madaraka haya yapunguzwe na/ama yadhibitiwe. Vigezo viwe wazi na uamuzi ufikiwe kwa njia shirikishi.
Tume huru ya uchaguzi na Tume nyinginezo
Kwa sababu inaundwa kwa njia ya uteuzi bila vigezo kuwekwa wazi, wananchi wengi wamekosa imani nayo, na malalamiko yamekuwa mengi. Uundwaji wa Tume zetu ufanyike kwa uwazi na iliyo shirikishi.
Dhana ya kuwa Serikali haina dini (Secularity of the State)
Msingi huu ndio nguzo ya umoja na amani katika nchi yetu. Ifafanuliwe na kusimamiwa kikatiba ikiwa ni pamoja na kuweka mipaka katika uhuru wa kuabudu kwa kuwa tumeshaona unatumika vibaya kama vile kuleta mgawanyiko na mtikisiko katika familia, kufanya mihadhara ya kukashifu dini nyingine, kuharibu mali za wengine na kusababisha uvunjifu wa amani. Vile vile msukumo wa kuanzisha mahakama ya kadhi ndani ya mfumo wa mahakama za nchi siyo haki kwa hiyo isiwemo katika Katiba kwa kuwa ni mambo ya kidini na huenda ni njia ya kuifikisha nchi yetu katika kukiuka dhana ya kuwa serikali yetu haina dini.
Muungano
Kwa mujibu wa Katiba ya sasa ya Zanzibar, Katiba ya Muungano imevunjwa, wakati huo huo msukumo wa watu kutaka Muungano uangaliwe upya una hoja zenye nguvu. Tutoe maoni yetu tukizingatia sababu za waasisi wa muungano, na pia faida na hasara za muungano kwa wakati huu. Mapendekezo ya kutambua Tanganyika kama nchi yametambuliwa na Katiba ya sasa ya Zanzibar, kwa hiyo wazo la kuwa na Muungano wenye Serikali tatu ni hoja ambayo tunaweza kutolea maoni yetu.
Haki ya kuishi
Kwetu sisi Wakatoliki ni jambo la kupigania kwa nguvu zote Katiba iweze kulinda uhai tangu kutungwa mimba. Vile vile tunaweza kutoa maoni yetu juu ya adhabu ya kifo. Hapa tuna wajibu wa pekee kabisa kutoka imani yetu inayotufundisha kwamba mwenye mamlaka ya kutoa uhai na kuutwaa ni Mungu Mwenyewe.
Umiliki ardhi
Haki ya watu wa Tanzania Visiwani kumiliki ardhi ya Bara ifutwe kama ilivyo kwa watu kutoka Tanzania Bara kutoweza kumiliki ardhi huko Visiwani.

Saturday, January 19, 2013

KIKAO CHA DHARULA MBEYA PRESS CLUB KINATEGEMEA MAAMUZI YA "MEMBERS POWER"

Nawasalimu wapendwa wote katika jukwaa hili,Tunaingia ndani ya nyumba katika ghorofa hili la Mbeya Peak Hotel kujadili  afya ya klabu yetu,tunaingia tukiwa na shahuku kubwa ya kuendelea kuiweka Mbeya Press Club yetu katika mstari ule ule wa klabu kongwe,strong yenye mwelekeo mzuri wa kuigwa,kitakachojiri humu ndani kuhusu maamuzi ya "MEMBERS POWER,"baada ya takribani masaa kama sita kutokana na unyeti wa ajenda zenyewe tutawajuza,mwenyezi mungu atujalie hekima,busara,uvumilivu na kuwa na moyo wa subira katika yote,Amina!.

Thompson Mpanji.

Friday, January 18, 2013

Wakatoliki na Kanuni msingi katika utoaji wa maoni juu ya mchakato wa kuandika Katiba Mpya ya Tanzania

Kanuni msingi katika utoaji wa maoni juu ya mchakato wa kuandika Katiba Mpya ya Tanzania



Katika utoaji wa maoni ya Katiba Mpya ya Tanzania, Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania katika mwongozo wake kuhusu mchakato huu, linawahamasisha waamini na watanzania wote kuhakikisha kwamba, wanadumisha: umoja na mshikamano wa kitaifa; maelewano na utlivu; amani na udugu. RealAudioMP3

Waamini wa Kanisa Katoliki waendelee kuchangia maoni yao wakizingatia kwa namna ya pekee: utu na heshima ya kila mtu aliyeumbwa kwa sura na mfano wa Mungu; upendo, mafao ya wengi, haki msingi za binadamu, ustawi na maendeleo ya wengi nchini Tanzania.

