Na Thompson
Mpanji,Mbeya
MTU mmoja amefariki
dunia na wengine 25 kujeruhiwa baada ya Basi la abiria la kampuni ya
Abood
lililokuwa likitokea Dar es salaam kuelekea Tunduma, kugongana na lori
la
mizigo lililokuwa likielelekea Dar es salaama katika maeneo ya Sae kwa
Mbilinyi
jijini Mbeya.
Kwa mujibu
wa
mashuhuda wa tukio hilo linalodaiwa kutokea jana majira kati yasaa moja
na mbili
usiku walimtaja kwa jina moja mtu
aliyefariki dunia papo hapo kuwa ni mmoja wa
makondakta wa basi
aliyefahamika kwa jina la white na
wengine kujeruhiwa vibaya baada ya lori
lenye konteiner lenye nambari za
usajili T.616 ATQ kutaka kuikwepa basi dogo la abiria maarufu daladala
iliyogeuza ghafla maarufu kusinga katika
eneo la Mbilinyi,Sae na kujikuta likivaana na
Basi lenye nambari za usajili T545 AZE lililokuwa likielekea
Tunduma.
Mashuhuda hao
walisema baada ya dereva wa lori
kulikwepa daladala na alikutana na
basi la Abood
na hivyo kufanya jitihada za
kulikwepa na kujikuta basi hilo likiingia katika upande
wa konteiner la lori.
Kamanda wa polisi
Diwani Athuman amethibitisha kutokea kwa ajili hiyo na kwamba uchunguzi
unaendelea kujuwa chanzo cha ajali.
Muuguzi mkuu wa
Hospitali ya Rufaa Mbeya,Thomas akizungumza kwa
njia ya simu alisema walipokea
wagonjwa 25 ambapo hadi kufikia leo asubuhi wamebakia na wagonjwa wanne
na
kwamba taarifa ya jana jioni inaonesha walipokea
maiti mbili lakini inakinzana na taarifa
ya chumba cha kuhifadhia maiti ambayo inaonesha wamepokea maiti moja
iliyotokana na ajali ambapo marehemu alitambulika kwa jina la Charles
almaarufu
white,kabila mpale mkazi wa Kilimanjaro na tayari imechukuliwa na ndugu
zake na
kusafirishwa.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment