Na Thompson Mpanji,Mbeya
MLEZI Mkuu wa Chama cha vijana,wanawake wa kikristo
Tanzania(YWCA),Tawi la Mbeya,Askofu Evaristo Chengula wa kanisa Katoliki
Jimbo la Mbeya ametoa wito kwa watanzania wote wenye mapenzi mema bila
kujali itikadi za kisiasa,dini,kabila wala rangi kuchangia Kijiji cha
watoto yatima wanaoishi katika mazingira hatarishi na wenye mtindio wa
ubongo cha Kambarage ili kuweza kukamilisha ujenzi huo.
Askofu Chengula ambaye ndiye msimamizi mkuu wa YWCA amemualika
Naibu Waziri wa elimu na mafunzo ya ufundi,Philipo Mulugo (MP)
kuendesha harambee ya ujenzi wa Kijiji cha watoto yatima cha Kambarage
novemba, 24 mwaka huu.
Naibu waziri Mulugo anatarajia kuwa mgeni rasmi katika changizo
hilo litakaloambatana na maandhimisho ya miaka 20 ya YWCA,Tawi la Mbeya
hafla inayotarajia kufanyika katika ukumbi wa Mkapa,jijini Mbeya.
Askofu Chengula ataungana na walezi na wasimamizi wenzake wa chama
hicho ambao ni Askofu wa kanisa la Anglikana,nyanda za juu kusini, John
Mwela,Askofu wa kanisa la Moravian jimbo la kusini magharaibi,Alinikisa
Cheyo,Askofu wa Jimbo la Moravian jimbo la kusini, Lusekelo Mwakafwila
na Askofu wa KKKT Dayosisi ya Konde,Dkt.Islael Mwakyolile.
Akizungumza kwa niaba ya Askofu Chengula,Katibu wa YWCA Tawi la
Mbeya,Bi.Tabitha Bughali alisema watarajia mgeni rasmi,Naibu Waziri
Mulugo atafanikisha kuchangisha Sh.Mil.100 ili kuendeleza ujenzi huo kwa
awamu ulioanza tangu mwaka 2009 ambapo zaidi ya sh.Bil.2 zinahitajika
kukamilisha ujenzi huo.
Katibu huyo alisema awali Mwenyekiti wa IPP Media, Reginald Mengi
alichangia zaidi ya Sh.Mil.25 kusaidia ujenzi huo na baadhi ya wadau
wengine waliochangia ni pamoja na mmiliki wa shule za Clementine
foundation Marry Camm ambaye anatarajiwa kuwasili katika shughuli
hizo,Prof.Mwansoko,Mbunge wa viti maalum Mh.Hilda Ngoye,Prof.Mark
Mwandosya na wadau wengi.
Amewataja wageni watakaohudhuria katika changizo hilo ni Mkuu wa
Mkoa wa Mbeya,Abbas Kandoro,Wakuu wa Wilaya zote za Mkoa wa
Mbeya,wabunge,wakurugenzi wa halmashauri,wakurugenzi wa mahoteli ambapo
baadhi ya wadau tayari wameshaanza kutoa michango yao kama Wakili
Mbise,,Makasini Hotel,Mwenyekiti wa umoja wa wamiliki wa hoteli
Mahenge,Penge Hoteli,Wakili Mshokolwa na wakili Msigwa.
Bi.Bughali alisema shughuli hiyo itaendeshwa na kamati ya
maandalizi inayoongozwa na Jaji Upendo Msuya ambaye ndiye Mwenyekiti wa
kamati ya hiyo na kwamba wafanyabiashara,taasisi za serikali na binafsi
na watu mbalimbali wenye mapenzi mema wanatarajia kushiriki katika
harambee hiyo na ametoa wito kwa watanzania wote kujitokeza kuiunga
mkono YWCA katika harakati za kuwasaidia watoto yatima.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment