Kanuni msingi katika utoaji wa maoni juu ya mchakato wa kuandika Katiba Mpya ya Tanzania
Waamini wa Kanisa Katoliki waendelee kuchangia maoni yao wakizingatia kwa namna ya pekee: utu na heshima ya kila mtu aliyeumbwa kwa sura na mfano wa Mungu; upendo, mafao ya wengi, haki msingi za binadamu, ustawi na maendeleo ya wengi nchini Tanzania.
Watanzania wanahitaji Katiba itakayojibu kero sugu na changamoto ambazo zimekuwa ni kikwazo cha maendeleo ya wengi; ijielekeze katika kudumisha haki na amani. Katiba mpya iwe ni ile Katiba inayotekelezeka na kuwajibisha. ibainishe sheria na kanuni za kupambana na saratani ya rushwa ambayo imejikita katika mihimili ya dola ambayo ni Serikali, Mahakama na Bunge.
No comments:
Post a Comment