Baba
Mtakatifu Francisko amemteua Mheshimiwa sana Padre Vincent Mduduzi
Zungu, kutoka Shirika la Ndugu Wafrancisko Wakapuchini kuwa Askofu mpya
wa Jimbo Katoliki la Port Elizabeth, Afrika ya Kusini. Kabla ya uteuzi
huu Askofu mteule alikuwa ni msimamizi Wakapuchini kutoka Kusini mwa
Afrika, kwenye Makao Makuu ya Shirika mjini Roma.
Askofu mteule Vincent Mduduzi Zungu alizaliwa tarehe 28 Aprili 1966, Jimboni Eshowe. Baada ya majiundo na malezi ya Kipadre na kitawa, akaweka nadhiri zake za daima hapo tarehe 2 Julai 1994 na kupewa Daraja Takatifu la Upadre tarehe 8 Julai 1995.
Baada ya Upadrisho alitekeleza utume wake kama Paroko msaidizi, Mlezi wa Wanovisi, Jalim na baadaye alichaguliwa kuwa ni Padre Mkuu wa Kanda ya Wakapuchini Afrika ya Kusini.
Itakumbukwa kwamba, tangu Mwaka 2011 Jimbo la Port Elizabeth lilikuwa wazi baada ya Askofu Michael Gower Coleman kung'atuka kutoka madarakani kwa sababu za kiafya.
Askofu mteule Vincent Mduduzi Zungu alizaliwa tarehe 28 Aprili 1966, Jimboni Eshowe. Baada ya majiundo na malezi ya Kipadre na kitawa, akaweka nadhiri zake za daima hapo tarehe 2 Julai 1994 na kupewa Daraja Takatifu la Upadre tarehe 8 Julai 1995.
Baada ya Upadrisho alitekeleza utume wake kama Paroko msaidizi, Mlezi wa Wanovisi, Jalim na baadaye alichaguliwa kuwa ni Padre Mkuu wa Kanda ya Wakapuchini Afrika ya Kusini.
Itakumbukwa kwamba, tangu Mwaka 2011 Jimbo la Port Elizabeth lilikuwa wazi baada ya Askofu Michael Gower Coleman kung'atuka kutoka madarakani kwa sababu za kiafya.