Translate

Wednesday, October 31, 2012

Mtoto wa miaka nane ajinyonga

MTOTO  mdogo aliyefahamika kwa jina la Calvin Patrick mwenye umri wa miaka nane  mwanafunzi wa darasa la tatu katika shule ya msingi Iwambi ,Mkazi wa Mtaa wa Ivwanga Kata ya Iwambi Mkoani Mbeya amefariki dunia baada ya kujinyonga kwa kutumia kamba ya viatu nje ya nyumba yao.
Tukio la kujinyonga kwa mtoto Patrick limetokea majira ya saa 5.00 octobar 27 mwaka huu asubuhi katika mtaa wa Ivwanga wakati wazazi wa mtoto huyo walipokuwa wametoka nyumbani hapo na ndipo mtoto huyo alipochukua jukumu hilo zito na la aina yake.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, Mwenyekiti wa mtaa huo Chonde Calisto alisema wakati tukio hilo linatokea Baba mzazi wa mtoto huyo Patrick Mwakapalila alikuwa ametoka na kaka mkubwa wa marehemu aitwaye Joshua kuelekea mjini kutafuta mahitaji na kwamba baada ya tukio hilo baba mzazi wa mtoto huyo alipigiwa simu na kutakiwa kurudi haraka nyumbani.

Amesema kuwa baada ya tukio baba mzazi wa mtoto huyo alipigiwa simu ili arudi nyumbani kuona tatizo lililotokea kwa mtoto wake na kwamba baada ya kufika alikuta mwanae huyo mdogo akiwa nje ya nyumba yao akiwa ananing'inia juu akiwa amejinyonga kwa kamba ya viatu"alisema.

Hata hivyo mama mzazi wa mtoto huyo nae hakuwepo nyumbani hapo kwani alikuwa katika shughuli zake za kibiashara ambako anauza duka la mahitaji mbali mbali ya nyumbani eneo la Iwambi ambako jirani na nyumbani.

Chonde amesema mpaka sasa bado hakijafahamika chanzo cha kujinyonga kwa mtoto huyo na polisi walifika eneo la tukio na kuchukua mwili wa marehemu kwa uchunguzi zaidi ili ndugu waweze kukabidhiwa mara baada ya uchunguzi huo kukamilika .


Mwisho.

No comments:

Post a Comment