Watanzania wanahitaji Katiba itakayojibu kero sugu na changamoto ambazo zimekuwa ni kikwazo cha maendeleo ya wengi; ijielekeze katika kudumisha haki na amani. Katiba mpya iwe ni ile Katiba inayotekelezeka na kuwajibisha. ibainishe sheria na kanuni za kupambana na saratani ya rushwa ambayo imejikita katika mihimili ya dola ambayo ni Serikali, Mahakama na Bunge.

Tuesday, January 15, 2013

Askofu Desiderius Rwoma ateuliwa kuwa Askofu Mpya wa Jimbo Katoliki Bukoba, Jimbo la Singida sasa liko wazi!

Askofu Desiderius Rwoma ateuliwa kuwa Askofu Mpya wa Jimbo Katoliki Bukoba, Jimbo la Singida sasa liko wazi!



Baba Mtakatifu Benedikto wa kumi na sita, amekubali ombi la Askofu Nestori Timanywa wa Jimbo Katoliki Bukoba, kung'atuka kutoka madarakani na badala yake amemchagua Askofu Desiderius M. Rwoma wa Jimbo Katoliki Singida, kuwa Askofu mpya wa Jimbo Katoliki la Bukoba, Tanzania.

Kwa sasa Jimbo Katoliki Singida, liko wazi. Wakati huo huo, Baba Mtakatifu Benedikto wa kumi na sita, amemteua Askofu Desiderius Rwoma kuwa Msimamizi wa Kitume wa Jimbo Katoliki Singida.

Askofu Rwoma, alizaliwa kunako tarehe 8 Mei 1947, Jimboni Bukoba. Baada ya masomo na majiundo yake ya Kikasisi akapadrishwa kunako tarehe 28 Julai 1974. Kwa miaka mingi alikuwa ni Gombera wa Seminari Ndogo ya Rubya na Makamu Askofu jimbo Katoliki Bukoba.

Tarehe 19 Aprili 1999 aliteuliwa na Baba Mtakatifu Yohane Paulo wa Pili kuwa Askofu wa Jimbo Katoliki Singida, kufuatia kifo cha Askofu Bernard Mabula. Akawekwa wakfu na Kardinali Polycarp Pengo, Askofu mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam hapo tarehe 11 Julai 1999, Kwenye Kanisa kuu la Moyo Mtakatifu wa Yesu, Jimbo Katoliki Singida.

Wanasiasa msitatute umaarufu kwa rasilimali ya Tanzania kwani ni mali ya watanzania wote!

Wanasiasa msitatute umaarufu kwa rasilimali ya Tanzania kwani ni mali ya watanzania wote!



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Mrisho Kikwete amekemea tabia ya baadhi ya viongozi wa kisiasa kutumia suala la raslimali za taifa, ikiwamo gesi asilia kujifatufia umaarufu wa kisiasa na kuwapotosha wananchi. Aidha, Rais Kikwete amesema kuwa ni jambo la hatari na lisilo na tija kwa wanasiasa kujaribu kuigawa nchi vipande vipande kwa sababu ya kujitafutia umaarufu kwa kutumia raslimali za taifa.

Rais Kikwete ameyasema hayo, Januari 15, 2013 wakati alipokutana na Balozi wa Uingereza nchini ambaye anamaliza muda wake, Mheshimiwa Dianne Corner ambaye alifika Ikulu, Dar Es Salaam kumuaga baada ya kumaliza muda wake wa uwakilishi katika Tanzania. Rais Kikwete na Balozi Corner wamezungumzia masuala mbali yanayohusu uhusiano kati ya Tanzania na Uingereza, masuala ya ukanda wa Afrika Mashariki na masuala ya kimataifa.

