Translate

Wednesday, October 31, 2012

Tazara saccos kujenga Hosteli ya kisasa

Na Thompson Mpanji,Mbeya

CHAMA cha kuweka na kukopa cha Tazara Saccos Mkoani Mbeya kinatarajia kujenga hosteli kubwa ya kisasa ili kuachana na dhana ya kuwa tegemezi kutoka kwenye taasisi za kibenki na kuwa mradi huo mkubwa utaweza kusaidia chama kujitegemea chenyewe badala ya kutegemea zaidi kukopa katika benki hizo.



Hatua ya kuwa na ujenzi huo wa hosteli imekuja baada ya uongozi wa Tazara kwa kushirikiana na wanachama kuamua kwa pamoja kuwa na kitega uchumi chao wenyewe ambacho kitasababisha kuacha kukopa katika mabenki kwani hosteli hiyo itakapokuwa imekamilika hakutakuwa na sababu ya kukimbilia tena katika mabenki badala yake watatumia kitega uchumi chao kukuza mtaji wa chama.

Akizungumza katika Mkutano Mkuu wa Chama hicho wa kumi na tisa toka kuanzishwa kwake, Mwenyekiti wa Tazara Saccos Mkoani Mbeya Ambrose Shayo amesema kwamba kuanzia wameona kuwa mradi pekee ambao wanaweza kuanza nao ni hosteli kutokana na vyuo vingi kuanzishwa Mkoani hapa na ongozeko la wananchi kuwa kubwa.


Shayo amesema kuwa mradi huo utagarimu kiasi cha shilingi bilioni. 2 na kuwa fedha hizo zitapatikana kwa kila mwanachama kuchangia hisa zake ambazo ni shilingi 3,0000 ambazo watatoa kwa kila mwezi na kwamba mbali ya hisa za wachama pia chama kama kitakuwa kinanunua hisa za mil.8 kila ujenzi huo unatarajio kukamilika ndani ya miaka mitano ijayo sababu uwanja upo tayari ni kuanza tu mchakato wa kutafuta fedha mapema kutoka taasisi zingine kwa kutumia njia mbali mbali.

Aidha Mwenyekiti huyo amesema mwisho wa utekelezaji wa mpango huo ni kuweza kuwekeza na kuanza kujitegemea wenyewe badala ya kutegemea mabenki zaidi ambazo wamekuwa wakitumia kwa muda mrefu.
Mwiisho.

No comments:

Post a Comment