Translate

Monday, November 26, 2012

TAMISEMI yawataka tanesco na mamlaka nyingine zisikwamishe ujenzi wa miradi ya Worl Bank

Na Thompson Mpanji,Mbeya

OFISI ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa  na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) imewaagiza  Mameneja wa mikoa wa tanesco,mamlaka za maji na simu kuhakikisha wanatoa ushirikiano katika kuhakikisha  miradi iliyofadhiriwa na Benki ya dunia haihujumiwi.

Aidha imesema uchgelewaji wa  miradi hiyo ambayo imetolewa fedha  na benki ya dunia zaidi ya Sh.Bil.28 katika Halamshauri saba na CDA imekuwa ikichelewa kukamilika hasa katika baadhi ya mikoa ya Dodoma,Arusha kutokana na  baadhi ya wakuu wa taasisi mbali mbali zinazohusika na miundo mbinu  kuchelewa kuondoa miundo mbinu yao kwa madai ya gharama kubwa za kuhamisha.

Rai hiyo ilitolewa  na Kaimu katibu mkuu  ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa  na Serikali za Mitaa (TAMISEMI),Jumanne Sagin wakati akifungua  mkutano wa wakurugenzi wa Halmashauri saba Nchini na  Mamlaka  ya ustawishaji Dodoma (CDA)  ambako ipo miradi hiyo (Nov,19)jana Jijini Mbeya  katika ukumbi wa Mkapa.

Sagin alisema kuwa   katika kipindi cha  miezi 15 tangu kuanza  utekelezaji wa awamu ya miradi hiyo kumekuwepo na mafanikio   makubwa katika  miradi hiyo ambayo ni pamoja na miundo mbinu ya barabara,masoko,vituo vya mabasi,madampo,utunzaji na uhifadhi wa mazingira na kwamba baadhi ya miradi ilikwamba  kutokana na ukiritimba wa baadhi ya wakuu wa taasisi.

Bw.Sagin Alisema kuwa kutokana na hali hiyo amepanga kuonana na makatibu wakuu wa wizara zinazosimamia taasisi hizo ikiwa ni pamoja na wizara ya  Nishati na Madini na Maji  kwa ajili ya kuhakikisha mameneja  wa Tanesco wa Mikoa wanakuwa na uelewa  kuhusiana na umuhimu wa kukamilika kwa  miradi hiyo.

Alisema kuwa wakuu wa  Taasisi hizo wanapaswa kujua kuwa  kukamilika kwa miradi hiyo ni ukombozi wa watanzania  na ukuaji wa  uchumi  kutokana na ukweli kuwa   kuwapo kwa  miundo mbinu hiyo kunalenga  kuondoa umaskini  miongoni mwa watanzania na kutekeleza adhama ya maisha bora kwa kila mtanzania .

Alisema kuwa  warsha hiyo ya siku mbili inalenga  kuwakumbusha wakuu wa Halmashauri na wadau wengi walioalikwa  kuona  umuhimu wa kuhakikisha wanasimamia na kutoa ushirikiano kuhakikisha  miradi hiyo inakamilika  kwa wakati uliopangwa  na kuachana na tabia ya sasa ya kila mtu  kutaka kulipwa kwa ajili ya kuhamisha miundo mbinu yake  zikiwemo nguzo.

Kaimu katibu mkuu  huyo alisema kuwa  miradi hiyo inalenga kubadili maisha ya watanzania kwa ajili ya kuhakikisha wanatumia  miundo  mbinu hiyo katika kuachana na umaskini mkubwa walio nao na kuwa na hali bora kutokana na miundo mbinu hiyo  kwa kusimamiwa na kutunzwa vema.

Aidha aliwataka wakurugenzi  wa Halmashauri hizo kutunza na kuendeleza  miradi hiyo  ili iweze kuwa  endelevu na bora na hivyo kuwasaidia watanzania  wengi kwa muda mrefu tofauti na  ilivyo sasa  ambapo  miradi mingi imekuwa  ikihujumiwa .

Mwisho

No comments:

Post a Comment