Na Thompson Mpanji,Mbeya Askofu Evaristo Chengula wa Jimbo Katoliki Mbeya, Tanzania anatarajiwa kufungua Maadhimisho ya Sinodi ya Jimbo Katoliki Mbeya, Januari, 2013 kwa kupania kujikita zaidi katika Utume wa Familia. Waamini wataweza kupata nafasi ya kutembeleana nyumba hadi nyumba ili kuimarisha Utume wa Familia, ambayo kwa sasa inakabiliwa na changamoto mbali mbali kutoka ndani na nje ya familia yenyewe. Askofu Chengula anabainisha kwamba, Sinodi ya Jimbo Katoliki Mbeya, itakuwa ni fursa ya kufanya tafakari ya kina kuhusu maisha na utume wake mintarafu mchakato wa Uinjilishaji Mpya, changamoto iliyotolewa na Mababa wa Sinodi ya Maaskofu juu ya Uinjilishaji Mpya, iliyohitimishwa hivi karibuni mjini Vatican. Katika maadhimisho hayo, Jimbo Katoliki Mbeya, litazindua pia Mkakati wa shughuli za kichungaji, ambao utakuwa dira na mwongozo wa Jimbo Katoliki Mbeya kwa miaka kadhaa ijayo. Kanisa linapenda kuimarisha imani miongoni mwa waamini kwa kujikita zaidi katika masuala ya Maandiko Matakatifu, Katekesimu Mpya ya Kanisa Katoliki, Mafundisho Jamii ya Kanisa pamoja na kuendelea kutafakari kuhusu utajiri mkubwa unaofumbatwa katika Nyaraka za Mtaguso Mkuu wa Pili wa Vatican; changamoto kwa waamini kuchuchumilia utakatifu wa maisha, sanjari na kuendeleza jitihada za Mama Kanisa katika kuyatakatifuza malimwengu kwa njia ya ushuhuda wa maisha yao amini. Maadhimisho ya Sinodi ya Jimbo Katoliki Mbeya, itakuwa ni fursa kwa Kanisa Jimboni Mbeya, kufanya tathmini ya kina kuhusu: majadiliano ya kidini na kiekumene, ikizingatiwa kwamba, Mbeya ni kati ya mikoa ambayo ina idadi kubwa ya madhehebu mbali mbali ya Kikristo, pengine, kuliko sehemu nyingine yoyote ya Tanzania. Ni muda wa kukazia majadiliano ya kidini na waamini wa dini ya Kiislam, ili kujenga na kuimarisha misingi ya: haki, amani, upendo na mshikamano wa kitaifa; daima wajikitahidi kutafuta mafao ya wengi. Uchumi na maendeleo ya Kijamii ni mada itakayochambuliwa mintarafu Mafundisho Jamii ya Kanisa, ikizingatiwa kwamba, leo hii kuna idadi kubwa ya watu wanaoendelea kutumbukia katika baa la umaskini, ujinga na njaa na kwamba, hali inazidi kuwa mbaya hata kuliko ilivyokuwa miaka kadhaa iliyopita! Hapa kuna haja ya sera na mikakati ya maendeleo kutoa kipaumbele cha kwanza kwa utu na heshima ya binadamu, aliyeumbwa kwa sura na mfano wa Mungu. Baada ya Maadhimisho ya Sinodi ya Jimbo Katoliki Mbeya, Askofu Evaristo Chengula anatarajiwa kutoa Waraka mara baada ya Sinodi, utakaokuwa ni dira na mwongozo wa Kanisa Katoliki Mbeya katika mikakati yake ya shughuli za kichungaji na kitume! Ni mwaliko kwa Familia ya Mungu Jimbo Katoliki Mbeya kushikamana na kutembea kwa pamoja, ili waweze kwa pamoja kutolea ushuhuda wa imani yao kwa Kristo na Kanisa lake. |
Translate
Friday, November 30, 2012
Jimbo Katoliki Mbeya linajiandaa kuadhimisha Sinodi ya Jimbo kwa kujikita katika Utume wa Familia
Monday, November 26, 2012
mwanamke anayetuhumiwa kumtesa hadi kukatwa mkono mtoto Aneth kizimbani
Na Thompson Mpanji,Mbeya
MWANAMKE
anayetuhumiwa kumtesa kumlisha kinyesi na kumchoma moto mtoto wa kaka yake
kumfungia ndani, amepandishwa kizimbani kwa mara ya pili katika mahakama ya Wilaya ya Mbeya kujibu
shtaka linalomkabili.
Mwendesha
mashtaka wa Serikali, Achiles Mulisa ameileza Mahakama kuwa Mtuhumiwa Wilvina Mkandala (24)
Mkazi wa Majengo jijini humo alitenda kosa la kusababisha majeraha akiwa
na nia ovu ambayo imemsababishia ulemavu mtoto Aneth Gasto (4).
Mulisa
akisoma mashtaka hayo mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi wa mahakama hiyo Gilbert
Ndeuruo amesema kosa hilo ni kinyume cha kanuni ya adhabu kifungu cha
222(a) sura ya 16 kama ilivyorejewa mwaka 2002.
Kutokana na hali hiyo
mwendasha mashitaka huyo ameileza mahakama kuwa kesi inayo mkabili mwanamke
huyo ilihitaji mashahidi sita ambao ni Dactari aliye mfanyia upasuaji mtoto
huyo mwenyekiti wa Mtaa na barozi wake pamoja na Askari
mpelelezi wa kesi hiyo na mtoto mwenye .
Amesema
teyari mashahidi wanne kati ya sita wamekwisha toa ushahidi wao mahakani hapo .
Kutokana
na kosa hilo mshtakiwa amekana shitaka hilo ambapo alirudishwa mahabusu hadi
Novemba 27 Mwaka huu kesi hiyo itakapotajwa tena.
Amesema
upande wa Jamhuri unamashahidi wanne ambao watatu kati yao teyari wamekwsha toa
ushahidi wao katika mahakama hiyo .
Amewataja
mashahidi hao kuwa ni Mwenyekiti wa Mtaa wa Majengo Shuku Mwakanyamale, Daktari
anayemtibu mhanga katika Hospitali ya Rufaa ya Mbeya Dr. Paul Kasubi na Habiba Mwakanyamale.
Wengine
ni Askari Polisi aliyepeleza kesi hiyo WP Pudensia na Mtoto mwenyewe ambao wako tayari kufika mahakamani na kutoa
ushahidi wao mbele ya mahakama.
