Watoto wana haki ya kuonja upendo kutoka kwa mama na baba zao!
Askofu mkuu Laffitte katika mahojiano kwa njia ya simu na Shirika la Habari la Zenit, ameshutumu muswada wa sheria ya ndoa za watu wa jinsia moja kwa kusema kwamba, watu wenye mapenzi mema wana haki ya kupinga sheria ambazo zinakwenda kinyume cha mafao ya wengi, utu na heshima ya binadamu.
Katika kampeni yake kuwania nafasi ya Urais nchini Ufaransa, Rais Francois Hollande aliahidi kwamba, ikiwa kama angeshinda uchaguzi mkuu nchini Ufaransa, angetunga sheria inayoruhusu ndoa za watu wa jinsia moja. Muswada huu wa sheria unaanza kujadiliwa nap engine, ukapita na kuanza kutumika kama sheria, baada ya kupitishwa, mwishoni mwa Mwezi Juni, 2013.
Askofu mkuu Jean Laffitte anawapongeza na kuwashukuru watu wote waliosimama kidete kupinga mmong’onyoko wa maadili; kwa kusimamia mafao ya wengi, kwani kwa asili ndoa ni kati ya bwana na bibi na wala si kinyume chake. Hii ndiyo taasisi ya kweli ambamo motto anaweza kuonja upendo wa kweli kutoka kwa baba na mama yake!
No comments:
Post a Comment