Na Thompson Mpanji,Chunya
ASKARI Polisi wa kituo kidogo cha Polisi Mkwajuni wilayani Chunya, G.68.PC Jaffari Karume Mohamed (30), amefariki dunia wakati akipatiwa matibabu katika Hospitali Teule ya Mwambani,wilayani humo baada ya kupigwa risasi katika majibizano ya risasi na majambazi.
Imeelezwa kuwa tukio limetokea jana februari,6 majira ya saa 6 usiku ,jirani na klabu ya pombe cha Mwaulambo,Mwambani Klabu,wilayani Chunya baada ya majambazi hayo kudaiwa kufanya uharifu katika maeneo tofauti na kufanikiwa kupora zaidi ya Sh.Mil.2.2 katika kituo cha mafuta cha mfanyabiashara aliyetajwa kwa jina la Samora Muyombe walielekea Mkwajuni wakiwa na gari aina ya Toyota Colora yenye nambari za usajili T.227 BST iliyokuwa ikiendeshwa na Shaban Msule(33),Mbena,Mkazi wa makambakoLand Cruiser.
Walisema majambazi hayo yalipita maeneo ya Makongolosi na Saza wakijaribu kupora bila mafanikio na hatimaye kufika Mkwajuni marehemu Jaffari akiwa doria na askari wenzake waliokuwa wakifuatilia tukio hilo baada ya kupokea taarifa walifanikiwa kuwakuta vna kupambana nao na ndipo alipojeruhiwa kwa kupigwa risasi ubavu wa kulia na kukimbizwa Hospitali ambapo alifariki dunia akiwa anapatiwa matibabu.
Walisema baada ya polisi wa kituo cha Mkwajuni kupata taarifa hiyo waliweka mtego na kufanikiwa kuliona gari likipita jirani na kituo na baada ya kuwafuatilia walilikuta gari hilo limepaki jirani na klabu hiyo huku Dereva wa gari hilo akishuka kwenda kununua maji ya kunywa na ndipo mkuu wa kituo aliyefahamika kwa jina moja la Dominiki akiwa amevalia kiraia alimfuatilia lakini kabla ya kumfikia dereva huyo Askari polisi jaffari alishuka akiwa na bunduki na majambazi kumshtukia na kummiminia risasi.
Walisema polisi nao walijibu mashambulizi na kufanikiwa kumuuwa jambazi dereva Msule ambapo wengine watatu walifanikiwa kutoroka kwa miguu na kuliacha gari ambalo lipo katika kituo cha polisi Mkwajuni.
Kaimu Kamanda wa polisi Mkoa wa Mbeya,Mrakibu Mwandamizi wa polisi Barakael Masaki amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kudaiwa kuwa gari hilo limekamatwa lipo kituo cha polisi mkwajuni na mwili wa marehemu umehifadhiwa katika Hospitali Teule ya Wilaya ya Chunya ya Mwambani,Kata ya Mkwajuni ukisubiri taratibu nyingine za maziko ya kijeshi.
Kamanda Msaki alisema wamefanikiwa kukamata maganda tisa ya risasi aina ya SMG na SAR pamoja na risasi sita na kwamba msako mkali unaendelea chini ya uongozi wa Mkuu wa upelelezi wa makosa ya jinai Mkoa wa Mbeya Robert Mayala (SSP),askari polisi na wananchi ili kuwabaini na kuwakamata watuhumiwa waliohusika na tukio hilo.
ASKARI Polisi wa kituo kidogo cha Polisi Mkwajuni wilayani Chunya, G.68.PC Jaffari Karume Mohamed (30), amefariki dunia wakati akipatiwa matibabu katika Hospitali Teule ya Mwambani,wilayani humo baada ya kupigwa risasi katika majibizano ya risasi na majambazi.
Imeelezwa kuwa tukio limetokea jana februari,6 majira ya saa 6 usiku ,jirani na klabu ya pombe cha Mwaulambo,Mwambani Klabu,wilayani Chunya baada ya majambazi hayo kudaiwa kufanya uharifu katika maeneo tofauti na kufanikiwa kupora zaidi ya Sh.Mil.2.2 katika kituo cha mafuta cha mfanyabiashara aliyetajwa kwa jina la Samora Muyombe walielekea Mkwajuni wakiwa na gari aina ya Toyota Colora yenye nambari za usajili T.227 BST iliyokuwa ikiendeshwa na Shaban Msule(33),Mbena,Mkazi wa makambakoLand Cruiser.
Walisema majambazi hayo yalipita maeneo ya Makongolosi na Saza wakijaribu kupora bila mafanikio na hatimaye kufika Mkwajuni marehemu Jaffari akiwa doria na askari wenzake waliokuwa wakifuatilia tukio hilo baada ya kupokea taarifa walifanikiwa kuwakuta vna kupambana nao na ndipo alipojeruhiwa kwa kupigwa risasi ubavu wa kulia na kukimbizwa Hospitali ambapo alifariki dunia akiwa anapatiwa matibabu.
Walisema baada ya polisi wa kituo cha Mkwajuni kupata taarifa hiyo waliweka mtego na kufanikiwa kuliona gari likipita jirani na kituo na baada ya kuwafuatilia walilikuta gari hilo limepaki jirani na klabu hiyo huku Dereva wa gari hilo akishuka kwenda kununua maji ya kunywa na ndipo mkuu wa kituo aliyefahamika kwa jina moja la Dominiki akiwa amevalia kiraia alimfuatilia lakini kabla ya kumfikia dereva huyo Askari polisi jaffari alishuka akiwa na bunduki na majambazi kumshtukia na kummiminia risasi.
Walisema polisi nao walijibu mashambulizi na kufanikiwa kumuuwa jambazi dereva Msule ambapo wengine watatu walifanikiwa kutoroka kwa miguu na kuliacha gari ambalo lipo katika kituo cha polisi Mkwajuni.
Kaimu Kamanda wa polisi Mkoa wa Mbeya,Mrakibu Mwandamizi wa polisi Barakael Masaki amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kudaiwa kuwa gari hilo limekamatwa lipo kituo cha polisi mkwajuni na mwili wa marehemu umehifadhiwa katika Hospitali Teule ya Wilaya ya Chunya ya Mwambani,Kata ya Mkwajuni ukisubiri taratibu nyingine za maziko ya kijeshi.
Kamanda Msaki alisema wamefanikiwa kukamata maganda tisa ya risasi aina ya SMG na SAR pamoja na risasi sita na kwamba msako mkali unaendelea chini ya uongozi wa Mkuu wa upelelezi wa makosa ya jinai Mkoa wa Mbeya Robert Mayala (SSP),askari polisi na wananchi ili kuwabaini na kuwakamata watuhumiwa waliohusika na tukio hilo.
Hata
hivyo Kaimu Kamnada huyo ametoa wito kwa mtu ama watu wenye taarifa
kuhusu mahali walipo watu wanaodhaniwa kuhusika na tukio hilo watoe
taarifa ili wakamatwe na sheria iweze kuchukuwa mkondo wake vinginevyo
wajisalimishe.
No comments:
Post a Comment