Translate

Saturday, October 27, 2012

Thomas Nyimbo awashangaa watanzania kumshangaa waziri Mulugo




MWANASIASA mkongwe nchini,Thomas Nyimbo amesema yaliyotokea kwa Naibu Waziri wa Elimu na ufundi stadi,Philipo Mulugo katika mkutano nchini Afrika ya kusini siyo ya kushangaza katika serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwani hiyo ndiyo taswari ya viongozi wetu.



Nyimbo ambaye amewahi kuwa Mbunge wa Jimbo la Njombe,mwasisi wa TANU na Chama cha Mapinduzi (CCM) na mlezi wa CHADEMA ameyasema hayo leo katika mkutano wake na wanahabari katika Hoteli ya Mount Livingstone,jijini hapa na kuongeza kuwa tukio la Naibu waziri Mulugo kuzungumza mambo ambayo hayaendani na nafasi yake siyo jambo jipya kwake kutokana na nchi inavyoendeshwa.



Alisema hiyo ni taswira tosha kuwa asilimia kubwa ya Viongozi wa nchi wanaoteuliwa hawana sifa ya uongozi bali wanapewa nafasi hizo kama zawadi kutokana na kufanikisha jambo fulani hali itakayoendelea kuwatafuna watanzania kutokana na mfumo na utaratibu huo.



"Hili jambo ni jipya kwa watu wasiojuwa utaratibu na mfumo mzima wa nchi,kwagu mimi siyo jipya...nimeambiwa nilete dereva nami badala yake nampeleka 'Tandiboi' unategemea nini ndiyo manaa nchi haiendi,"alisema.



Aliongeza kwa kusema hakuna sababu ya kumlaumu Mulugo kwa kuonekana kushindwa kuzungumza lugha ya kiingereza vizuri sanjari na kutoijuwa historia ya Tanzania kwa sababu wapo wengine ambao wangeshindwa kabisa hata kuongea na kuishia mabubu.



"Wanamlaumu nini huyo Waziri hii ndiyo hali halisi,afadhari hata yeye aliyejitahidi hata kuzungumza na mmesikia,wapo wengine wanaweza kunyama kwa kushindwa kuzungumza na tusingejuwa,aibu hii tuendelee kubeba,kwa sababu watamlinda,"alisema.



Baadhi ya wananchi wa jimbo la Songwe ambao ndiye Mbunge wao walisema kuwa tukio hilo limepokelewa kwa maoni tofauti kutokana na kushindwa kuamini kile kilichomtokea Mbunge wao Mulugo.



"Tunamsubiri aje atuambie,ni nini kilichomsibu,ndiyo hali halisi ya uwezo wake ama alikumbwa na kitu ambacho hatujakijuwa ni nini...lakini ili ni mojawapo ya nyundo ya kummaliza kisiasa katika uchaguzi mkuu mwaka 2015,"alisema mmoja wa wananchi hao.



Mkazi wa Kijiji cha Mkwajuni wilayani Chunya (jina limehifadhiwa ) alisema yeye ni mwanachama wa CHADEMA lakini amempongeza Naibu waziri kwa kutoa nafasi na matumiani makubwa kwa upinzani kushindwa katika uchaguzi mkuu unaokuja kutokana na kuonesha uwezo wake mdogo wa ufahamu na hivyo kushindwa kuwaletea maendeleo.



"Kama Naibu waziri wa elimu katika wizara nyeti kama hiyo haelewi hata historia ya nchi yake ataifanyia nini Tanzania na hawezi kutusaidia hata wapiga kura wake katika maendeleo kwa sababu uwezo na upeo wake unaonekana ni mdogo,na kibaya zaidi amekuwa akionekana kutumia mabavu na vitisho vingine kuongoza,"alisema.



Alisema kuwa Mulugo alifikia hatua ya kupeleka viti vya walemavu zaidi ya 200 akisema amenunua yeye pamoja na msaada wa wa visima vya maji ya kunywa vilivyofadhiriwa na mfanyabishara maarufu nchini Sabodo akidai alitoa yeye jambo linaloonesha kuwa haijapangi katika kuzungumza.



"Amefikia hatua anawaagiza watendaji wa vijiji na Kata kuwa hataki vyama vya siasa katika jimbo lake,kweli anaelewa maana ya Demokrasia?,na kila anapopita anatoa vitisho hata kwa walimu,nchi haiwezi kuongozwa kwa mtindo wa mabavu akama anavyotaka yeye,alisema.



Mwisho.

No comments:

Post a Comment