Akizungumza na Shirika la Habari za Kimissionari, FIDES, Askofu Melchisedech Sikuli Paluku wa Jimbo Katoliki Butembo-Ben, mahali ambako Wamissionari watatu waliotekwa nyara walikuwa wanafanya shughuli zao za kichungaji anasema, kuna haja kwa watu kuvuta subira kwani kuna makuburi mawili yaliyopatikana yakiwa na miili kadhaa, lakini haijafahamika ikiwa kama kuna miili pia ya Mapadre waliotekwa nyara. Viongozi wa Kanisa wanaendelea kufanya uchunguzi wa kina ili kubainisha ukweli wa mambo.
Wamissionari waliotekwa nyara ni Padre Jean Pierre Ndulani, Padre Anselme Wasikundi pamoja na Padre Edmond Bamutute, walitekwa nyara hapo tarehe 21 Oktoba 2012 walipokuwa katika Parokia ya Notre Dame des Pauvres, Kilometa 70 kutoka Makao makuu ya Jimbo Katoliki la Butembo Beni, lililoko nchini DRC.
No comments:
Post a Comment