Awali
mshatakiwa huyo aliieleza mahakama kuwa na uhusiano na mtoto huyo ambapo
pia alikiri kuwa na taarifa za kile kinachoendelea juu ya matibabu ya mtoto huyo
na kuhusu kukatwa kwa mkono wake wa kushoto na kufungwa bandeji ngumu(POP)
kwenye mkono uliobaki.
TAMISEMI yawataka tanesco na mamlaka nyingine zisikwamishe ujenzi wa miradi ya Worl Bank
Na Thompson Mpanji,Mbeya
OFISI ya Waziri Mkuu
Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
(TAMISEMI) imewaagiza Mameneja wa mikoa wa tanesco,mamlaka za maji na
simu kuhakikisha wanatoa ushirikiano katika kuhakikisha miradi
iliyofadhiriwa na Benki ya dunia haihujumiwi.
Aidha
imesema uchgelewaji wa miradi hiyo ambayo imetolewa fedha na benki ya
dunia zaidi ya Sh.Bil.28 katika Halamshauri saba na CDA imekuwa
ikichelewa kukamilika hasa katika baadhi ya mikoa ya Dodoma,Arusha
kutokana na baadhi ya wakuu wa taasisi mbali mbali
zinazohusika na miundo mbinu kuchelewa kuondoa miundo mbinu yao kwa madai ya gharama kubwa za kuhamisha.
Rai hiyo ilitolewa na
Kaimu katibu mkuu ofisi ya Waziri Mkuu
Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
(TAMISEMI),Jumanne Sagin wakati akifungua
mkutano wa wakurugenzi wa Halmashauri saba Nchini na Mamlaka
ya ustawishaji Dodoma (CDA) ambako ipo miradi hiyo (Nov,19)jana Jijini Mbeya katika ukumbi wa Mkapa.
Sagin alisema kuwa katika
kipindi cha miezi 15 tangu kuanza utekelezaji wa awamu ya miradi hiyo
kumekuwepo na mafanikio makubwa katika miradi hiyo ambayo ni pamoja na miundo mbinu
ya barabara,masoko,vituo vya mabasi,madampo,utunzaji na uhifadhi wa mazingira na kwamba baadhi
ya miradi ilikwamba kutokana na ukiritimba wa baadhi ya wakuu wa
taasisi.
Bw.Sagin Alisema kuwa kutokana na hali hiyo amepanga kuonana
na makatibu wakuu wa wizara zinazosimamia taasisi hizo ikiwa ni pamoja na
wizara ya Nishati na Madini na Maji kwa ajili ya kuhakikisha mameneja wa Tanesco wa Mikoa wanakuwa na uelewa kuhusiana na umuhimu wa kukamilika kwa miradi hiyo.
Alisema kuwa wakuu wa
Taasisi hizo wanapaswa kujua kuwa
kukamilika kwa miradi hiyo ni ukombozi wa watanzania na ukuaji wa
uchumi kutokana na ukweli
kuwa kuwapo kwa miundo mbinu hiyo kunalenga kuondoa umaskini miongoni mwa watanzania na kutekeleza adhama ya maisha bora kwa kila mtanzania .
Alisema kuwa warsha
hiyo ya siku mbili inalenga kuwakumbusha
wakuu wa Halmashauri na wadau wengi walioalikwa
kuona umuhimu wa kuhakikisha wanasimamia na kutoa ushirikiano kuhakikisha
miradi hiyo inakamilika kwa wakati uliopangwa na kuachana na tabia ya sasa ya kila mtu kutaka kulipwa kwa ajili ya kuhamisha miundo
mbinu yake zikiwemo nguzo.
Kaimu katibu mkuu
huyo alisema kuwa miradi hiyo
inalenga kubadili maisha ya watanzania kwa ajili ya kuhakikisha wanatumia miundo
mbinu hiyo katika kuachana na umaskini mkubwa walio nao na kuwa na hali
bora kutokana na miundo mbinu hiyo kwa kusimamiwa na kutunzwa vema.
Aidha aliwataka wakurugenzi
wa Halmashauri hizo kutunza na kuendeleza miradi hiyo ili iweze kuwa
endelevu na bora na hivyo kuwasaidia watanzania wengi kwa muda mrefu tofauti na ilivyo sasa ambapo
miradi mingi imekuwa ikihujumiwa
.
Mwisho
Tanzania itakombolewa na wanahabri
Na Thompson Mpanji,Mbeya.
IMEELEZWA kuwa Tanzania
itakombolewa endapo wanahabari wataisoma
historia tangu uhuru,kuchambua na kufuatiliaji utekelezaji wa sera sanjari
na kutoa taarifa sahihi na kamili
kupitia vyombo vya habari.
Hayo yamesemwa na mwezeshaji
wa mafunzo ya uchambuzi wa sera na mchanganuo wa bajeti,Robert Renatus wakati
akitoa mada katika mafunzo yanayoendelea kwa wanahabari katika ukumbi wa
Ukaguzi jijini Mbeya.
Alisema wanahabari ndiyo watu pekee watakaoweza
kuikomboa nchi kutokana na hali ngumu ya maisha kwa watanzania kupitia kuzichambua sera mbalimbali na
kuziandikia habari za kina ikiwemo na makala juu ya utekelezaji wake.
Mwezeshaji huyo alitolea mfano Nchi za Ulaya na
magharibi wamefanikiwa katika uchumi wa
mtu mmoja mmoja na taifa kwa ujumla na hatimaye kufikia maendeleo
makubwa kutokana na kutumia mfumo wa SWOT Analysis kwa kuangalia
uwezo,udhaifu,fursa na vitisho.
Alisema vyombo vya habari
vinapaswa kutumia nafasi yake kukosoa utekelezaji mbovu wa sera ili sekta husika ziweze kubadilika,kujisahihisha,kuwa
makini na kufanya usimamizi mzuri na
hatimaye kufikia lengo lililokusudiwa la kumsaidia mtanzania.
Hata hivyo wakipitia
muhtasari wa mada ya sera washiriki wa mafunzo hayo walisema wamepata ufahamu
mkubwa na kubaini kuwa sera zinatungwa ngazi za juu bila kushirikishwa wananchi na hivyo kushindwa kutekelezeka,.
Aidha katika mafunzo hayo
imebainika kuwa baadhi ya wanahabari wamekuwa wakilipua katika kufanya kazi zao
kwani hawazami kwa undani katika
uandishi kutokana na kutojuwa sera ikiwemo umuhimu wa vyombo vya habari katika
kufuatilia na kutathmini utekelezaji wa sera.
Mwisho.
