Translate

Sunday, October 28, 2012

CHADEMA yapata pigo,yadaiwa kuhusika kwa asilimia 50 mauaji ya Mwangosi

Na Thompson Mpanji,Mbeya




CHAMA cha Demokrasia na maendeleo nchini(CHADEMA) kimepata pigo kubwa kutokana na kujiondoa uanachama kwa aliyekuwa mmojawapo wa wafadhiri na walezi wakuu wa chama hicho huku akidai hakuna lolote jipya zaidi ya viongozi kuangalia kuchumia tumboni.



Aidha Mlezi huyo ambaye ni mwanasiasa machachari na mkongwe,muasisi wa TANU na Chama cha Mapinduzi na amewahi kuwa Mbunge wa Njombe kupitia CCM kwa miaka 10 ,Thomas Nyimbo licha ya kutangaza rasmi kujiondoa uanachama wa Chadema kwa madai ya kupumzika siasa za vyama na kwamba watu wanaopaswa kutuhumiwa na mauaji ya mtoto wake,rafiki yake Mwanahabari Daud Mwangosi ni Polisi kwa asilimia 50 na CHadema asilimia 50.



“Ninajihudhuru na mambo ya chama nimeona hakuna jipya katika vyama hivi siyo CCM wala Chadema zaidi ya kila mmoja kuangalia malahi binafsi na siyo wawafanyie nini watanzania…ukisema wewe ni CCM damu na Nyerere je?,Viongozi wa vyama hawaambiliki,hawasikii,unakwenda kufungua tawi la Nyororo nililolifunguwa mimi Nyimbo miezi miwili,mitatu iliyopita maana yake nini, ”alisema.



Aliongeza,”sintojishughulisha na siasa nina resign Party Politics nilizaliwa Kiongozi nitabaki kuwa kiongozi wa wananchi,kama kuna jambo nitajitokeza kama kiongozi wa wananchi kukemea kwa sababu tukiendeleza u-darling darling tutaipeleka nchi pabaya,kazi ya siasa nitaifanya nje ya vyama ambapo Mu kwanza chama baadaye…nitaifanya katika church forum nitatumia legal forum.”



Alisema utafiti wake alioufanya akiwepo katika vyama vya siasa tangu alipokuwa TANU na baadaye CCM, alipoanzisha Chama cha Pona, na kuhamia Chadema ni kwamba Viongozi walio wengi wamejawa tamaa ya kujitajirisha jambo ambalo halitasaidia chochote hata kama kutakuwepo na mabadaliko kama ya (Movement for change-M4C).



Nyimbo alisema ni makosa kujenga dhana katika vichwa vya watanzania kuwa maendeleo na maisha bora kwa kila mtanzania yataletwa kwa njia ya mabadiliko M4C,haitasaidia kuondoa CCM kuleta Chadema,ondoa hiki weak kile na matokeo yake wanaweza kuwa kama senene na kuanza kujitafuna wenyewe.



Alisema pamoja na kujiondoa Chadema kama alivyowahi kujiondoa CCM na kuendelea kubaki na kadi za Umoja wa vijana wa TANU(TANU Youth league) na baadaye CCM ataendelea kubaki na kadi za chama kwa sababu ni mali yake na haki yake ya msingi na hatathubutu kukitukana chama chochote zaidi ya kukemea maovu yatakayobainika.



Alisema Chama cha Mapinduzi kinavurugu amani kutokana na kutowadhibiti watendaji wa vijiji na Kata wanaoendelea kuonekana miungu watu kwa kufikia hatua ya kuwavua nguo wanakijiji kwa kukosa mchango wa maendeleo na hivyo kuifanya CCM kuchukiwa kwa kitendo cha mtu mmoja,ihamke na isijiweke pembeni katika mamlaka iliyoomba kuwatumikia wananchi.



Alikadhalika alitolea mfano chama cha Chadema kuwa utaratibu wa kuitisha mikutano kwa ghafla bila kufuata mpangilio huku kukiwepo na matamshi kama “katika mkutano wa leo Tutapasua jipu”,tuandalieni ikulu 2015 nayo itaweza kuchochea uvunjifu wa amani kwa sababu inaajenga watu kuwa na uhakika wa kushinda na endapo hawatashinda wataleta vurugu.



Mwanasiasa huyo mkongwe alitolea mfano kwa Rais wa Zambia Chiluba ambaye alikuwa Mwenyekiti wa chama cha MMD kutoka chama cha wafanyakazi wa Labour Movement kuwa alitumia Mobe justice ambapo wananci walimbeba kupeleka Ikulu lakini ndiyo hao hao waliompeleka Mahakamani baada ya kushindwa kutekeleza aliyoahidi.



“Juzi tumeshuhudia nguvu ya umma Sumbawanga iliyovyoleta athari kwa watu kuchoma moto matrekta bila sababu za msingi,nchi hii ina watanzania zaidi ya Mil.40 lakini wanasiasa hawafikii hata asilimia 10,kwa hiyo tuangalie maslahi ya watanzania na siyo ya watu wachache,ndani ya vyama siyo CCM wala Chadema ukiwashauri hiki wanafanya kile,”alisema.



Nyimbo alisema kwa muda wa miaka miwili tangu aingie chadema mwaka 2012 anaifahamu vizuri nao wanamfahamu vyema kama ilivyo kwa CCM na hatimaye kufikia hatua ya kujibizana na akina mkapa na Sumaye kwa ajili ya masuala ya umeme ambayo leo amempongeza Waziri wa Nishati na madini Prof.Mhongo amekuja kuyasema na kuyashughulikia.



“Wapo watu wanasema leo makanisa yanachomwa moto Rais hasemi mnataka aseme nini wakati IGP yupo na DI yupo?,kwa sababu Rais anaweza kuwa kuwa kipofu ama bubu lakini hao wanaweza kuiendesha nchi bila tatizo,angekuwa kila kitu anasema mngesema Rais Mlopokaji,mnaiuwa nchi vijana vyma vinatupeleka pabaya,tayari wamekufa watu 20 kwa ajili ya mikutano mseme sasa inatosha,”alisema.



Alifafanua kuwa kifo cha Mwangosi kisingetokea kama Viongozi wa Chadema wangefuata utaratibu wa kuandaa mikutano mapema na kuwasiliana na Viongozi wa Iringa na Nyororo.



“Uongozi wa Chadema unaweza kutoka makao makuu na kuja mahali bila kibali wala taarifa kwa viongozi wa maeneo husika na kuanza kutafuta kibali kuitisha mikutano huo si utaratibu,unasababisha kuhatarisha amani na ndiyo yaliyotokea Nyororo,mimi nilishalifunguwa lile tawi alipouawa Mwangosi miezi miwili mitatu iliyopita ,sasa akina Dkt.Slaa walikuja kufungua nini tena,na kibaya zaidi hata sisi Vingozi wa Iringa hatukuwa na taarifa,nasema Chadema wanahusika kwa asilimia 50,kifo cha Mwangosi,”alisema.



Alielezea kuhusu tume ya nchi kuwa angeteuliwa yeye angekataa kwa sababu wamekwenda kuchunguza ama kuthibitisha namna Nchimbi,Jeshi na wengine walivyoshiriki kufanya mauaji.



Nyimbo alisema ili nchi iweze kuendelea na kupata viongozi bora siyo bora viongozi wanaowazia matumbo kama ilivyo kwa Viongozi walio wengi wa vyama ni lazima katiba mpya ipitishe mbomgea urais binafsi ili aweze kuja kupata fursa ya kuwachagua mawaziri wasiotokana na bunge,kuwepo na sera ya taifa ya maendeleo kama ilivyo Marekani,utaifa kwanza vyama baadaye.



“Mimi nilibuni bango langu la kuogombea ubunge ukiliangalia mimi ndiye mtu wa kwaza kunadi sera ya MTU KWANZA VYAMA BAADAYE na ndiyo maana ukiliangalia bango langu bendera ya Chadema imekuwa ndogo na bendera ya taifa imebeba nafasi kubwa na nilisema nimedhaminiwa na Chadema,pia tunaomba matamshi yaangaliwe kwani ni hatari kuvuka mto kama haujafika na kuangalia,”alihitimisha.



Mwisho.



















No comments:

Post a Comment