Translate

Friday, November 2, 2012

Abood lauwa Kondakta na kujeruhi 25,ni baada ya kufika Mbeya,ni la Dar Tunduma,mochwari wachanganya maiti

Na Thompson Mpanji,Mbeya

MTU mmoja amefariki dunia na wengine 25 kujeruhiwa baada ya Basi la abiria la kampuni ya Abood lililokuwa likitokea Dar es salaam kuelekea Tunduma, kugongana na lori la mizigo lililokuwa likielelekea Dar es salaama katika maeneo ya Sae kwa Mbilinyi jijini Mbeya.
 
Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo linalodaiwa kutokea jana majira kati yasaa moja na mbili usiku walimtaja  kwa jina moja mtu  aliyefariki dunia papo hapo  kuwa ni mmoja wa makondakta wa basi aliyefahamika kwa jina la  white na wengine kujeruhiwa vibaya baada ya lori  lenye konteiner lenye  nambari za usajili T.616 ATQ kutaka kuikwepa basi dogo la abiria maarufu daladala iliyogeuza ghafla  maarufu kusinga katika eneo la Mbilinyi,Sae na kujikuta likivaana na  Basi lenye nambari za usajili T545 AZE lililokuwa likielekea Tunduma.
 
Mashuhuda hao walisema  baada ya dereva wa lori kulikwepa daladala na   alikutana na  basi la Abood  na hivyo  kufanya jitihada za kulikwepa na kujikuta basi hilo likiingia katika  upande wa konteiner la lori.
 
Kamanda wa polisi Diwani Athuman amethibitisha kutokea kwa ajili hiyo na kwamba uchunguzi unaendelea kujuwa chanzo cha ajali.
 
Muuguzi mkuu wa Hospitali ya Rufaa Mbeya,Thomas  akizungumza kwa njia ya simu alisema walipokea wagonjwa 25 ambapo hadi kufikia leo asubuhi wamebakia na wagonjwa wanne na kwamba  taarifa ya jana jioni inaonesha walipokea maiti mbili lakini inakinzana na  taarifa ya chumba cha kuhifadhia maiti ambayo inaonesha wamepokea maiti moja iliyotokana na ajali ambapo marehemu alitambulika kwa jina la Charles almaarufu white,kabila mpale mkazi wa Kilimanjaro na tayari imechukuliwa na ndugu zake na kusafirishwa.
 
Mwisho.

No comments:

Post a Comment