Translate

Monday, November 26, 2012

Tanzania itakombolewa na wanahabri

Na Thompson Mpanji,Mbeya.

IMEELEZWA kuwa Tanzania itakombolewa  endapo wanahabari wataisoma historia tangu uhuru,kuchambua na kufuatiliaji  utekelezaji wa sera sanjari na kutoa taarifa sahihi na kamili  kupitia vyombo vya habari.

Hayo yamesemwa na mwezeshaji wa mafunzo ya uchambuzi wa sera na mchanganuo wa bajeti,Robert Renatus wakati akitoa mada katika mafunzo yanayoendelea kwa wanahabari katika ukumbi wa Ukaguzi jijini Mbeya.

Alisema  wanahabari ndiyo watu pekee watakaoweza kuikomboa nchi kutokana na hali ngumu ya maisha kwa watanzania  kupitia kuzichambua sera mbalimbali na kuziandikia habari za kina ikiwemo na makala juu ya utekelezaji wake.

Mwezeshaji huyo  alitolea mfano Nchi za Ulaya na  magharibi  wamefanikiwa katika uchumi  wa mtu mmoja mmoja na taifa kwa ujumla na hatimaye kufikia maendeleo makubwa kutokana na kutumia mfumo wa SWOT Analysis kwa kuangalia uwezo,udhaifu,fursa na vitisho.

Alisema vyombo vya habari vinapaswa kutumia nafasi yake kukosoa utekelezaji mbovu wa sera  ili sekta husika ziweze kubadilika,kujisahihisha,kuwa makini na kufanya usimamizi mzuri  na hatimaye kufikia lengo lililokusudiwa la kumsaidia mtanzania.

Hata hivyo wakipitia muhtasari wa mada ya sera washiriki wa mafunzo hayo walisema wamepata ufahamu mkubwa na kubaini kuwa sera  zinatungwa ngazi za juu bila kushirikishwa wananchi na hivyo kushindwa kutekelezeka,.

Aidha katika mafunzo hayo imebainika kuwa baadhi ya wanahabari wamekuwa wakilipua katika kufanya kazi zao kwani  hawazami kwa undani katika uandishi kutokana na kutojuwa sera ikiwemo umuhimu wa vyombo vya habari katika kufuatilia na kutathmini utekelezaji wa sera.

Mwisho.

No comments:

Post a Comment