Translate

Sunday, January 12, 2014

mauaji mbeya



TAARIFA YA JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA KWA VYOMBO VYA HABARI
“PRESS RELEASE”TAREHE 09.01. 2014.

WILAYA YA ILEJE – MAUAJI.

WATU wawili wakazi wa Kitongoji cha Lupungu,Kijiji cha Ikinga,Kata ya Ikinga,Tarafa ya Bundali,Wilaya ya Ileje,mkoani Mbeya wanashikiliwa na Jeshi la polisi  kwa tuhuma za mauaji.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Kamishna msaidizi Mwandamizi wa polisi,Ahmed Msangi amesema watuhumiwa hao Laison Mshani(55), na Queen Minga(40) walitenda kosa hilo Januari,7,2014  baada ya kumkata kwa mapanga kichwani na sehemu mbalimbali  za mwili wake  Francis Mshani(30) kisha kumchoma moto kuanzia kwenye magoti hadi kichwani.

Amefafanua kuwa marehemu  alitoka kifungoni  gerezani  mwezi Novemba,2013 kwa kosa la kumjeruhi mtalaka  wake na kwamba chanzo cha mauaji hayo bado hakijafahamika.

Hata hivyo Kamanda ameendelea kutoa wito  kwa jamii kuacha tabia  ya kujichukulia sheria mkononi kwani madhara yake ni makubwa  na badala yake watumie njia za busara katika kutatua migogoro ya kifamilia na kijamii kwa ujumla.

Wakati huo huo,Mtu mmoja  aliyefahamika kwa jina la Dastan Gama(38),Mfanyabiashara Mkazi wa Songea,mkoani Ruvuma anashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa kosa la kukutwa na vipodozi vilivyopigwa marufuku  na serikali.

Kamanda msangi amesema mtuhumiwa  alikamatwa Januari,8,2014 majira ya saa 10.30 mchana  huko maeneo ya Ifisi,Kata ya Utengule,Tarafa ya usongwe,Wilaya ya Mbeya vijijini  ambapo askari polisi wakiwa katika doria  walifanikiwa kumkata Dastan  akiwa na  Sabuni boksi mbili,Carolight ndogo dazani nne,Epictem 10,Extra Crela dazani mbili,Diplozoni dazani 17,Movey dazani nne,soft touch dazani nne na Lemovet boksi tatu.
Mwisho.

No comments:

Post a Comment