Kuhusu ugunduzi wa gesi asilia uliofanywa na Kampuni BG ya Uingereza katika eneo la Msimbati kwenye Bahari ya Hindi, walikubaliana kuwa hilo ni jambo jema na lenye kuleta matumaini kwa Tanzania hasa wakati itakapoanza kuvunwa katika miaka michache ijayo. Kuhusu siasa zilizoanza kujitokeza kufuatia ugunduzi huo mkubwa wa gesi asilia, Rais Kikwete amesema kuwa ni tabia ya hatari kwa wanasiasa kutumia gesi asilia hiyo ama raslimali nyingine kujijengea umaarufu wao ambao umeporomoka.

“Unawezaje kuwa na nchi moja na taifa moja wakati kila mmoja anadai raslimali kutoka kwenye eneo moja ibakie na kunufaisha watu wa eneo hilo tu. Huwezi kuwa na nchi moja na yenye umoja wakati kuna nchi ya gesi asilia kule Mtwara, kuna nchi ya kahawa kule Kilimanjaro, kuna nchi ya chai na ndizi kule Bukoba,” amesema Rais Kikwete na kuongeza: “Kwa sababu kama gesi asilia inatakiwa kubakia na kunufaisha watu wa Mtwara tu, basi wenye haki zaidi ya kudai jambo hili siyo watu wa Mtwara bali ni watu wa Msimbati ambako ndiko ilipogunduliwa kesi ambako ni maili 60 kutoka Mtwara, kilomita 200 kutoka Newala.”

Ameongeza: “Unajua nchi yetu inao baadhi ya wanasiasa wenye uchu wa umaarufu na ambao wanatumia jambo hili jema kwa manufaa yao binafsi bila kujali umoja na jadi ya taifa letu la raslimali zetu kutumika kuiendeleza nchi nzima.” Kuhusu uhusiano kati ya Tanzania na Uingereza, Rais Kikwete amemshukuru Balozi Corner kwa kazi nzuri ya kuimarisha uhusiano huo. “Umeufikisha uhusiano wetu kwenye hatua ya juu kabisa na tunakushukuru kwa jambo hili.” Mheshimiwa Corner ambaye amekuwa Balozi wa Uingereza nchini Tanzania kwa miaka minne amehamishiwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC).

Katiba Mpya ya Tanzania izingatie: haki msingi za binadamu, uhuru wa kuabudu na uhai wa binadamu dhidi ya utamaduni wa kifo!

Katiba Mpya ya Tanzania izingatie: haki msingi za binadamu, uhuru wa kuabudu na uhai wa binadamu dhidi ya utamaduni wa kifo!



Askofu Michael Msonganzila wa Jimbo Katoliki Musoma, Tanzania anasema kwamba, kwa miaka kadhaa, watanzania wameonesha hitaji la kuwa na Katiba Mpya, itakayokidhi mahitaji ya watanzania kwa sasa. Hitaji hili linadai mabadiliko ya kina miongoni mwa viongozi wa Serikali, viongozi wa vyama vya kisiasa, viongozi wa kidini na wananchi kwa ujumla wao. Kanisa Katoliki limeendelea kuwa mstari wa mbele kuwahamasisha Wakatoliki kushiriki kikamilifu katika mchakato wa kutoa maoni yao kuhusu Katiba Mpya ya Tanzania. RealAudioMP3
Mambo ya kuzingatia kwanza kabisa ni kuhakikisha kwamba, haki msingi za binadamu na uhuru wa watu unaheshimiwa, sanjari na uhuru wa kidini, ambao ni mhimili wa haki msingi za binadamu. Kwa vile Katiba ya nchi ni Sheria Mama, kamwe isibebe wala kukumbatia udini unaoweza kuwa ni shinikizo kutoka kwa makundi ya kidini nchini Tanzania.
Sharia, Mahakama ya Kadhi na Mahakimu wa Makahaka ya Kadhi ni mambo ambayo hayapaswi kuingizwa kwenye Katiba ya Tanzania, kwani Tanzania kimsingi ni nchi ambayo haina dini na wala Serikali yake haina dini, lakini watu wake wa dini na imani zao zinazopaswa kuheshimiwa na kulindwa Kikatiba. Shinikizo kutoka katika makundi ya kidini linaweza kuvuruga misingi ya haki, amani, utulivu na mshikamano wa kitaifa. Imani zisipingane na haki msingi za binadamu. Kama kuna kundi linalotaka uwapo wa Mahakama ya Kadhi, basi ijitegemee na wala isiwe ni sehemu ya shughuli za Serikali.
Kanisa Katoliki lina Mahakama yake, lakini hiki ni chombo huru kinachojitegemea na hakihitaji ridhaa ya ya Serikali ili kutekeleza majukumu yake. Katiba Mpya itetee na kulinda maisha ya mtu tangu pale anapotungwa mimba hadi mauti ya kawaida inapomfika, kamwe Katiba isikumbatie utamaduni wa kifo. Kuna haja pia ya kufuta adhabu ya kifo!

Mchango wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania katika mchakato wa kuandika Katiba Mpya

Mchango wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania katika mchakato wa kuandika Katiba Mpya



Askofu Severine Niwemugizi, Makamu Rais, Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania, mwishoni wa juma, amewasilisha mapendekezo ya Baraza la Maaskofu Katoliki katika mchakato wa kutoa maoni ya Katiba Mpya ya Tanzania, wakati huu, Tume ya Mabadiliko ya Katiba inapoendelea kupokea maoini kutoka kwa Makundi. Anasema, Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania linapinga Mahakama ya Kadhi kuanzishwa na kugharimiwa na Serikali na kwamba, hili ni suala ya waamini wa dini ya Kiislam, wanapaswa wao wenyewe kuianzisha na kuigharimia kwa fedha za waamini wenyewe. Mambo ya kidini si vyema yakaingizwa katika masuala na gharama za Serikali.
Mantiki inayoongoza ukweli huu ni kwamba, dini imekuwepo kabla hata ya Serikali, kumbe, dini inaweza kuongoza mambo yake bila ya kuhitaji ridhaa ya Serikali. Pili, waamini wasiokuwa wa dini ya Kiislam hawaifahamu kwa undani misingi ya Mahakama ya Kadhi, kwani Kadhi ni Mtawala ana Hakimu. Sifa ya kuwa Kadhi ni lazima uwe mwamini wa dini ya Kiislam. Canada ni mfano bora wa kuigwa katika kuendesha Mahakama ya Kadhi.
Akizungumzia kuhusu Tanzania kuwa na uhusiano wa Kidiplomasia na Vatican, Askofu Niwemugizi alifafanua kwamba, tangu Mwaka 1929 katika Mkataba wa Laterano, Vatican ilijitenga na Italia na hivyo kuwa ni nchi huru inayojitegemea kwa mambo yake na kwamba, inatambulikana hivyo hata katika Jumuiya ya Kimataifa na wala si Shirika au Jumuiya ya Kidini. Ikiwa Tanzania inataka kuvunja uhusiano wake wa Kidipolomasia na Vatican iko huru na ni sawa na kuvunja uhusiano na nchi kama Iran.
Askofu Niwemugizi, ambaye kitaaluma ni Jaalim wa Sheria za Kanisa, anafafanua kwamba, Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania limeweka bayana ukweli huu, kutokana na uvumi unaoendelea kuzagaa nchini Tanzania kwamba, Serikali inaoongozwa na kuendeshwa kwa mfumo wa Kanisa Katoliki na shinikizo kutoka kwa Waamini wa dini ya Kiislam kwamba, sasa umefika wakati kwa Tanzania kujiunga na Jumuiya ya Nchi za Kiislam, OIC. Lakini, ikumbukwe kwamba, lengo la OIC ni kueneza Uislam na kufuta Ukristo katika nchi wanachama. Kumbe, OIC haipaswi kuingizwa katika Katiba, kwa vile Tanzania ina uhusiano wa Kidiplomasia na Vatican.
Kwa uapnde wake Amri mkuu wa Baraza la Jumuiya na Taasisi za Kiislam nchini Tanzania, ameitaka Tume ya Marekebisho ya Katiba kutofanyia mzaha suala la Mahakama ya Kadhi na kupendekeza kwamba, suala hili linapaswa kutambulika Kikatiba na kugharimiwa na Serikali. Mahakama ya Kadhi itaongozwa na wasomi wa Sheria za dini ya Kiislam ambao watatoa hukumu kwa masuala ya ndoa, mirathi na talaka.
Anasema, ikiwa kama suala hili litaachiwa mikononi mwa Waislam wenyewe wanaweza kujikuta wakitumia Sharia, kinyume cha Sheria za Nchi. Waamini wa dini ya Kiislam wanataka Ijumaa, iwe ni Siku ya Mapumziko Kitaifa kwa Waislam wote na wanafunzi waruhusiwe kwenda misikitini inapofika saa sita mchana.

