Na Thompson Mpanji,Mbeya
BAADHI ya wazazi jijini Mbeya wamehoji ukimya wa serikali katika kuhusu
malalamiko yao ya utozwaji wa fedha za madawati na michango mingine
katika zoezi zima la uandikishaji wa wanafunzi wa darasa la kwanza kwa
mwaka 2013 katika shule mbalimbali zikiwemo za msingi na Kata.
Aidha wazazi hao wamehoji vinakopotelea baadhi ya vifaa vinavyoagizwa na wakuu wa shule za sekondari za kata kwa kila mwanafunzi kupeleka majembe,Madawati,fyekeo,ndoo na bunda la karatasi(Rim) kwani imekuwa ni kero kubwa.
"Kila mwaka walimu wanaagiza wanafunzi wanaofika kuanza kidato cha kwanza katika sekondari za kata kwenda na vifaa hivyo,hayo majembe ukienda kuangalia stoo zao hakuna wanayapeleka wapi,wanaagiza ndoo mpya lakini hata bustani ya kumwagilia hawana,alisema Mzazi aliyejitambulisha kwa jina la Johnson Mwambepo,mkazi wa Forest.
Mzazi mwingine aliyejitambulisha kwa jina la Richard mngoni mkazi wa Kata ya Ruanda alihoji fedha wanayotozwa kiasi cha Sh.24,500 kwa ajili ya kumwandikisha mtoto darasa la kwanza katika shule ya msingi Muungano,jijini Mbeya.
Alisema yeye(Richard) yupo kitandani kwa muda wa mwezi mmoja sasa akiwa anasumbuliwa na homa lakini ameshangazwa kupelekewa taarifa na mke wake aliyempeleka mtoto kuandikisha darasa la kwanza katika shule hiyo iliyopo maeneo ya Stereo kuwa zinahitajika fedha hizo ilhali hajafanyakazi ya kuingiza fedha kutokana na kuuguwa.
Wakati wazazi hao wakilalamikia hali hiyo serikali ya mtaa wa Ilomba,jijini Mbeya nayo imelalamikiwa kwa kuwatoza Sh.12,500 mchango wa kuandikisha jina la kuingia darasa la kwanza mwaka 2013.
Aidha wazazi hao wamehoji vinakopotelea baadhi ya vifaa vinavyoagizwa na wakuu wa shule za sekondari za kata kwa kila mwanafunzi kupeleka majembe,Madawati,fyekeo,ndoo na bunda la karatasi(Rim) kwani imekuwa ni kero kubwa.
"Kila mwaka walimu wanaagiza wanafunzi wanaofika kuanza kidato cha kwanza katika sekondari za kata kwenda na vifaa hivyo,hayo majembe ukienda kuangalia stoo zao hakuna wanayapeleka wapi,wanaagiza ndoo mpya lakini hata bustani ya kumwagilia hawana,alisema Mzazi aliyejitambulisha kwa jina la Johnson Mwambepo,mkazi wa Forest.
Mzazi mwingine aliyejitambulisha kwa jina la Richard mngoni mkazi wa Kata ya Ruanda alihoji fedha wanayotozwa kiasi cha Sh.24,500 kwa ajili ya kumwandikisha mtoto darasa la kwanza katika shule ya msingi Muungano,jijini Mbeya.
Alisema yeye(Richard) yupo kitandani kwa muda wa mwezi mmoja sasa akiwa anasumbuliwa na homa lakini ameshangazwa kupelekewa taarifa na mke wake aliyempeleka mtoto kuandikisha darasa la kwanza katika shule hiyo iliyopo maeneo ya Stereo kuwa zinahitajika fedha hizo ilhali hajafanyakazi ya kuingiza fedha kutokana na kuuguwa.
Wakati wazazi hao wakilalamikia hali hiyo serikali ya mtaa wa Ilomba,jijini Mbeya nayo imelalamikiwa kwa kuwatoza Sh.12,500 mchango wa kuandikisha jina la kuingia darasa la kwanza mwaka 2013.
