Na Thompson
Mpanji,Mbeya
KIJANA anayedai kuwa ni mdogo wa msanii maarufu wa Bongo
Movie marehemu ‘The Great’Steven Kanumba
aliyejitambulisha kwa jina la Lameck
Ngogo(20),Mkazi Sokomatola,jijini Mbeya ameibuka na kudai kuwa marehemu Kanumba
ni Kaka yake aliyezaliwa naye kwa
Baba lakini Mama tofauti.
‘Kanumba’ mdogo huyo ameibuka asubuhi ya Januari,3,2013
katika mkutano wa waandishi wa habari na
viongozi na wanachama wa Chama cha NCCR waliofukuzwa kutoka Chama cha
Demokrasia na maendeleo (CHADEMA),jijini Mbeya katika ukumbi wa Baa ya Double J,Sinde.
Ilikuwa kama ‘movie’ baada ya kijana huyo mwenye uso wa
upole,tabasamu kama la marehemu Kanumba alipoingia na mwandishi wa habari wa
kujitegemea,Samwel Mamba,Mkazi wa wilayani Mbozi na kutulia kama msikilizaji ama naye
Mwanahabari lakini macho ya wanahabari wengi yaligonga na kutuwa katika sura
yake huku wakiwa na maswali mengi ya
kujiuliza wakisubiri mkutano huo umalizike mapema na kuanza kumhoji mwandishi
Samwel kulikoni kijana huyo.
Mara baada ya kumalizika kwa kikao hicho Samwel huku akiwa
ameshabaini kiu ya wanahabari alianza kwa kusema,”jamani nimewaletea mdogo wake
kanumba…,nimemuibua kutoka katika guest ya Eden iliyopo maeneo ya uhindini
jijini Mbeya ndiko anakofanyakazi.”
Aliendelea kwa kusema,” mimi sina la kuongea zaidi ya kumsikiliza yeye asimulie historia yake
maana mimi nililala katika nyumba hiyo ya kulala wageni leo(januari,3) na baada
ya kumuona nilishtuka sana nilipomwita na kumuuliza alinielezea historia yake
iliyonisababisha kumuombea ruhusa kwa wakubwa wake ili nije naye hapa leo
nikijuwa tutakutana waandishi katika press conference hii.”
Kijana lameck hauwezi kumsingizia kwa zile hulka za marehemu Star wa Bongo
Movie Steve Kanumba ambapo alianza kusimulia historia yake kuwa yeye ni mtoto wa kwanza wa Mama yake Alatwingisya Ngogo na
kwamba hilo jina analolitumia la Ngogo
ni la Babu yake mzaa mama yake.
Alisema Mama yake ni
mkazi wa Uwanji,Kata ya Mlondo,Wilaya ya Makete mkoani Njombe na kwamba aliwahi
kuchukuliwa na Mama yake Mkubwa aliyemtaja kwa jina moja la Jane(Dada yake) na
kuishi naye mkoani Shinyanga miaka 20 iliyopita ambapo alibahatika kupata uja uzito wa yeye(Lameck) na kutokana na Mama
yake mkubwa kuchukia hali hiyo aliamua kumfukuza na kumrejesha nyumbani uwanji
anapoishi hadi leo.
Lameck alisema kuwa Mama yake mkubwa huyo ambaye anaishi
hadi leo mkoani Shinyanga hakumuuliza Mama yake kuwa mimba hiyo alipewa na nani
zaidi ya kumrudisha nyumbani hadi alipojifungua na kuendelea na maisha hadi
alipokuja kuolewa na kuendelea
kuishi na Mume wake hadi leo.
“Lakini nilipokuwa nikiendelea kukua na kupata ufahamu watu
walikuwa wakiniambia kuwa huyo siyo Baba yangu mzazi licha ya mama kunieleza
kuwa ndiyo baba yangu mzazi lakini baada ya kumdadisi sana aliamua kunieleza kuwa ni kweli baba yangu
alinikataa tangu nikiwa tumboni huko Shinyanga ambaye ni Baba yake msanii
kanumba kabla hajafa,”alisema.
“Baadaye nililelewa na Bibi yangu anaitwa Nilang’ilwa na
niliendelea na masomo na kuishia kidato cha pili katika shule ya Sekondari ya
Mlondwe na hivyo nikaja kwa Mjomba wangu
Uyole kumsaidia kuuza viatu vya mitumba na baadaye nikatafuta kazi
nikapata katika nyumba ya kulala wageni
ya Eden iliyopo Uhindini ambako huyu
Mwandishi alinikuta na kunihoji baada ya mimi kumuona amebeba mabegi ya camera
na kuanza kumsimulia historia yangu hii,”alisema.
Aidha Lameck alisema aprili,mwaka 2011 alitafuta nauli na
kwenda kumtafuta Baba yake na alifikia
kwa Mama yake mkubwa Jane huku
akifanyakazi katika Gereji moja inayoitwa kwa Remmy Shinyanga ambapo alifika
katika nyumba ya baba yake na hakufanikiwa kumpata lakini alipata nambari yake
ya simu na kumpigia akijitambulisha
lakini mzee huyo alimkataa katu katu kwa mara ya pili ambapo awali kwa mujibu
ya maelezo ya mama yake kuwa aliikataa mimba.
“Ninajuwa mzee anayo haki ya kukataa kwa sababu hajaniona
ama hatujaenda kupima DNA kama kweli mimi ni mwanawe ama hapana,mwezi Disemba
nilirudi Mbeya ambavyo kama
nilivyosimulia nilipo sasa na baada ya kumweleza mama alinisihi niache
kumtafuta baba zaidi niangalie maisha yangu,nimekata tamaa na sasa nahangahika
na maisha yangu,”alisema kwa majonzi Lameck.
Alipoulizwa kuwa
baada ya kusikia kifo cha kaka yake Kanumba
alikipokea vipi na kama aliwahi kwenda
katika msiba huo,alitikisa mabega kukataa kutokana na kukata tamaa ya
kukataliwa na Baba yake,na hakuwa na nauli ya kwenda huko,lakini ameahidi kuwa
ipo siku atakwenda moja kwa moja kwa baba yake akamkatae ana kwa ana,hivyo anatafuta nauli.
Hata hivyo kijana huyo alisema yeye anakipaji cha
kutunga tamthiliya na hadithi na kwamba aliwahi kwenda kujiunga
katika kikundi kimoja cha kuigiza kilichopo pembeni kidogo mwa Jiji la Mbeya,katika
mji mdogo wa Mbalizi kinachoongozwa na mtu aliyefahamika kwa jina la Mzushi
lakini alikwama kutokana na kushindwa kulipa hela ya kiingilio Sh.250,000
lakini ndoto yake amedai iko pale pale ya kurithi
kipaji cha kaka yake The Great
Kanumba.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment