Mshikamano wa Caritas na wananchi wanaoteseka kutokana na vita nchini Mali
Taarifa zinaonesha kwamba, kuna zaidi ya watu 9,000 waliokimbilia katika nchi jirani ilikutafuta hifadhi ya maisha yao na wanaendelea kuhudumiwa na wananchi katika maeneo haya. Lakini, kutokana na wingi wa watu na ukosefu wa rasilimali fedha, chakula na mablanketi, wahamiaji hawa wamejikuta wanakabiliana na hali ngumu zaidi. Wanawake na watoto ndio wanaoathirika zaidi kutokana na kinzani pamoja na migogoro ya kijamii inayoendelea sehemu mbali mbali za dunia.
Msaada uliotolewa na Caritas unalenga kutoa walau lishe kwa watoto wanaokabiliwa na utapiamlo wa kutisha, ambao umeongezeka kwa asilia sita pamoja na dawa za kudhibiti magonjwa ya milipuko.
No comments:
Post a Comment