Wakizungumza na gazeti hili baadhi ya wazazi (majina
yamehifadhiwa)walisema kuwa wameshangazwa viongozi wa serikali ya mtaa
kuandikisha majina ya watoto kwa kutoza sh.12,500 na kwamba mzazi
asiyekuwa na kiasi hicho mtoto wake hawezi kupokelewa.
Walisema wameambiwa kuwa mzazi ambaye hataweza kutoa fedha hiyo
mtoto wake hawezi kusoma shuleni hapo na endapo atakubaliwa basi
atatakiwa kukaa chini kwenye vumbi hatoruhusiwa kukalia dawati jambo
ambalo wamedai ni unyanyasaji.
Mmoja wa wajumbe wa serikali ya mtaa wa Ilomba,Edwin Kamweli
alisema hizo ni mbinu chafu za baadhi ya wanasiasa kutaka kuzorotesha
maendeleo ya mtaa wa Ilomba kwani mkutano wa hadhara ulikaa na
kukubaliana wanannchi wote kutoa mchango huo kwa ajili ya kuboresha
mazingira ya shule.
"Huu mfumo wa vyama vingi utaturudisha nyuma tukiendekeza maneno
bila vitendo…kuna watu wavivu wanatumia fursa ya demokrasia kuturudisha
nyuma na sisi tunasema hatuwezi kukubali na haiwasaiidii tunasonga
mbele…vikao na mikutano ikiitishwa wanasema wapo bize tuikipitisha
maazimio wanasema tunawaonea,"alisema.
Kamwela alisema kiasi hicho cha sh.12,500 kilipitishwa na
wananchi waliohudhuria mkutano mmoja wa hadhara ikiwa na lengo la
kuboresha mazingira ya shule na wanafunzi ili waweze kusoma bila
kubanana.
Alisema mgawanyo wa fedha hiyo ni Sh.10,000 kwa ajili ya dawati
litakalochangiwa na wanafunzi watatu watakaolitumia ambapo kila mmoja
atachangia kiasi hicho na kukamilisha gharama ya ununuzi wa dawati moja
kwa Sh.30,000.
Mwalimu huyo mstaafu aliendelea kufafanua kuwa katika shule hizo
mbili za Kagera na Ruanda Nzwovwe kuna mlinzi anayelipwa na hivyo kila
mzazi wamekubaliana achangie Sh.1,500 ambapo mchango wa maji ni
Sh.1,000.
Ofisa Mtendaji wa Kata ya Ilomba,Erasto Mwakapoma alifafanua kuwa
uandikishwaji ni bure lakini michango hiyo ilitokana na wananchi wenyewe
baada ya kukaa katika mkutano wa hadhara wa mtaa wa Ilomba
Novemba,30,2012 ambapo yeye alikaribishwa na kwamba wanaochangia ni
wananchi wote na siyo wazazi wanaowaandikisha watoto shule pekee.
Mwakapoma alisema shule ya msingi Kagera na Ruanda Nzovwe
zinatarajia kuandikisha watoto zaidi ya 200 ingawa lengo lilikuwa watoto
130,lakini hawatoweza kukataa kuwaaandiskisha watoto waliofikia umri wa
kwenda shule hivyo kunahitajika madawati ya ziada.
Hata hivyo baadhi ya wakazi wa Jiji la Mbeya walisema endapo kila mwaka wanafunzi wanaenda na madawati mapya ama kulipia gharama ya madawati kusengeendelea kuwepo kwa tatizo la madawati na vifaa vingine kutokana na michango inayotolewa wakati wa uandikishwaji wa darasa la kwanza na kidato cha kwanza.
Mwisho.
Hata hivyo baadhi ya wakazi wa Jiji la Mbeya walisema endapo kila mwaka wanafunzi wanaenda na madawati mapya ama kulipia gharama ya madawati kusengeendelea kuwepo kwa tatizo la madawati na vifaa vingine kutokana na michango inayotolewa wakati wa uandikishwaji wa darasa la kwanza na kidato cha kwanza.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment