Translate

Wednesday, October 31, 2012

Ajinyonga kwa waya wa simu baada ya kumpiga mkewe

Na Thompson Mpanji,Mbeya

MKAZI wa Iziwa Mkoani Mbeya Mbwiga Mwalungwe(60), amefariki dunia baada ya kujinyonga nyumbani kwake kwa kutumia waya wa simu Oktoba 24 mwaka huu baada ya marehemu kumpiga mkewe.


Inadaiwa marehemu alimpiga mkewe aitwaye Taines Mbwiga(45) Oktoba 23 hali iliyompelekea kukimbizwa katika Hospitali ya Rufaa Jijini hapa ambapo alipewa PF3 kwa ajili ya kutibiwa na kulazimu kulazwa hospitalini hapo.

Kutokana na tukio la baada ya mkewe kulazwa hospitalini, Jeshi la Polisi lilianza kufuatilia tukio hilo ndipo marehemu alipogundua kuwa anakabiliwa na mkono wa sheria aliamua kuchukua uamuzi mgumu kwa kuchukua waya wa simu majira ya saa 4 kamili asubuhi Oktoba 24, kisha kujinyonga nyumbani kwake.


Aidha polisi walifika eneo la tukio majira ya saa 6:00 mchana na kuuchukua mwili wa marehemu hadi hospitali ya rufaa kwa ajili ya uchunguzi zaidi na kwamba hali ya mwanamke huyo inaendelea vema ambapo ameruhusiwa kutoka hospitalini Oktoba 2 na mwili wa marehemu umehifadhiwa katika hospitali hiyo.

Akizungumza na Mwandishi wa habari hizi,kuhusiana na tukio hilo Balozi wa mtaa huo Chaina Juma amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba amewaachia jeshi la polisi kufanya uchunguzi ili kupata kiini hasa cha Mwalungwe kujiua kwa kujinyonga na kumuacha mkewe akiendelea kuugua hospitali.


Mwisho.



No comments:

Post a Comment