Translate

Saturday, October 27, 2012

Mujata yaiasa jamii kushirikiana na Polisi

Na Thompson Mpanji,Mbeya




CHAMA cha Muungano wa Jamii Tanzania (MUJATA) kimewataka wanajamii wote kwa ujumla kushirikiana na Jeshi la Polisi ili kukomesha maovu yanayotokea kwenye jamii mbali mbali nchini.



Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa Mujata kanda,Shayo Soja katika kongamano la Chama hicho ambalo limehusisha viongozi mbalimbali na wajumbe kutoka mikoa mbalimbali ya nyanda za juu kusini ikiwepo Iringa,Njombe,Ruvuma,Katavi pamoja na Mbeya.



Akizindua kongamano hilo katika ukumbi wa Royal College of Tanzania tawi la Mbeya,kamanda wa polisi mkoani hapa Diwani Athuman amesema jeshi la polisi lipo kwa ajili ya kushirikiana na Mujata ili kuhakikisha kuwa maovu yote yanayotendeka katika jamii yanakomeshwa.



Diwani amewaomba Mujata kutoa ushirikiaano wa hali na mali kwa jeshi ili kuweza kutokomeza kabisa kila aina ya uovu na amewashukuru kwa kutoa taarifa kwa jeshi la polisi katika vitendo vya ukatili vilivyowahi kujitokeza hapo awali kwa kuzika watu wakiwa hai.



Alisema vitendo vya ukatili,unyanyasaji wa kijinsia pamoja na maovu yatendekayo kwenye jamii yatakomeshwa endapo jamii haitakuwa tayari kufumbia macho vitendo hivyo ikiwa ni pamoja na kutoa taarifa polisi.



Wakati huo huo,Chama hicho kimefanya uchaguzi wa kuteuwa viongozi katika nafasi mbalimbali za Chama ikiwa ni pamoja na kumpata Mwenyekiti wa pamoja na makamu wake.



Uchaguzi huo ambao umesimamiwa na kamati ya uchaguzi ya Mujata ambapo Mwenyekiti aliyechaguliwa ni Soja pamoja na makamu wake Christina Joel hao wote kwa pamoja wamekishukuru chama kwa kuwaamini kwa mara nyingine.



Mwisho.

No comments:

Post a Comment