JWTZ 10 mbaroni kwa kuuwa na kujeruhi Mbeya
Na Thompson Mpanji,Mbeya
ASKARI 10 wa Jeshi la wananchi (JWTZ) kikosi
cha 44kj Mbalizi,wanashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa tuhuma za mauaji
na kujeruhi watu wengine sita sanjari na kuharibu mali mbalimbali.
Kamanda wa polisi Mkoa wa Mbeya,Diwani
Athumani amethibitisha kutokea kwa kifo hicho Nov,18 majira ya saa 5 usiku katika hospitali teule ya Ifisi wilaya ya
mbeya vijijini mkoa wa mbeya na amemtaja marehemu kuwa ni Petro Sanga,( 25),mkulima,mkinga,
mkazi wa chapakazi, mbalizi ambaye alifariki dunia wakati akiendelea kupatiwa
matibabu hospitalini hapo.
Athuman amesema marehemu alichomwa kisu shingoni na mdomoni na
kikundi cha watu wanaosadikiwa kuwa askari
wa jeshi la wananchi wa Tanzania, tarehe hiyo majira ya saa 3 usiku akiwa katika
grocery iitwayo vavene mwe iliyopo mbalizi mara baada ya watu hao kuvamia bar iitwayo power night club
ambamo awali alikuwepo pia marehemu.
Amesema watu wengine sita walijeruhiwa kwa kupigwa sehemu mbalimbali za
miili yao na wanaodaiwa kuwa askari wa JWTZ
na kupatiwa hati ya matibabu [pf3] kwa matibabu kati yao watatu walilazwa
katika hospitali teule ya ifisi kwa matibabu zaidi na majeruhi wengine watatu walipatiwa matibabu na
kuruhusiwa.
Kamanda huyo amesema kufuatia vurugu hizo baadhi ya mali za watu
ziliharibiwa ambazo ni pamoja gari T.106 AWB aina ya toyota vista mali ya Paulo
Maximilian ilivunjwa kioo cha mbele,gari T.884 AUU Toyota Cresta mali ya Alile
Godfrey lilivunjwa side mirror upande wa kulia.
Kamanda huyo amesema kuwa wahalifu hao walianza kuwashambulia wananchi
kwa kuwapiga wakitumia ngumi, mateke, mikanda, marungu, sime na mapanga na
kwamba marehemu alijaribu kuokoa uhai wake kwa kukimbia toka
eneo hilo hadi katika grosary hiyo
lakini watu hao walimkimbiza hadi eneo hilo na kumjeruhi vibaya kwa kumchoma
kisu.
Amesema chanzo cha tukio hilo ni kulipiza
kisasi kufuatia askari Godfrey Matete( 30),mjita, wa kikosi cha 44kj mbalizi
kupigwa na walinzi wa kilabu cha pombe za kienyeji kiitwacho DDC kilichopo
mbalizi waliokuwa lindoni Nov,17,2012
majira ya saa 01:30.
Amefafanua kuwa baada ya kushambuliwa askari huyo alifungua kesi kituo cha polisi
mbalizi usiku huo kosa la kujeruhi na alipatiwa
hati ya matibabu [pf3] kwa ajili ya kwenda kupata matibabu hospitalini ambapo walinzi
wanne walikamatwa kuhusiana na tukio
hilo kwa mahojiano.
Amewataja walinzi hao kuwa ni Frenk
Mtasimwa (25),Mure Julias (26),Omari Charles (28) wote wakazi wa DDC mbalizi na Legnard Mwampete (30),mkazi wa Izumbwe na
kwamba upelelezi wa kesi hiyo bado
unaendelea.
Mwisho.
kuhusu sakata la Mbegu feki Mbozi,wakulima wapewa somo na mtafiti
Na Thompson Mpanji,Mbeya
WAKULIMA nchini wameshauriwa kujenga utamaduni wa kudai lisiti
wakati wa kununua mbegu za mazao ya aina mbalimbali katika maduka ya
pembejeo yanayotambulika ili kuepuka kuuziwa mbegu feki ambazo
zimetapakaa na kuwaletea hasara kubwa wakulima walio wengi sanjari na
kuhatarisha maisha ya walaji.
Aidha imeleezwa kuwa mbegu za mahindi ya njano ambazo zinadaiwa
kutoa unga wa njano baada ya kusagwa zinazodaiwa kusambazwa kwa wakulima
walio wengi wilayani Mbozi zinatumika kwa ajili ya malisho ya mifugo na
siyo kwa binadamu.
Akizungumza na gazeti hili Mtafiti wa zao la mahindi kutoka taasisi
ya utafiti kanda ya nyanda za juu kusini (ARI Uyole), Anderson
Elibariki Temu alisema mbegu za mahindi zenye rangi ya njano ni mojawapo
ya aina inayopendelewa sana nchini Marekani na imekuwa ikitumika kwa
ajili ya vyakula vya kuku na ng’ombe wa maziwa.
Mtafiti huyo alisema ingwa hajabahatika kuyaona mahindi hayo
yanayozungumziwa lakini kutokana na maelezo aliyoyapata ana uenda
yalizalishwa kwa ajili ya mifugo na siyo kwa ajili ya chakula cha
binadamu.
"Lakini nawashauri wakulima kwa kuona tatizo hilo na mbegu
hazijifichi inatakiwa wakulima wawe makini wawe waangalifu wakati wa
kununua mbegu kwa sababu hii imekuwa ni kero kubwa kwa wakulima wa kanda
ya nyanda za juu kusini na Tanzanja kwa ujumla Mkulima anapojitahidi
kuwa na mtaji hadi kununua mbegu, anaipanda,gharama za mbolea
,maandalizi ya shamba na gharama nyingine alafu mwisho anaikuta mbegu
aliyoipanda kwa mfano siyo Uyole Hybrid 615 ni hasara kubwa,"alisema.
Temu alisema ili mkulima aweze kukwepa udanganyifu huo anapaswa
anapoenda kununua mbegu ahakikishe mbegu ipo kwenye mifuko ya kampuni
halisia inayozalisha hiyo mbegu mfano kampuni inayozalisha mbegu za
uyole ya Highland seed growers ambapo nje ya mfuko kuna anuani na jina
la kampuni,na kwamba akwepe kununua mbegu zinazouzwa baada ya
kufunguliwa katika mfuko .
Alisema Mkulima naweza kununua mbegu iliyokuwepo katika mifuko kwa
sababu wanaweza kuiba mifuko ama kutumia ujanja wowote,kwa hiyo njia ya
mwisho ya kuwabana wauzaji wa mbegu feki ni kudai lisiti na kuitunza
hadi wakati wa msimu wa amvuno.
