Translate

Sunday, November 4, 2012

Vyombo vya habari vyanyooshewa kidole,ni kutokana na kutangaza vyuo feki,VETA yasema matangazo yasirushwe hadi wahakikishe wamethibitisha cheti kama kweli chuuo kina usajiri,ikibi wakaangalie na majengo,asema Grace College imesajiriwa rasmi na inajulikana kitaifa

Na Thompson Mpanji,Mbeya




VYOMBO vya habari nchini vimetakiwa kuhoji uhalali wa vyuo sanjari na kupata uthibitisho wa vyeti vya usajili kutoka Chuo cha ufundi stadi (VETA),kwa wahusika wanaohitaji kufanya matangazo ya biashara katika Radio,magazeti na Luninga ili kuwasaidia wazazi na wananfunzi wasiweze kupotea na kuingia hasara ya ada na gharama nyinginezo katika vyuo visivyosajiriwa.



Mkurugenzi wa VETA kanda ya nyanda za juu kusini,Justin Rutta ametoa wito huo wakati wa mahafali ya tisa ya wahitimu wa kozi za uhazili,utalii na masuala ya Hoteli na programu ya Kompyuta katika chuo cha kanisa la Neema cha Grace College kilichopo Forest Maghorofani,jijini Mbeya.



Rutta alisema vyombo vya habari kama jicho la jamii vinapaswa kuwasaidia wazazi na wanafunzi wanaohitaji kupata elimu bora inayotambulika kitaifa hasa katika wakati huu ambapo wajanja wengi wameibuka na kuanzisha vyuo visivyo na hadhi,visivyosajiliwa lakini kutokana na ujanja ujanja vimekuwa vikitumia gharama kubwa kujitangaza katika vyombo vya habari vikubwa vinavyotambulika kwa lengo la kuwalubuni wananchi.



"Media ndiyo mhimili unaotoa taswira kwa jamii kuhusu kipi kizuri na kipi kibaya kwa hiyo pamoja na kuhitaji matangazo nawaombeni msirushe matangazo ya vyuo hadi wawaonyeshe cheti cha usajili,kwa sababu vinginevyo media ndiyo itaonekana inashirikiana na mataperi kuipotosha jamii na waulizeni wanapotoka na ikibidi nendeni mkaangalie na majengo yao,"alisema.



Alifafanua kuwa hivi karibuni Veta ilivifunga vyuo vyote ambavyo havikuwa na vigezo vya kutoa elimu na kwamba katika mchakato wa sasa wa kupita kuvikagua na kuvipatia usajiri upya Chuo cha Grace College ni miongoni mwa vyuo vilivyosajiriwa na kutambulika kitaifafa baada ya Veta kukipitisha.



"Wazazi na vijana kuweni macho na vyuo vinavyoanzishwa kitaperi katika maghofu ya nyumba na voichochoro vya kutisha,na matokeo yake mzazi anagharamia ada na gharama nyingine lakini mtoto akihitimu cheti chake chenye mapambo mazuri hakitambuliki kitaifa,chuo hakijasajiriwa na hivyo inakuwa ni hasara kwa mzazi na mtoto anapoteza mwelekeo wake wa baadaye,"alisema Rutta.



Hata hivyo Mkurugenzi huyo aliwataka wahitimu hao kwenda kuwa kielelezo cha chuo cha Grace kuwa ni kisima cha elimu bora,wanafunzi wanaofuata maadili mema,uchapakazi,upendo,ubunifu sanjari na ushirikiano katika maeneo ya kazi watakayofanikiwa kuajiriwa huku akiwataka watakaokosa nafasi wasikate tamaa na badala yake waende kujiajiri na kuondokana na utegemezi.



Awali Mkuu wa chuo cha Grace College,Sinana Otaigo Daniel alisema licha ya chuo hicho kumilikiwa na kanisa la Neema lakini kinapokea wanafunzi wa imani zote,bila ubaguzi na kwamba wanatoa pia elimu ya stadi za maisha,malezi bora, sanjari na kozi ya lugha ya kiingereza na kifaransa, na maosmo ya sekondari kwa miaka miwili na ada zao ni nafuu huku wanafunzi wa kike wakikaa katika Hosteli iliyomo ndani ya uzio wa chuo.



Mkuu huyo alisema kutokana na uhataji wa mahali salama kwa malazi na patulivu kwa kusomea hasa kwa wananfunzi wa kike,mikakati imewekwa ya kuongeza majengo mengine kwa hosteli inayotarajia kulaza wanafunzi zaidi ya 70 huku jitihada nyingine za kujenga mabweni ya wanafunzi wa kiume zikiendelea kwa kushirikiana na wazazi,kanisa na wafadhiri mbalimbali.



Ametoa wito kwa wazazi,wadau wa elimu,wafadhiri na watanzania wote wenye mapenzi mema kujitokeza kukichangia chuo hicho ili kiweze kujenga mabweni ya kutosha na hivyo wanafunzi kuweza kusoma kwa usalama bila bughudha za kidunia na hatimaye kupata viongozi bora wa baadaye na wataalamu wa taifa.



Mwisho.

No comments:

Post a Comment