Translate

Sunday, September 8, 2013

TGNP WANAWAKE WAITAKA KATIKA KUWEKA BAYANA MASUALA YA WANAWAKE



Na Thompson Mpanji,Dar

WANAWAKE nchini wameendelea kupataza sauti zao  kwa tume ya Katiba kuwekwa wazi na kutamka bayana masuala yanayohusu wanawake katika rasimu ya katiba  mpya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ikiwemo  katika eneo la Tunu za Taifa  kwa kuongeza neno   Usawa wa jinsia.

Hayo yamesemwa  na mwezeshaji katika jukwaa la Katiba Ruth Meena   katika viwanja vya makao makuu ya Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP),Mabibo,jijini hapa wakati wa maadhimisho ya Tamasha la miaka  20 ya shirika hilo tangu kuanzishwa.

Meena amesema  katika Katiba mpya inayotarajiwa kuundwa ni muhimu kutoa kipaumbele na kuingizwa kmasuala ya wanawake   ambayo hayataleta mkanganyiko kwa namna yeyote ili mambo ya msingi yaendelea kuchukuliwa uzito. 

Mwezeshaji huyo amesema usawa wa jinsia lazima utiririke  katika katiba yote   kwani  ndiyo msingi mkuu huku akidai haki za wanawake  lazima zibainishwe kwa uwazi,haki za mtoto hasa wa kike ziwekwe bayana kwani  wanafahamu  muktadha wa jamii  katika  kumbagua mtoto wa kike.

Meena alisema mila na desturi  zinazokinzana   na wanawake  zibatilishe na katiba mpya iseme kwa uwazi,miiko watakayopewa viongozi watakawaongoza  ioneshe  kupinga ukatili  sanjari na vyama vya siasa  kupewa mipaka  katika kampeni kuhusu matumizi ya pesa ili nchi isije kuongozwa na  fedha chafu.

Awali kabla ya kuanza kwa mjadala wa  jukwaa la katiba ,vijana kutoka jukwaa la wanaharakati wanawake (WFF) kutoka  TGNP walitumbuiza kwa ngonjera  huku baadhi ya  washiriki wakishangilia  ubeti mmoja uliowavuita  wengi.

Akianzisha ubeti huo mmoja wa wanaharakati hao,Aisha Kijawala aliuliza  machangudoa wateja wake nani ambapo wenzake walijibu kuwa ni Mawaziri,Wabunge,Mapolisi  na wengine wengi ubeti uliowainua washiriki wote katika tamasha hilo la TGNP huku wakiwatuza fedha.

Mwisho.


No comments:

Post a Comment