"ili tatizo likijitokeza la mbegu kutokuwa halisi nenda kwa ofisa
shamba ukikutana na tatizo atakuelekeza ngazi na utaratibu wa kufuata
ili mhusika weze kufuatiliwa na ikibidi sheria ichukuwe mkondo wake kwa
sababu sheria zipo kuanzia kuzalisha mbegu kuhakikisha zina ubora na
mamlaka husika zinazofuatilia zipo,hakikisha una lisiti hadi mwisho wa
msimu,"alisisistiza Mtafiti huo.
Mwisho.
Wednesday, November 14, 2012
Askofu Chengulaamwalika waziri mulugo kuchangisha zaidi ya Sh.mil.100 ujenzi wa kijiji cha watoto yatima cha Kambarage Mbeya
Na Thompson Mpanji,Mbeya
MLEZI Mkuu wa Chama cha vijana,wanawake wa kikristo
Tanzania(YWCA),Tawi la Mbeya,Askofu Evaristo Chengula wa kanisa Katoliki
Jimbo la Mbeya ametoa wito kwa watanzania wote wenye mapenzi mema bila
kujali itikadi za kisiasa,dini,kabila wala rangi kuchangia Kijiji cha
watoto yatima wanaoishi katika mazingira hatarishi na wenye mtindio wa
ubongo cha Kambarage ili kuweza kukamilisha ujenzi huo.
Askofu Chengula ambaye ndiye msimamizi mkuu wa YWCA amemualika
Naibu Waziri wa elimu na mafunzo ya ufundi,Philipo Mulugo (MP)
kuendesha harambee ya ujenzi wa Kijiji cha watoto yatima cha Kambarage
novemba, 24 mwaka huu.
Naibu waziri Mulugo anatarajia kuwa mgeni rasmi katika changizo
hilo litakaloambatana na maandhimisho ya miaka 20 ya YWCA,Tawi la Mbeya
hafla inayotarajia kufanyika katika ukumbi wa Mkapa,jijini Mbeya.
Askofu Chengula ataungana na walezi na wasimamizi wenzake wa chama
hicho ambao ni Askofu wa kanisa la Anglikana,nyanda za juu kusini, John
Mwela,Askofu wa kanisa la Moravian jimbo la kusini magharaibi,Alinikisa
Cheyo,Askofu wa Jimbo la Moravian jimbo la kusini, Lusekelo Mwakafwila
na Askofu wa KKKT Dayosisi ya Konde,Dkt.Islael Mwakyolile.
Akizungumza kwa niaba ya Askofu Chengula,Katibu wa YWCA Tawi la
Mbeya,Bi.Tabitha Bughali alisema watarajia mgeni rasmi,Naibu Waziri
Mulugo atafanikisha kuchangisha Sh.Mil.100 ili kuendeleza ujenzi huo kwa
awamu ulioanza tangu mwaka 2009 ambapo zaidi ya sh.Bil.2 zinahitajika
kukamilisha ujenzi huo.
Katibu huyo alisema awali Mwenyekiti wa IPP Media, Reginald Mengi
alichangia zaidi ya Sh.Mil.25 kusaidia ujenzi huo na baadhi ya wadau
wengine waliochangia ni pamoja na mmiliki wa shule za Clementine
foundation Marry Camm ambaye anatarajiwa kuwasili katika shughuli
hizo,Prof.Mwansoko,Mbunge wa viti maalum Mh.Hilda Ngoye,Prof.Mark
Mwandosya na wadau wengi.
Amewataja wageni watakaohudhuria katika changizo hilo ni Mkuu wa
Mkoa wa Mbeya,Abbas Kandoro,Wakuu wa Wilaya zote za Mkoa wa
Mbeya,wabunge,wakurugenzi wa halmashauri,wakurugenzi wa mahoteli ambapo
baadhi ya wadau tayari wameshaanza kutoa michango yao kama Wakili
Mbise,,Makasini Hotel,Mwenyekiti wa umoja wa wamiliki wa hoteli
Mahenge,Penge Hoteli,Wakili Mshokolwa na wakili Msigwa.
Bi.Bughali alisema shughuli hiyo itaendeshwa na kamati ya
maandalizi inayoongozwa na Jaji Upendo Msuya ambaye ndiye Mwenyekiti wa
kamati ya hiyo na kwamba wafanyabiashara,taasisi za serikali na binafsi
na watu mbalimbali wenye mapenzi mema wanatarajia kushiriki katika
harambee hiyo na ametoa wito kwa watanzania wote kujitokeza kuiunga
mkono YWCA katika harakati za kuwasaidia watoto yatima.
Mwisho.
Tuesday, November 13, 2012
Wajasiliamali Mbeya wasema bidhaa za nje zinawatesa
Na Thompson Mpanji,Mbeya
BAADHI ya wajasiliamali wametoa wito kwa serikali kuwawezesha mitaji,mazingira ya kufanyia kazi sanjari na kuwaweka katika vikundi ili waweze kumudu na kuingia katika ushindani wa soko la ndani na nje kuliko ilivyo sasa ambapo bidhaa za nje zinawatesa katika soko la ndani kutokana na kuzalishwa kwa muda mfupi kwa wingi na kuuza bei ya chini.
Wakizungumza wakati wa maonesho ya wajasiliamali kutoka mikoa mbalimbali ya Tanzania na baadhi ya nchi za afrika mashariki,walisema kuwa kutokana na changamoto hiyo serikali haina budi kutumbukiza mkono wake kuwasaidia kwa hali na mali ili waweze kuendelea kujiajiri,kuwauzia watanzania wa chini,kati na juu bidhaa imara kwa bei nafuu sanjari na kupata tija na hatimaye kujiinua kiuchumi.
Mkurugenzi wa Witega Works and Fubrication iliyopo jijini Mbeya,William Gamba alisema kampuni yake inajishughulisha na utengenezaji wa zana za kilimo mathalani majembe ya kukokota kwa ng'ombe (plau) na majiko banifu lakini wamekuwa wakikumbana na ushindani mkubwa kutoka kwa wafanyabiashara kutoka nje kutokana na kuwa na mitaji midogo na vitendea kazi vya kukodi.
Alisema endapo serikali itamwezesha anao uwezo wa kutengeneza majembe ya kukokota kwa ng'ombe zaidi ya 200 kwa mwaka ambayo atawauzia wakulima kwa bei nafuu na hivyo kufikia adhama ya kauli mbiu ya taifa ya kilimo kwanza kwa vitendo na hivyo kuwakomboa wakulima hasa wa vijijini na wote wakafanikiwa kujiinua kiuchumia na kuongeza uzalishaji wa zana za kilimo na mazao.
Gamba alisema kutokana na utaalamu alioupata kutoka katika kiwanda cha utengenezaji wa zana za kilimo(ZZK) cha jijini Mbeya kilichokufa katika miaka ya 70 anao uwezo wa kutengeneza majembe ya mkono,koleo na fyekeo lakini mtaji mdogo ndiyo kikwazo.
Hata hivyo ameiomba serikali kuwaangalia kwa macho mawili waandaaji wa maonyesho mbalimbali ya wajasiliamali kwani ni kazi ngumu kuwakusanya pamoja hadi kufanikisha zoezi hilo linalohitaji wadhamani wa kutosha na fedha za kuendeshea shughuli hiyo.
Naye Mhasibu wa kampuni hiyo ambaye pia ni Mke wa Mkurugenzi huyo,Odilia Gamba ametoa wito kwa wanawake kuwasaidia waume zao katika shughuli mbalimbali za ujasiliamali ili kuinua kipato cha familia na kuendeleza miradi mbalimbali waliyoianzisha.
Maonyesho hayo ni ya tatu kuaandaliwa na Kampuni ya Mbeya Trade Fair and Enterteinment yalifunguliwa na Mkuu wa mkoa wa Mbeya,Abbas kandoro na kuwakilishwa na Mkuu wa wilaya ya Mbeya,Dkt.Norman Sigalla ambapo wageni wengine waliohudhuria maonyesho hayo ni Mkuu wa wilaya ya Ileje na kufungwa na Kamanda wa polisi Mkoa wa Mbeya,Diwani Athuman.
Katika maonyesho hayo wakazi mbalimbali kutoka ndani na nje ya Mkoa wa Mbeya walijitokeza kwa wingi kujionea na kununua bidhaa mbalimbali vikiwemo vyakula na vinywaji vya asili,nguo za asili,tiba asili,zana za kilimo na majiko banifu yanayosaidia kwa kiasi kikubwa utunzaji na uhifadhi wa mazingira.
Mwisho.
BAADHI ya wajasiliamali wametoa wito kwa serikali kuwawezesha mitaji,mazingira ya kufanyia kazi sanjari na kuwaweka katika vikundi ili waweze kumudu na kuingia katika ushindani wa soko la ndani na nje kuliko ilivyo sasa ambapo bidhaa za nje zinawatesa katika soko la ndani kutokana na kuzalishwa kwa muda mfupi kwa wingi na kuuza bei ya chini.
Wakizungumza wakati wa maonesho ya wajasiliamali kutoka mikoa mbalimbali ya Tanzania na baadhi ya nchi za afrika mashariki,walisema kuwa kutokana na changamoto hiyo serikali haina budi kutumbukiza mkono wake kuwasaidia kwa hali na mali ili waweze kuendelea kujiajiri,kuwauzia watanzania wa chini,kati na juu bidhaa imara kwa bei nafuu sanjari na kupata tija na hatimaye kujiinua kiuchumi.
Mkurugenzi wa Witega Works and Fubrication iliyopo jijini Mbeya,William Gamba alisema kampuni yake inajishughulisha na utengenezaji wa zana za kilimo mathalani majembe ya kukokota kwa ng'ombe (plau) na majiko banifu lakini wamekuwa wakikumbana na ushindani mkubwa kutoka kwa wafanyabiashara kutoka nje kutokana na kuwa na mitaji midogo na vitendea kazi vya kukodi.
Alisema endapo serikali itamwezesha anao uwezo wa kutengeneza majembe ya kukokota kwa ng'ombe zaidi ya 200 kwa mwaka ambayo atawauzia wakulima kwa bei nafuu na hivyo kufikia adhama ya kauli mbiu ya taifa ya kilimo kwanza kwa vitendo na hivyo kuwakomboa wakulima hasa wa vijijini na wote wakafanikiwa kujiinua kiuchumia na kuongeza uzalishaji wa zana za kilimo na mazao.
Gamba alisema kutokana na utaalamu alioupata kutoka katika kiwanda cha utengenezaji wa zana za kilimo(ZZK) cha jijini Mbeya kilichokufa katika miaka ya 70 anao uwezo wa kutengeneza majembe ya mkono,koleo na fyekeo lakini mtaji mdogo ndiyo kikwazo.
Hata hivyo ameiomba serikali kuwaangalia kwa macho mawili waandaaji wa maonyesho mbalimbali ya wajasiliamali kwani ni kazi ngumu kuwakusanya pamoja hadi kufanikisha zoezi hilo linalohitaji wadhamani wa kutosha na fedha za kuendeshea shughuli hiyo.
Naye Mhasibu wa kampuni hiyo ambaye pia ni Mke wa Mkurugenzi huyo,Odilia Gamba ametoa wito kwa wanawake kuwasaidia waume zao katika shughuli mbalimbali za ujasiliamali ili kuinua kipato cha familia na kuendeleza miradi mbalimbali waliyoianzisha.
Maonyesho hayo ni ya tatu kuaandaliwa na Kampuni ya Mbeya Trade Fair and Enterteinment yalifunguliwa na Mkuu wa mkoa wa Mbeya,Abbas kandoro na kuwakilishwa na Mkuu wa wilaya ya Mbeya,Dkt.Norman Sigalla ambapo wageni wengine waliohudhuria maonyesho hayo ni Mkuu wa wilaya ya Ileje na kufungwa na Kamanda wa polisi Mkoa wa Mbeya,Diwani Athuman.
Katika maonyesho hayo wakazi mbalimbali kutoka ndani na nje ya Mkoa wa Mbeya walijitokeza kwa wingi kujionea na kununua bidhaa mbalimbali vikiwemo vyakula na vinywaji vya asili,nguo za asili,tiba asili,zana za kilimo na majiko banifu yanayosaidia kwa kiasi kikubwa utunzaji na uhifadhi wa mazingira.
Mwisho.
Wednesday, November 7, 2012
Polisi Mbeya wafanikiwa kuzima jaribio la kuteka malori ya mafuta yanayosafirisha kwenda nchi jirani kupitia Mbeya,wahusika wapanga mawe barabara ya Mbeya/Tunduma maeneo ya mama john wakiwa na vidumu vitupu vya mafuta,wadai haiwezekani kukosa mafuta ilhali mafuta yanapita machoni pao,wang'ang'ania makufuli ya matenki ya mafuta
Na Thompson Mpanji,Mbeya
JESHI la polisi limefanikiwa kuzima jaribio la baadhi ya madereva
wa boda boda na daladala kuzuia magari yanayobeba mafuta kusafirisha
kwenda nchi za jirani za Zambia baada ya kuamua kuweka kizuizi cha mawe
katika barabara ya Mbeya/ Tunduma,katika maeneo ya mama John kwa madai
ya kukerwa na adha ya mafuta huku wakiyaona yakipita kuelekea nchi
jirani.
