Na Thompson Mpanji,Njombe
WAKATI sakata la mgomo wa walimu likiendelea kwa nchi nzima
kuanzia leo(julai,31),Mkuu wa Mkoa wa Njombe,Capt.Mstaafu Aseri Msangi
amemshusha cheo mmoja wa watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Njombe kuanzia
leo kutokana na madai ya kuhamasisha mgomo wa walimu.
Aidha Mkuu huyo wa Mkoa amewasihi walimu wote kurejea katika maeneo yao ya kazi na kuendelea kufundisha kwani serikali imeshatangaza kuwa mgomo huo ni batili kutokana na suala hilo kuendelea kushughulikiwa mahakani.
Akitoa tamko hilo wakati wa ufunguzi wa mkutano mkuu wa kwanza wa mwaka wa wanahisa wa Benki ya wananchi Njombe,Capt.Msangi amemuagiza Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Njombe,Robert Nehatta kumshusha cheo hadi kuwa mwalimu wa kawaida wa shule ya msingi Mwenyekiti wa Chama cha walimu Tanzania(CWT),mkoani Njombe,Godfray Hambo kutokana na madai ya kuhamasisha mgomo aliodai unashughulikiwa kisheria.
Capt.Msangi amesema haiwezekani Hambo kuisaliti serikali kwa kuendelea kuhamasisha walimu kufanya mgomo ilhali naye ni kiongozi wa serikali jambo aliloagiza kuchukuliwa hatua za awali za kumshusha cheo na kwenda kufundisha katika shuel ya sekondari ama ya msingi wakati taratibu nyingine za kinidhamu ikiwemo na sheria za utumishi wa umma zikifuatiwa.
Mkuu wa Mkoa amesema Mwenyekiti huyo wa CWT Njombe hakupaswa kushika wadhifa huo kutokana na nafasi yake ya Ofisa elimu takwimu na vifaa wa Halmashauri ya Wilaya ya Njombe ambapo alitakiwa kuhamasisha walimu kufundisha badala ya kuweka kalamu chini.
Amesema endapo walimu wataendelea kugoma na hivyo kusababisha wanafunzi kukosa masomo ni sawa na kuendeleza adui mmojawapo mbaya wa ujinga kwa taifa,donda alilodai halitapona maumivu wala kufutika kovu lake kwa vizazi wanavyovijenga na kuviandaa leo.
Hata hivyo Mkuu huyo wa Mkoa wa Njombe amewashukuru walimu wote ambao kwa aslimi kubwa hawajagoma na wanaendelea na kazi na kwamba kwa Njombe mjini ni walimu wasiopungua 24 waliogoma ambapo kwa wilaya ya Makete amepokea taarifa ya shule moja wa sekondari ambayo walimu wake wamegoma ingawa hakuweza kuitaja jina na kama binafsi ama ya serikali.
Aidha Mkuu huyo wa Mkoa amewasihi walimu wote kurejea katika maeneo yao ya kazi na kuendelea kufundisha kwani serikali imeshatangaza kuwa mgomo huo ni batili kutokana na suala hilo kuendelea kushughulikiwa mahakani.
Akitoa tamko hilo wakati wa ufunguzi wa mkutano mkuu wa kwanza wa mwaka wa wanahisa wa Benki ya wananchi Njombe,Capt.Msangi amemuagiza Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Njombe,Robert Nehatta kumshusha cheo hadi kuwa mwalimu wa kawaida wa shule ya msingi Mwenyekiti wa Chama cha walimu Tanzania(CWT),mkoani Njombe,Godfray Hambo kutokana na madai ya kuhamasisha mgomo aliodai unashughulikiwa kisheria.
Capt.Msangi amesema haiwezekani Hambo kuisaliti serikali kwa kuendelea kuhamasisha walimu kufanya mgomo ilhali naye ni kiongozi wa serikali jambo aliloagiza kuchukuliwa hatua za awali za kumshusha cheo na kwenda kufundisha katika shuel ya sekondari ama ya msingi wakati taratibu nyingine za kinidhamu ikiwemo na sheria za utumishi wa umma zikifuatiwa.
Mkuu wa Mkoa amesema Mwenyekiti huyo wa CWT Njombe hakupaswa kushika wadhifa huo kutokana na nafasi yake ya Ofisa elimu takwimu na vifaa wa Halmashauri ya Wilaya ya Njombe ambapo alitakiwa kuhamasisha walimu kufundisha badala ya kuweka kalamu chini.
Amesema endapo walimu wataendelea kugoma na hivyo kusababisha wanafunzi kukosa masomo ni sawa na kuendeleza adui mmojawapo mbaya wa ujinga kwa taifa,donda alilodai halitapona maumivu wala kufutika kovu lake kwa vizazi wanavyovijenga na kuviandaa leo.
Hata hivyo Mkuu huyo wa Mkoa wa Njombe amewashukuru walimu wote ambao kwa aslimi kubwa hawajagoma na wanaendelea na kazi na kwamba kwa Njombe mjini ni walimu wasiopungua 24 waliogoma ambapo kwa wilaya ya Makete amepokea taarifa ya shule moja wa sekondari ambayo walimu wake wamegoma ingawa hakuweza kuitaja jina na kama binafsi ama ya serikali.