Translate

Friday, April 15, 2011

Kibaka aliyeiba Sh.10,000 yang'angania mkononi,apooza miguu na mkono

Na Thompson Mpanji,Mbozi

KIJANA mmoja mpiga debe wa magari yanayofanya safari zake Kamsamba-Mlowo wilayani Mbozi amekumbwa na mkasa wa aina yake baada ya  kudaiwa kuiba fedha  ambayo baadaye ilikutwa imenasa katika mkono wake wa kulia na miguu yote miwili kupooza huku akiwa amelazwa katika zahanati moja wilayani humo.

Tukio hilo la aina yake limetokea ,aprili,10 majira ya mchana baada ya kijana huyo aliyefahamika kwa jina la Jacob Jengela kuokota fedha Sh.10,000 inayodaiwa kudondoshwa na  muhudumu wa kituo cha kuuza  mafuta kinachomilikiwa na mfanyabiashara aliyetajwa kwa jina moja la Chaula kilichopo maeneo ya Mlowo wilayani humo na kuikanyaga kwa mguu baada ya kuiona na baadaye kuificha mkononi ambapo mhudumu huyo baada ya kushtuka alipiga kelele ya kuibiwa na kijana huyo aliamua kutimua mbio lakini mbio zake ziliishia sakafuni baada ya kudondoka ghafla na kupooza.

Mashuhuda wa tukio hilo wamesema kuwa baada ya kijana huyo kuanguka chini huku akiwa anajizoa zoa na kuonekana anashindwa kunyanyuka wananchi wenye hasira kali walimvamia na kutaka kumchoma moto lakini askari polisi wa kituo kidogo cha Polisi cha mlowo walifanikiwa kumuokoa na kumkimbiza katika zahanati iliyotajwa kwa jina la Tumaini kwa ajili ya  uchunguzi na matibabu zaidi.

Aidha  inadaiwa kuwa chanzo cha kuanguka na kupooza miguu yote miwili na mkono wa kulia ulionasa noti hiyo  ya sh.10,000 iliyoendelea kung'ang'ania  ikiwa imenasa mkononi huku akiwa amelazwa  katika zahanati hiyo  hadi kipindi hiki kinaporuka hewani ni kutokana na imani inayohusishwa na masuala ya kishirikana kuwa fedha hiyo ilikuwa imetegwa.

Hata hivyo kipindi hiki baada ya kusasiliana na mmiliki wa kituo hicho aliyetajwa kwa jina moja la Chaula amesema anadhani kijana huyo alikuwa na matatizo ya maradhi ya muda mrefu kwani baada ya yeye kupokea taarifa hiyo alimuuliza mhuhudu ambaye alidai hakumbuki kama alidondosha fedha hiyo.

Mwisho.

No comments:

Post a Comment