Sakata hilo limedumu kwa takribani masaa mawili tangu saa 1 asubuhi
hadi saa 3 asubuhi baada ya madereva wa daladala na waendesha boda
boda kudaiwa kupandwa na jazba ya kukosa mafuta katika kituo cha Orxy
Mama John na hivyo kuamua kupanga mawe barabarani jambo ambalo inadaiwa
endapo Polisi wasingejitokeza haraka hali ingekuwa tete kutokana na
baadhi yao kuonekana waking'ang'ania makufuli ya malori ya mafuta
waliyofanikiwa kuyazuia na kuwateremsha madereva kwa nguvu.
"Ninakwambia kulikuwa na hatari kubwa kama wasingetokea wale FFU
kwa sababu wengine walitaka kuyapiga kiberiti malori hayo ya mafuta
baada ya kuwalazimisha madereva wa magari hayo kufungua nao wakagoma na
huku madereva wa malori ya mafuta nao walikuwa wamechukia kwa hiyo
tungekuwa tunazungumza kitu kingine,na madereva wengine wa malori
walivyopata taarifa kuwa hali siyo shwari waligeuza na kurudi Uyole
kuegesha Uyole walivyopata lakini walipotokea maaskari
walitawanyika,"alisema mmoja wa wafanyakazi wa kituo hicho cha mafuta
ambaye hakutaka kutaja jina lake.
Alisema kuwa chanzo cha hasira ya watu hao hawakuamini kama mafuta
waliyokuwa wakiyatoa ya petroli kama yamekwisha na kubakiwa na mafuta ya
dizeli na hivyo kuanza kupiga kelele na kuhamishia hasira zao
barabarani hadi Jeshi la polisi likiongozwa na Mkuu wa Polisi wa Wilaya
ya Mbeya Sylivester Ibrahim kuwaaminisha kwa kumuomba mmiliki wa kituo
hicho kupima na kuhakikisha kweli hakuna mafuta waliamua kuondoka.
Gazeti hili limeshuhudia majira ya saa 4 asubuhi baada ya hali ya
utulivu kurejea malori ya mafuta yalionekana yakipita kasi katika maeneo
ya mama John tofauti na siku nyingine ambapo taarifa kutoka kituo cha
Mafuta cha Uyole yanapoegeshwa magari yanayoelekea Tukuyu kuwa mafuta
yapo ila bei ya mafuta ya petroli kwa lita inadaiwa kufikia Sh.3,000.
Mmoja wa waendesha boda boda ambaye hakutaka kutaja jina lake
alisema wamekerwa sana na kitendo cha kuhangahika na kukosa mafuta kwa
takribani siku nne sasa huku magari ya mafuta yakiwa yanapitishwa
machoni pao kwenda zambia na kwingineko jambo ambalo alidai bado
linawasumbua katika vichwa vyao kuwa serikali inafurahi kero hii
wanayoipata walala hoi wa chini huku familia zao zikiendelea kuteseka na
njaa kwa kukosa kufanyakazi.
Suala hili la ukosefu wa mafuta bado linaonekana ni kitendawili kwa
watanzania na kwamba endapo serikali haitalishughulikia na kulimaliza
haraka iwezekanavyo kuna hatari ya malori yanayosafirisha mafuta kwenda
nchi ya zambia kupitia Mbeya yakafanyiwa hujuma kutokana na kuwepo na
tetesi kuwa hawajaridhika kukosa mafuta ilhali wanayaona yanapita mbele
ya machjo yao.
Hata hivyo Mwandishi wa habari hizi ameshuhudia Mkuu wa Polisi wa
Wilaya ya Mbeya,Sylivester,Mkuu wa upelelezi wa Wilaya,Ntatiro,ofisa
habari wa Polisi na baadhi ya makachero wakiwa wamesimamia hali ya
usalama katika zoezi la utoaji wa mafuta ya Petroli na mafuta ya taa
katika kituo cha Total Mafiati huku kukiwa na foleni kubwa ya
magari,waendesha boda boda,watu walioshika vidumu vya lita tatu na tano.
Mwisho.
Sunday, November 4, 2012
Vyombo vya habari vyanyooshewa kidole,ni kutokana na kutangaza vyuo feki,VETA yasema matangazo yasirushwe hadi wahakikishe wamethibitisha cheti kama kweli chuuo kina usajiri,ikibi wakaangalie na majengo,asema Grace College imesajiriwa rasmi na inajulikana kitaifa
Na Thompson Mpanji,Mbeya
VYOMBO vya habari nchini vimetakiwa kuhoji uhalali wa vyuo sanjari na kupata uthibitisho wa vyeti vya usajili kutoka Chuo cha ufundi stadi (VETA),kwa wahusika wanaohitaji kufanya matangazo ya biashara katika Radio,magazeti na Luninga ili kuwasaidia wazazi na wananfunzi wasiweze kupotea na kuingia hasara ya ada na gharama nyinginezo katika vyuo visivyosajiriwa.
Mkurugenzi wa VETA kanda ya nyanda za juu kusini,Justin Rutta ametoa wito huo wakati wa mahafali ya tisa ya wahitimu wa kozi za uhazili,utalii na masuala ya Hoteli na programu ya Kompyuta katika chuo cha kanisa la Neema cha Grace College kilichopo Forest Maghorofani,jijini Mbeya.
Rutta alisema vyombo vya habari kama jicho la jamii vinapaswa kuwasaidia wazazi na wanafunzi wanaohitaji kupata elimu bora inayotambulika kitaifa hasa katika wakati huu ambapo wajanja wengi wameibuka na kuanzisha vyuo visivyo na hadhi,visivyosajiliwa lakini kutokana na ujanja ujanja vimekuwa vikitumia gharama kubwa kujitangaza katika vyombo vya habari vikubwa vinavyotambulika kwa lengo la kuwalubuni wananchi.
"Media ndiyo mhimili unaotoa taswira kwa jamii kuhusu kipi kizuri na kipi kibaya kwa hiyo pamoja na kuhitaji matangazo nawaombeni msirushe matangazo ya vyuo hadi wawaonyeshe cheti cha usajili,kwa sababu vinginevyo media ndiyo itaonekana inashirikiana na mataperi kuipotosha jamii na waulizeni wanapotoka na ikibidi nendeni mkaangalie na majengo yao,"alisema.
Alifafanua kuwa hivi karibuni Veta ilivifunga vyuo vyote ambavyo havikuwa na vigezo vya kutoa elimu na kwamba katika mchakato wa sasa wa kupita kuvikagua na kuvipatia usajiri upya Chuo cha Grace College ni miongoni mwa vyuo vilivyosajiriwa na kutambulika kitaifafa baada ya Veta kukipitisha.
"Wazazi na vijana kuweni macho na vyuo vinavyoanzishwa kitaperi katika maghofu ya nyumba na voichochoro vya kutisha,na matokeo yake mzazi anagharamia ada na gharama nyingine lakini mtoto akihitimu cheti chake chenye mapambo mazuri hakitambuliki kitaifa,chuo hakijasajiriwa na hivyo inakuwa ni hasara kwa mzazi na mtoto anapoteza mwelekeo wake wa baadaye,"alisema Rutta.
Hata hivyo Mkurugenzi huyo aliwataka wahitimu hao kwenda kuwa kielelezo cha chuo cha Grace kuwa ni kisima cha elimu bora,wanafunzi wanaofuata maadili mema,uchapakazi,upendo,ubunifu sanjari na ushirikiano katika maeneo ya kazi watakayofanikiwa kuajiriwa huku akiwataka watakaokosa nafasi wasikate tamaa na badala yake waende kujiajiri na kuondokana na utegemezi.
Awali Mkuu wa chuo cha Grace College,Sinana Otaigo Daniel alisema licha ya chuo hicho kumilikiwa na kanisa la Neema lakini kinapokea wanafunzi wa imani zote,bila ubaguzi na kwamba wanatoa pia elimu ya stadi za maisha,malezi bora, sanjari na kozi ya lugha ya kiingereza na kifaransa, na maosmo ya sekondari kwa miaka miwili na ada zao ni nafuu huku wanafunzi wa kike wakikaa katika Hosteli iliyomo ndani ya uzio wa chuo.
Mkuu huyo alisema kutokana na uhataji wa mahali salama kwa malazi na patulivu kwa kusomea hasa kwa wananfunzi wa kike,mikakati imewekwa ya kuongeza majengo mengine kwa hosteli inayotarajia kulaza wanafunzi zaidi ya 70 huku jitihada nyingine za kujenga mabweni ya wanafunzi wa kiume zikiendelea kwa kushirikiana na wazazi,kanisa na wafadhiri mbalimbali.
Ametoa wito kwa wazazi,wadau wa elimu,wafadhiri na watanzania wote wenye mapenzi mema kujitokeza kukichangia chuo hicho ili kiweze kujenga mabweni ya kutosha na hivyo wanafunzi kuweza kusoma kwa usalama bila bughudha za kidunia na hatimaye kupata viongozi bora wa baadaye na wataalamu wa taifa.
Mwisho.
VYOMBO vya habari nchini vimetakiwa kuhoji uhalali wa vyuo sanjari na kupata uthibitisho wa vyeti vya usajili kutoka Chuo cha ufundi stadi (VETA),kwa wahusika wanaohitaji kufanya matangazo ya biashara katika Radio,magazeti na Luninga ili kuwasaidia wazazi na wananfunzi wasiweze kupotea na kuingia hasara ya ada na gharama nyinginezo katika vyuo visivyosajiriwa.
Mkurugenzi wa VETA kanda ya nyanda za juu kusini,Justin Rutta ametoa wito huo wakati wa mahafali ya tisa ya wahitimu wa kozi za uhazili,utalii na masuala ya Hoteli na programu ya Kompyuta katika chuo cha kanisa la Neema cha Grace College kilichopo Forest Maghorofani,jijini Mbeya.
Rutta alisema vyombo vya habari kama jicho la jamii vinapaswa kuwasaidia wazazi na wanafunzi wanaohitaji kupata elimu bora inayotambulika kitaifa hasa katika wakati huu ambapo wajanja wengi wameibuka na kuanzisha vyuo visivyo na hadhi,visivyosajiliwa lakini kutokana na ujanja ujanja vimekuwa vikitumia gharama kubwa kujitangaza katika vyombo vya habari vikubwa vinavyotambulika kwa lengo la kuwalubuni wananchi.
"Media ndiyo mhimili unaotoa taswira kwa jamii kuhusu kipi kizuri na kipi kibaya kwa hiyo pamoja na kuhitaji matangazo nawaombeni msirushe matangazo ya vyuo hadi wawaonyeshe cheti cha usajili,kwa sababu vinginevyo media ndiyo itaonekana inashirikiana na mataperi kuipotosha jamii na waulizeni wanapotoka na ikibidi nendeni mkaangalie na majengo yao,"alisema.
Alifafanua kuwa hivi karibuni Veta ilivifunga vyuo vyote ambavyo havikuwa na vigezo vya kutoa elimu na kwamba katika mchakato wa sasa wa kupita kuvikagua na kuvipatia usajiri upya Chuo cha Grace College ni miongoni mwa vyuo vilivyosajiriwa na kutambulika kitaifafa baada ya Veta kukipitisha.
"Wazazi na vijana kuweni macho na vyuo vinavyoanzishwa kitaperi katika maghofu ya nyumba na voichochoro vya kutisha,na matokeo yake mzazi anagharamia ada na gharama nyingine lakini mtoto akihitimu cheti chake chenye mapambo mazuri hakitambuliki kitaifa,chuo hakijasajiriwa na hivyo inakuwa ni hasara kwa mzazi na mtoto anapoteza mwelekeo wake wa baadaye,"alisema Rutta.
Hata hivyo Mkurugenzi huyo aliwataka wahitimu hao kwenda kuwa kielelezo cha chuo cha Grace kuwa ni kisima cha elimu bora,wanafunzi wanaofuata maadili mema,uchapakazi,upendo,ubunifu sanjari na ushirikiano katika maeneo ya kazi watakayofanikiwa kuajiriwa huku akiwataka watakaokosa nafasi wasikate tamaa na badala yake waende kujiajiri na kuondokana na utegemezi.
Awali Mkuu wa chuo cha Grace College,Sinana Otaigo Daniel alisema licha ya chuo hicho kumilikiwa na kanisa la Neema lakini kinapokea wanafunzi wa imani zote,bila ubaguzi na kwamba wanatoa pia elimu ya stadi za maisha,malezi bora, sanjari na kozi ya lugha ya kiingereza na kifaransa, na maosmo ya sekondari kwa miaka miwili na ada zao ni nafuu huku wanafunzi wa kike wakikaa katika Hosteli iliyomo ndani ya uzio wa chuo.
