Translate

Friday, March 8, 2013

Hospitali ya Peramiho inatoa matibabu bure agharamia usafiri na chakula wagonjwa wa Fistula



HOSPITALI ya Mtakatifu Joseph  Mission Peramiho inatangaza huduma ya matibabu ya ugonjwa wa fistula kwa akina mama bure  ikiwemo chakula na nauli  ya kumfikisha hospitali na kumrudisha.

Fistula ni ugonjwa unaopelekea mwanamke kuvuja mkojo  au haja kubwa au vyote kwa pamoja bila mgonjwa  kuweza kujizuia ambapo hutokea  baada ya kujifungua na madhara yake ni makubwa  ikiwa ni pamoja na kutengwa  na wenzi wao na jamii kwa ujumla kutokana na harufu mbaya ya mkojo na haja kubwa.

Katika taarifa yake   iliyosambazwa katika majimbo,parokia,makanisa mbalimbali ,Dkt.Gaudens Komba kwa niaba ya Mganga mkuu wa St.joseph’s Mission Hospital Peramiho amesema Hospitali ya misheni peramiho iliyoko wilayani songea,mkoani Ruvuma itaendesha mpango maalum wa kutoa matibabu kwa akina mama wenye fistula kuanzia mwezi aprili,29 hadi mei,11,2013.

Dkt.Komba alisema katika mpango huo wagonjwa wote watakaojitokeza watapatiwa huduma za nauli ya kumfikisha hospitali ya Peramiho,matibabu ya ugonjwa wa fistula bure,chakula bure akiwa hospitalini na nauli ya kumrudisha nyumbani baada ya matibabu.

Mganga huyo alisema  kwa wale wenye matatizo hayo wanaweza kuwasiliana na Hospitali ya peramiho kupitia nambari za simu ili kupangiwa utaratibu:0754/0784/0715 662029 ama wagonjwa wafike Hospitali ya peramiho kuanzia aprili,28,2013 tayari kwa matibabu.

Mwisho.

No comments:

Post a Comment