Translate

Sunday, August 14, 2011

chadema yamtumia salama Mstahiki Meya wa Mbeya

Na Thompson Mpanji,Mbeya




CHAMA cha Demokrasia na maendeleo kimemtaka Katibu Mwenezi wa Chama cha Mapinduzi,Wilaya ya Mbeya mjini,Athanas Kapunga akisubiri Mahakamani ili waweze kuyatolea ushahidi madai yao kwake ya kuweka mikakati ya kukihujuma chama hicho.



Aidha Chadema imesema wataendelea kumshtakia kwa wananchi kuhusu hujuma anazoendelea kuzifanya yeye kama kiongozi wa chama kuwahujumu wananchi na hivyo kurudisha maendeleo ya Jiji la Mbeya nyuma kutokana na kuwarubuni Madiwani wa Chadema kuhamia CCM.



Hayo yamesemwa jana na Jacob Kalua Mratibu wa Operesheni Twanga kote kote, iliyohitimishwa jana katika Kata ya Iganzo,jijini Mbeya wakati akizungumza na gazeti hili.



Kalua alisema madai ya Kapunga kutishia nyau hayajaanza leo,na kwamba kitendo cha kutoa vitisho hivyo kunawaongezea kasi ya kuendelea kusema kwa waannchi yale anayoyafanya na kwamba wamemtaka atangulie mahakamani kudaifidia hizo na watamkuta na kuyaweka yote bayana.

“Kapunga hasiwashe moto ambao atashindwa kuuzima kuita vyombo vya habari asidhani tunatishika, kwa sababu tunayoyasema tunayo ushahidi nayo,tutamweka hadhrani huko mahakamni na vyombo vya habari vitayaandika,”alisema.



Kampunga ambaye pia Mstahiki Meya wa Halmashauri ya Jiji la Mbeya ameelezea dhamria yake ya kukifikisha chama hicho mahakamani kudai fidia kutokana na kile alichoelezwa kumtukana sanjari na kumtuhumu kuwanunua madiwani hasa Diwani wa Kata ya Nzovwe kupitia Chadema Ezron Mwakalobo aliyehamia CCM.



Wakati huo huo Chadema imeombwa kuwa makini na wapambe wa Chama hicho ambao wanakipaka matope Chama hicho kwa kauli chafu ambazo zinapelekea baadhi ya wananchi kukiita chama cha kihuni.



Hayo yamesemwa na mmoja wa wananchi wa Kata ya Iganzo wakati wa hitimisho la mkutano wa operesheni twanga kote kote na kudai kuwa wapambe ndiyo wanaochafua sifa ya chama ambacho kinaonekana dhahiri kina lengo la kumkomboa mtanzania.



Mwisho.