Mkuu huyo alisema kutokana na uhataji wa mahali salama kwa malazi na patulivu kwa kusomea hasa kwa wananfunzi wa kike,mikakati imewekwa ya kuongeza majengo mengine kwa hosteli inayotarajia kulaza wanafunzi zaidi ya 70 huku jitihada nyingine za kujenga mabweni ya wanafunzi wa kiume zikiendelea kwa kushirikiana na wazazi,kanisa na wafadhiri mbalimbali.
Ametoa wito kwa wazazi,wadau wa elimu,wafadhiri na watanzania wote wenye mapenzi mema kujitokeza kukichangia chuo hicho ili kiweze kujenga mabweni ya kutosha na hivyo wanafunzi kuweza kusoma kwa usalama bila bughudha za kidunia na hatimaye kupata viongozi bora wa baadaye na wataalamu wa taifa.
Mwisho.
Friday, November 2, 2012
Abood lauwa Kondakta na kujeruhi 25,ni baada ya kufika Mbeya,ni la Dar Tunduma,mochwari wachanganya maiti
Na Thompson
Mpanji,Mbeya
MTU mmoja amefariki
dunia na wengine 25 kujeruhiwa baada ya Basi la abiria la kampuni ya
Abood
lililokuwa likitokea Dar es salaam kuelekea Tunduma, kugongana na lori
la
mizigo lililokuwa likielelekea Dar es salaama katika maeneo ya Sae kwa
Mbilinyi
jijini Mbeya.
Kwa mujibu
wa
mashuhuda wa tukio hilo linalodaiwa kutokea jana majira kati yasaa moja
na mbili
usiku walimtaja kwa jina moja mtu
aliyefariki dunia papo hapo kuwa ni mmoja wa
makondakta wa basi
aliyefahamika kwa jina la white na
wengine kujeruhiwa vibaya baada ya lori
lenye konteiner lenye nambari za
usajili T.616 ATQ kutaka kuikwepa basi dogo la abiria maarufu daladala
iliyogeuza ghafla maarufu kusinga katika
eneo la Mbilinyi,Sae na kujikuta likivaana na
Basi lenye nambari za usajili T545 AZE lililokuwa likielekea
Tunduma.
Mashuhuda hao
walisema baada ya dereva wa lori
kulikwepa daladala na alikutana na
basi la Abood
na hivyo kufanya jitihada za
kulikwepa na kujikuta basi hilo likiingia katika upande
wa konteiner la lori.
Kamanda wa polisi
Diwani Athuman amethibitisha kutokea kwa ajili hiyo na kwamba uchunguzi
unaendelea kujuwa chanzo cha ajali.
Muuguzi mkuu wa
Hospitali ya Rufaa Mbeya,Thomas akizungumza kwa
njia ya simu alisema walipokea
wagonjwa 25 ambapo hadi kufikia leo asubuhi wamebakia na wagonjwa wanne
na
kwamba taarifa ya jana jioni inaonesha walipokea
maiti mbili lakini inakinzana na taarifa
ya chumba cha kuhifadhia maiti ambayo inaonesha wamepokea maiti moja
iliyotokana na ajali ambapo marehemu alitambulika kwa jina la Charles
almaarufu
white,kabila mpale mkazi wa Kilimanjaro na tayari imechukuliwa na ndugu
zake na
kusafirishwa.
Mwisho.
wananchi Mbeya wafunga barabara kwa masaa sita ,ni kutokana na kugongwa watu zaidi ya 30 wakiwemo watoto wawili wa chekechea
Na Thompson Mpanji,Mbeya
MATUKIO ya ajali yameendelea kuundama Mkoa wa Mbeya
baada ya wananchi wa Kijiji cha Imezu kata ya Inyala wilaya
ya Mbeya Vijijini leo kulazimika kufunga bara bara ya Mbeya
Dar es Salaam kwa takribani saa sita baada ya kutokea ajali iliyoua
watoto wawili wa chekechea wanaokadiriwa kuwa na umri wa miaka
mitano mpaka sita.
Kamanda wa kikosi cha usalama barabarani Mkoa wa Mbeya
(RTO) Butusyo Mwambelo amewataja Watoto hao kuwa ni ,Timotheo Omary (5)
na Thadeo Braiston Malila (5) ambapo kati ya watoto hao mmoja
tayari mazishi yake yamefanyika na mwili wa mtoto mwingine utasafilishwa
kwenda kijiji cha uwanji Matamba Wilayani Makete.
Amesema kuwa tukio hilo limetokea majira ya saa
1.15 asubuhi baada ya watoto hao kugongwa na gari aina ya yenye namba
za usajili T 798 BVY tela T698 BVA lilokuwa kiendeshwa
na Dominick Mwakalundwa (34) mabibo dar e s salaam lililokuwa
likitokea Mbeya kwenda Mkoani Iringa liligonga watoto hao waliokuwa
pembeni ya bara bara wakitoka shule na kwamba aliokolewa na askari Polisi baada
ya wananchi kutaka kumshambulia..
Wakizungumza na Radio
five na matukio katika eneo la ajali
hiyo Wananchi hao, wamesema kuwa waliamua kuchukua uamuzi huo
baada ya kuchoshwa na ahadi za serikali kupitia wakala wa bara bara
za kuweka matuta katika eneo hilo la la shule ili kuepusha
ajali ambazo zimekuwa zikitokea mara kwa mara .
Bw.Michael Mashamba mkazi wa kijiji cha Imezu amesema kuwa
baada ta tukio hilo kutokea wananchi walijaa eneo la ajali na kuanza
kufunga bara bara kwa kutumia magogo na mawe ili kuzuia magari
yasipite eneo hilo kwa lengo la kushinikiza serikali kuweka matuta ili kuzuia
ajali kutokana na madai ya kufariki watu zaidi ya 30 kwa ajili katika maeneo
hayo.
Hata hivyo baada ya tukio hilo Mkuu wa Wilaya ya Mbeya
Dkt. Norman Sigalla aliwaomba wananchi kufungua bara bara
wakati serikali kwa kushirikiana na wakala wa bara bara (TAN ROADS) ikiwa
inaweka utaratibu wa kuweka matuta hayo haraka iwezekanavyo.
Aidha Sigalla ameliagiza jeshi la polisi Mkoani hapa
kuwachukulia hatua kali madereva watakoendesha magari kwa mwendo
kasi na kwamba watozwe faini na adhabu kali ambayo itawafanya wawe na
nidhamu na askari wasiwe marafiki wa madereva.
Mwisho
Subscribe to:
Posts (Atom)