Wanajeshi wa vikosi vya ulinzi na usalama mjini Vatican wanahimizwa kutolea ushuhuda ujumbe wa Injili katika medani mbali mbali za maisha!

Wanajeshi wa vikosi vya ulinzi na usalama mjini Vatican wanahimizwa kutolea ushuhuda ujumbe wa Injili katika medani mbali mbali za maisha!



Baba Mtakatifu Benedikto wa kumi na sita, Jumatatu, tarehe 14 Januari 2013 amekutana na kuzungumza na wanajenzi wa vikosi vya ulinzi na usalama vinavyotekeleza majukumu yao mjini Vatican, kama sehemu ya utamaduni wa kutakiana kheri na matashi mema kwa Mwaka Mpya wa 2013.

Amewashukuru kwa utekelezaji wa majukumu ya ulinzi na usalama mjini Vatican yanayozingatia sadaka na weledi wa kazi, kwa maelfu ya watu wanaofika mjini Vatican kumtembelea Khalifa wa Mtakatifu Petro pamoja na Makaburi ya Mitume na Mapapa waliotanguliwa mbele ya haki wakiwa na tumaini la ufufuko, lakini kwa namna ya pekee Mwenyeheri Yohane Paulo wa Pili.

Utekelezaji wa majukumu haya unajionesha hata wakati wa hija zake za kichungaji ndani na nje ya mji wa Roma, mambo yanayomsukuma Baba Mtakatifu Benedikto wa kumi na sita, kuonesha kweli moyo wa shukrani kutokana na utayari wao katika huduma, makini na watu ambao wana sifa. Hii ni heshima kama sehemu ya utambulisho wao kama wafanyakazi wa serikali na Wanajumuiya wa Kanisa na ni kielelezo cha uhusiano mwema kati ya Vatican na Serikali ya Italia.

Ni matumaini ya Baba Mtakatifu kwamba, magumu na sadaka kubwa wanayoitoa katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku, bila kusahau changamoto na hatari wanazoweza kukutana nazo, kiwe ni kielelezo cha imani yao ya Kikristo, tunu msingi ya maisha ya kiroho ambayo wao wameirithi kutoka kwa wazazi wao na sasa wanaalikwa kuwarithisha pia watoto wao.

Maadhimisho ya Mwaka wa Imani iwe ni fursa kwa wanajeshi wa vikosi vya ulinzi na usalama kutangaza kwa njia ya ushuhuda wa maisha yao, Ujumbe wa Injili ya Kristo uweze kupenya katika dhamiri, maisha ya kawaida kwa kushuhudia nguvu ya upendo wa Mungu katika medani mbali mbali za maisha.

Baba Mtakatifu anasema kwamba, katika ujumbe wake kwa Siku ya Kuombea Amani Duniani kwa Mwaka 2013, amebainisha aina mbali mbali za kazi za kulinda na kudumisha amani, jambo linaloonesha wito wa mwanadamu katika kulinda amani, kwani hamu ya kuishi katika amani ni kielelezo cha tamaa ya kutaka kupata utimilifu wa maisha na furaha ya kweli.

Baba Mtakatifu anawatakia wanajeshi wa vikosi vya ulinzi na usalama utaratibu na utulivu; mambo yanayojenga maisha yenye amani na utulivu na kielelezo cha ustaarabu wa kweli. Anawaweka wote chini ya ulinzi na usimamizi wa Bikira Maria, ili aweze kuwaombea kwa Mwanaye Mpendwa: maendeleo, amani, utulivu na kuwalinda dhidi ya hatari zote za maisha: kiroho na kimwili.

Askofu Desiderius Rwoma ateuliwa kuwa Askofu Mpya wa Jimbo Katoliki Bukoba, Jimbo la Singida sasa liko wazi!

Askofu Desiderius Rwoma ateuliwa kuwa Askofu Mpya wa Jimbo Katoliki Bukoba, Jimbo la Singida sasa liko wazi!



Baba Mtakatifu Benedikto wa kumi na sita, amekubali ombi la Askofu Nestori Timanywa wa Jimbo Katoliki Bukoba, kung'atuka kutoka madarakani na badala yake amemchagua Askofu Desiderius M. Rwoma wa Jimbo Katoliki Singida, kuwa Askofu mpya wa Jimbo Katoliki la Bukoba, Tanzania.

Kwa sasa Jimbo Katoliki Singida, liko wazi. Wakati huo huo, Baba Mtakatifu Benedikto wa kumi na sita, amemteua Askofu Desiderius Rwoma kuwa Msimamizi wa Kitume wa Jimbo Katoliki Singida.

Askofu Rwoma, alizaliwa kunako tarehe 8 Mei 1947, Jimboni Bukoba. Baada ya masomo na majiundo yake ya Kikasisi akapadrishwa kunako tarehe 28 Julai 1974. Kwa miaka mingi alikuwa ni Gombera wa Seminari Ndogo ya Rubya na Makamu Askofu jimbo Katoliki Bukoba.

Tarehe 19 Aprili 1999 aliteuliwa na Baba Mtakatifu Yohane Paulo wa Pili kuwa Askofu wa Jimbo Katoliki Singida, kufuatia kifo cha Askofu Bernard Mabula. Akawekwa wakfu na Kardinali Polycarp Pengo, Askofu mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam hapo tarehe 11 Julai 1999, Kwenye Kanisa kuu la Moyo Mtakatifu wa Yesu, Jimbo Katoliki Singida.

Wabunge wa Kenya wajiongezea marupurupu kibao kabla ya kuvunjwa kwa Bunge!

Wabunge wa Kenya wajiongezea marupurupu kibao kabla ya kuvunjwa kwa Bunge!



Kabla ya wananchi wa Kenya hawajarejea tena kwenye mchakato wa uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika hapo tarehe 4 Machi, 2013, Wabunge wa Kenya wameamua kujiongezea marupurupu zaidi, yatakayoigharimu Serikali ya Kenya kiasi cha shilingi billioni mbili, watakapokuwa wanahitimisha shughuli zao Bungeni. Katika muswada huo wa sheria, wabunge wanataka wapewe hati za kusafiria zenye hadhi ya kibalozi, usalama wao pamoja na kupewa mazishi ya kitaifa.

Wananchi wengi wa Kenya wanauangalia muswada huu kwa jicho la makengeza, wakati wanasubiri kama utapishiwa na Rais Mwai Kibaki ili uweze kuwa ni sheria. Katika muswada huo, Rais wa Kenya baada ya kumaliza utumishi wake, atakabidhiwa kitita cha jumla ya shilingi za Kenya millioni 12.6. Baadhi ya wananchi wa Kenya waliohojiwa wanasema kwamba, katika muswada huu Wabunge wameshindwa kuonesha uzalendo kwa nchi yao na badala yake wamejizamisha katika uchu wa mali na heshima, ingawa baadhi yao wanaendelea kushutumiwa kwamba ni mafisadi, wala rushwa na wazembe.

Waziri mkuu wa Kenya, Raila Odinga anasema, Wabunge wanapaswa kutekeleza wajibu na dhamana yao kwa wananchi waliowapigia kura badala ya kujiingiza katika tamaa ya kupenda fedha mno, inayoweza kuhatarisha amani, usalama na ustawi wa nchi. Hata baada ya kung'atuka madarakani bado wabunge wanataka wapewe ulinzi? Baadhi ya wananchi wanaendelea kuhoji! Wamesahau kwamba, kuna watu wasiokuwa na hatia nchini Kenya wanaendelea kupoteza maisha yao kutokana na ukosefu wa ulinzi na usalama! Lakini wao, jambo hili wanalifumbia macho na kutoa kipaumbele cha kwanza kwa masilahi yao binafsi.